SEASON 7: SEHEMU YA 13
Daniel Swai na Irene
wakawasili katika makazi ya
Monica wakashuka katika taksi
wakaingia ndani.Monica
akataarifiwa kufika kwao
“ karibuni sana” akasema
Monica na kukumbatiana na
Daniel kisha akasalimiana na Irene
“ Daniel kimya chako
kimenishangaza sana.Si kawaida
yako kukaa kimya namna hiyo bila
hata kunijulia hali.Kuna tatizo
lolote? Akauliza Monica
“ Hakuna tatizo
Monica.Nilikuwa na vijisafari vya
hapana pale ndiyo maana umeona
kimya namna hii.”
“ Simu nayo ilikuwa safari?
Monica akauliza na wote
wakacheka
“I’m sorry for that Monica.It
wont happen again” akasema
Daniel
“ Haya niambie.Naona
umeniletea mrembo leo” akasema
Monica na kwa mbali Irene
akajilazimisha kutabasamu
“ Anaita Irene maboko ni
rafiki yangu anafanya kazi ikulu.”
Akasema Daniel
“ Irene huyu anaitwa Monica
benedict ni rafiki yangu
mkubwa.Tumekuwa marafiki toka
tukiwa watoto wadogo na hadi
sasa tuko pamoja.Ni mtu wangu wa
karibu sana na ndiyo maana
umeona analalama kwa nini
sijawasiliana naye kwa siku
kadhaa.” Akasema Daniel.Monica
akainuka na kwenda kumpa
mkono Irene
“Karibu sana Irene.Nafurahi
kukufahamu” akasema Monica
“ Monica nimekuja kwako
nina shida nahitaji msaada wako.”
“ Sema shida yako Daniel.”
“ Irene ana matatizo na
anahitaji sehemu salama ya
kujihifadhi kwa muda mfupi
wakati tatizo lake likitafutiwa
ufumbuzi.Kwa kuwa ni rafiki
yangu na mimi ndiye tegemeo lake
nimeona nije hapa nikuombe Irene
akae hapa kwako kwani ni sehemu
salama na kuna ulinzi wa kutosha
hadi hapo suala lake litakapokuwa
limetatuliwa.Naomba sana Monica”
akasema Daniel.Monica
akatabasamu na kusema
“ Daniel hapa ni nyumbani
kwako na hupaswi kuomba.Irene
karibu sana utaishi hapa.Nyumba
hii ni kubwa na bado ninahitaji
watu wa kuishi nao humu.Ulinzi
hapa ni wa uhakika na hupaswi
kuwa na hofu yoyote.Daniel
amekuleta sehemu sahihi”
akasema Monica na wote
wakacheka.Irene akainuka na
kwenda kumpa mkono Monica
akamshukuru
“Monica nashukuru sana kwa
msaada wako huu.Ahsante kwa
kunikaribisha niishi hapa kwako
kwa muda” akasema Irene
“Baada ya kulikubali ombi
lako ni wakati sasa wa kulifahamu
tatizo la Irene” akasema Monica
“ Monica tatizo la Irene ni
binafsi kwa hiyo itoshe tu
kumsaidia sehemu ya kukaa.Hayo
mengine sidhani kama yana
umuhimu ” akasema Daniel
“ Daniel hili si tatizo binafsi
tena.Tayari limekuwa tatizo letu
sote.Nimekubali kumsaidia Irene
kwa moyo mmoja kwa hiyo
nitahitaji kufahamu Irene ana
tatizo gani? Akauliza Monica
“ Monica tatizo la Irene ni
kubwa na tayari ninalishughulikia
kwa hiyo nitakufahamisha pale
ufumbuzi wake utakapokuwa
umepatikana” akasema Daniel
“ Daniel haijawahi kutokea
ukanificha kitu chochote hata zile
siri zako kubwa umekuwa
unanieleza.Thats because you trust
me.Kama umeniamini ukanieleza
mambo yako yote,niamini pia
katika hili” Akasema
Monica.Daniel akatazamana na
Irene halafu akamwambia
“I trust her with my life.Hana
tatizo hata akifahamu” Irene
akatikisa kichwa kukubaliana na
Daniel
“ Kama nilivyokueleza awali
kwamba Irene anafanya kazi
ikulu.Ndiye anayehusika na mfumo
wote wa ulinzi wa mtandao wa
kompyuta wa ikulu.Katika
shughuli zake hizo alifanikiwa
kuyanasa maongezi ya simu kati ya
rais na mkuu wa majeshi
wakizungumzia kuhusu shambulio
lile lililotokea jana.Mazungumzo
hayo aliyanasa kabla shambulio
hilo halijatokea na hii inatoa picha
kwamba rais na mkuu wa majeshi
walifahamu kuhusu kutokea kwa
shambulio hilo kabla .Mapema leo
nikiwa na Irene pale Tiger hotel
walikuja watu wawili wakamtaka
Irene aongozane nao lakini
nilipambana nao kisha
tukafanikiwa kuondoka.Tulipofika
nyumbani kwao tukakuta nyumba
imevurugwa mno,mfanyakazi wa
ndani amepigwa risasi na
wazaziwake hawajulikani
walipo.Tukiwa pale wakatokea
wau wawili tukapambana nao na
kufanikiwa kutoroka ndipo Irene
aliponieleza kila kitu kilichotokea”
Akasema Daniel halafu
akamuomba Irene amuwekee
Monica rekodi ile aisikilize.Monica
akaisikiliza na kuwatazama Daniel
na Irene kwa mshangao
“ Is this true?!! Akauliza akiwa
haamini alichokisikia
“ Yes .Its true” akajibu Irene
“ Jesus Christ !! akasema
Monica
“ Irene una hakika hawa
wanaozungumza humu ni rais
Ernest na mkuu wa majeshi? Siyo
kwamba kuna watu wametumia
teknolojia wakatengeneza sauti
hizi? Akauliza Monica
“Hiki si kitu cha kutengeneza
Monica.Hizi ni sauti za kweli za
rais na mkuu wa
majeshi.Niliyanasa mimi
mwenyewe kwa kutumia simu
yangu.”akasema Irene
“ Dah ! nimeishiwa nguvu”
akasema Monica
“Pembeni ya maiti ya
mfanyakazi wa ndani wa akina
Irene kuliachwa karatasi hii” Danel
akaitoa karatasi ile akampa
Monica akaisoma
“Nilipiga namba hizo za simu
nikaongea na hao jamaa
wakasisitiza kwamba wanataka
kuzungumza na Irene na si mtu
mwingine kisha wakatuma video
hii” akasema Daniel na
kumuonyesha Monica video ile ya
mama yake Irene akilia akimtaka
Irene amsaidie.Monica
akashindwa kujizuia akainuka na
kwenda kumkumbatia Irene wote
wawili wakilia
“ Pole sana Irene.Hili ni tatizo
kubwa lakini nakuahidi kwamba
litakwisha.Utawapata tena wazazi
wako” Akasema Monica na kufuta
machozi halafu akasema
“ Nina safari ya kuelekea
Congo kwa ajili ya kuhudhuria
mazishi ya mke wa rais wa Congo
na kama isingekuwa hivyo
ningeahirisha safari hiyo kwa ajili
ya suala hili lakini si muda mrefu
toka sasa atakuja hapa mtu mmoja
anaitwa Austin January.Huyu ni
mpele..”
“ Monica hebu subiri
kidogo.Umesema Austin January?!
Akauliza Daniel
“ Ndiyo.Do you know him?
‘ Yes but that man is dead!!
Akasema Daniel
“ He’s not dead.He’s alive na
muda sio mrefu sana toka sasa
atafika hapa.” Akasema
Monica.Daniel alionekana
kushangaa sana
“ Monica hayo unayosema ni
ya kweli?
“ Ni kweli kabisa Danny”
akajibu Monica
“ he must be a ghost.Austin
January ninafahamiana naye na
alifariki nchini Somalia miaka
kadhaa iliyopita.Nashangaa
kuniambia kwamba yuko hai na
yuko hapa Tanzania.”
“ Daniel niamini
nikwambiavyo kwamba Austin
yupo na atakuja hapa utaonana
naye.Austin ni mpelelezi
mashuhuri na atalishughulikia
suala hili .Irene usijali suala hili
litakwisha na wazazi wako
utawapata.” Akasema Monica na
kuwaomba akina Daniel
wamsubiri pale akamalizie
kujiandaa kwa ajili ya safari.
“ Irene,huyo Austin January
aliyemsema Monica ni mtu hatari
sana .Amewahi kufanya kazi katika
idara ya ujasusi na sote tuliamini
kwamba alifariki nchini Somalia
kumbe yuko hai.Haya ni maongozi
ya Mungu kwani suala hili sasa
limefika katika mikono salama na
litashughulikiwa ipasavyo” Daniel
akamwambia Irene
“ Thanx Daniel.Huyu rafiki
yako Monica anafahamu kama
wewe ni mpelelezi? Akauliza Irene
“ Hafahamu chochote.Hakuna
miongoni mwa marafiki zangu
anayefahamu suala hili ni wewe tu
ambaye nimekueleza ukweli.Ila
Austin ananifahamu vyema”
akasema Daniel
“Daniel kuna jambo limekuwa
linaniumiza sana kichwa
changu.Unadhani rais anahusika
katika lile tukio? Akauliza
“ Ni mapema mno kusema
chochote kwa sasa hadi hapo
uchunguzi utakapofanyika
tutafahamu kila kitu” akasema
Daniel
Monica aliingia chumbani
kwake kwa dhumuni la kumalizia
kujiandaa kwa safari lakini
akajikuta akikaa kitandani
kutokana na mawazo mengi
aliyokuwa nayo
“ Ernest Mkasa .Is this the
president I voted? Kwa ushahidi
huu alionao Irene ni wazi rais
anahusika na mashambulio haya
mawili.Oh my Gosh ! huyu mtu
anaipeleka wapi nchi hii?
Ningekuwa na uwezo kama wa
akina Austin ningehakikisha
anafikishwa mbele ya sheria na
anahukumuwa kifo.Ameua watu
wengi wasiona hatia.I hate him so
much” akawaza Monica
Daniel Swai na Irene
wakawasili katika makazi ya
Monica wakashuka katika taksi
wakaingia ndani.Monica
akataarifiwa kufika kwao
“ karibuni sana” akasema
Monica na kukumbatiana na
Daniel kisha akasalimiana na Irene
“ Daniel kimya chako
kimenishangaza sana.Si kawaida
yako kukaa kimya namna hiyo bila
hata kunijulia hali.Kuna tatizo
lolote? Akauliza Monica
“ Hakuna tatizo
Monica.Nilikuwa na vijisafari vya
hapana pale ndiyo maana umeona
kimya namna hii.”
“ Simu nayo ilikuwa safari?
Monica akauliza na wote
wakacheka
“I’m sorry for that Monica.It
wont happen again” akasema
Daniel
“ Haya niambie.Naona
umeniletea mrembo leo” akasema
Monica na kwa mbali Irene
akajilazimisha kutabasamu
“ Anaita Irene maboko ni
rafiki yangu anafanya kazi ikulu.”
Akasema Daniel
“ Irene huyu anaitwa Monica
benedict ni rafiki yangu
mkubwa.Tumekuwa marafiki toka
tukiwa watoto wadogo na hadi
sasa tuko pamoja.Ni mtu wangu wa
karibu sana na ndiyo maana
umeona analalama kwa nini
sijawasiliana naye kwa siku
kadhaa.” Akasema Daniel.Monica
akainuka na kwenda kumpa
mkono Irene
“Karibu sana Irene.Nafurahi
kukufahamu” akasema Monica
“ Monica nimekuja kwako
nina shida nahitaji msaada wako.”
“ Sema shida yako Daniel.”
“ Irene ana matatizo na
anahitaji sehemu salama ya
kujihifadhi kwa muda mfupi
wakati tatizo lake likitafutiwa
ufumbuzi.Kwa kuwa ni rafiki
yangu na mimi ndiye tegemeo lake
nimeona nije hapa nikuombe Irene
akae hapa kwako kwani ni sehemu
salama na kuna ulinzi wa kutosha
hadi hapo suala lake litakapokuwa
limetatuliwa.Naomba sana Monica”
akasema Daniel.Monica
akatabasamu na kusema
“ Daniel hapa ni nyumbani
kwako na hupaswi kuomba.Irene
karibu sana utaishi hapa.Nyumba
hii ni kubwa na bado ninahitaji
watu wa kuishi nao humu.Ulinzi
hapa ni wa uhakika na hupaswi
kuwa na hofu yoyote.Daniel
amekuleta sehemu sahihi”
akasema Monica na wote
wakacheka.Irene akainuka na
kwenda kumpa mkono Monica
akamshukuru
“Monica nashukuru sana kwa
msaada wako huu.Ahsante kwa
kunikaribisha niishi hapa kwako
kwa muda” akasema Irene
“Baada ya kulikubali ombi
lako ni wakati sasa wa kulifahamu
tatizo la Irene” akasema Monica
“ Monica tatizo la Irene ni
binafsi kwa hiyo itoshe tu
kumsaidia sehemu ya kukaa.Hayo
mengine sidhani kama yana
umuhimu ” akasema Daniel
“ Daniel hili si tatizo binafsi
tena.Tayari limekuwa tatizo letu
sote.Nimekubali kumsaidia Irene
kwa moyo mmoja kwa hiyo
nitahitaji kufahamu Irene ana
tatizo gani? Akauliza Monica
“ Monica tatizo la Irene ni
kubwa na tayari ninalishughulikia
kwa hiyo nitakufahamisha pale
ufumbuzi wake utakapokuwa
umepatikana” akasema Daniel
“ Daniel haijawahi kutokea
ukanificha kitu chochote hata zile
siri zako kubwa umekuwa
unanieleza.Thats because you trust
me.Kama umeniamini ukanieleza
mambo yako yote,niamini pia
katika hili” Akasema
Monica.Daniel akatazamana na
Irene halafu akamwambia
“I trust her with my life.Hana
tatizo hata akifahamu” Irene
akatikisa kichwa kukubaliana na
Daniel
“ Kama nilivyokueleza awali
kwamba Irene anafanya kazi
ikulu.Ndiye anayehusika na mfumo
wote wa ulinzi wa mtandao wa
kompyuta wa ikulu.Katika
shughuli zake hizo alifanikiwa
kuyanasa maongezi ya simu kati ya
rais na mkuu wa majeshi
wakizungumzia kuhusu shambulio
lile lililotokea jana.Mazungumzo
hayo aliyanasa kabla shambulio
hilo halijatokea na hii inatoa picha
kwamba rais na mkuu wa majeshi
walifahamu kuhusu kutokea kwa
shambulio hilo kabla .Mapema leo
nikiwa na Irene pale Tiger hotel
walikuja watu wawili wakamtaka
Irene aongozane nao lakini
nilipambana nao kisha
tukafanikiwa kuondoka.Tulipofika
nyumbani kwao tukakuta nyumba
imevurugwa mno,mfanyakazi wa
ndani amepigwa risasi na
wazaziwake hawajulikani
walipo.Tukiwa pale wakatokea
wau wawili tukapambana nao na
kufanikiwa kutoroka ndipo Irene
aliponieleza kila kitu kilichotokea”
Akasema Daniel halafu
akamuomba Irene amuwekee
Monica rekodi ile aisikilize.Monica
akaisikiliza na kuwatazama Daniel
na Irene kwa mshangao
“ Is this true?!! Akauliza akiwa
haamini alichokisikia
“ Yes .Its true” akajibu Irene
“ Jesus Christ !! akasema
Monica
“ Irene una hakika hawa
wanaozungumza humu ni rais
Ernest na mkuu wa majeshi? Siyo
kwamba kuna watu wametumia
teknolojia wakatengeneza sauti
hizi? Akauliza Monica
“Hiki si kitu cha kutengeneza
Monica.Hizi ni sauti za kweli za
rais na mkuu wa
majeshi.Niliyanasa mimi
mwenyewe kwa kutumia simu
yangu.”akasema Irene
“ Dah ! nimeishiwa nguvu”
akasema Monica
“Pembeni ya maiti ya
mfanyakazi wa ndani wa akina
Irene kuliachwa karatasi hii” Danel
akaitoa karatasi ile akampa
Monica akaisoma
“Nilipiga namba hizo za simu
nikaongea na hao jamaa
wakasisitiza kwamba wanataka
kuzungumza na Irene na si mtu
mwingine kisha wakatuma video
hii” akasema Daniel na
kumuonyesha Monica video ile ya
mama yake Irene akilia akimtaka
Irene amsaidie.Monica
akashindwa kujizuia akainuka na
kwenda kumkumbatia Irene wote
wawili wakilia
“ Pole sana Irene.Hili ni tatizo
kubwa lakini nakuahidi kwamba
litakwisha.Utawapata tena wazazi
wako” Akasema Monica na kufuta
machozi halafu akasema
“ Nina safari ya kuelekea
Congo kwa ajili ya kuhudhuria
mazishi ya mke wa rais wa Congo
na kama isingekuwa hivyo
ningeahirisha safari hiyo kwa ajili
ya suala hili lakini si muda mrefu
toka sasa atakuja hapa mtu mmoja
anaitwa Austin January.Huyu ni
mpele..”
“ Monica hebu subiri
kidogo.Umesema Austin January?!
Akauliza Daniel
“ Ndiyo.Do you know him?
‘ Yes but that man is dead!!
Akasema Daniel
“ He’s not dead.He’s alive na
muda sio mrefu sana toka sasa
atafika hapa.” Akasema
Monica.Daniel alionekana
kushangaa sana
“ Monica hayo unayosema ni
ya kweli?
“ Ni kweli kabisa Danny”
akajibu Monica
“ he must be a ghost.Austin
January ninafahamiana naye na
alifariki nchini Somalia miaka
kadhaa iliyopita.Nashangaa
kuniambia kwamba yuko hai na
yuko hapa Tanzania.”
“ Daniel niamini
nikwambiavyo kwamba Austin
yupo na atakuja hapa utaonana
naye.Austin ni mpelelezi
mashuhuri na atalishughulikia
suala hili .Irene usijali suala hili
litakwisha na wazazi wako
utawapata.” Akasema Monica na
kuwaomba akina Daniel
wamsubiri pale akamalizie
kujiandaa kwa ajili ya safari.
“ Irene,huyo Austin January
aliyemsema Monica ni mtu hatari
sana .Amewahi kufanya kazi katika
idara ya ujasusi na sote tuliamini
kwamba alifariki nchini Somalia
kumbe yuko hai.Haya ni maongozi
ya Mungu kwani suala hili sasa
limefika katika mikono salama na
litashughulikiwa ipasavyo” Daniel
akamwambia Irene
“ Thanx Daniel.Huyu rafiki
yako Monica anafahamu kama
wewe ni mpelelezi? Akauliza Irene
“ Hafahamu chochote.Hakuna
miongoni mwa marafiki zangu
anayefahamu suala hili ni wewe tu
ambaye nimekueleza ukweli.Ila
Austin ananifahamu vyema”
akasema Daniel
“Daniel kuna jambo limekuwa
linaniumiza sana kichwa
changu.Unadhani rais anahusika
katika lile tukio? Akauliza
“ Ni mapema mno kusema
chochote kwa sasa hadi hapo
uchunguzi utakapofanyika
tutafahamu kila kitu” akasema
Daniel
Monica aliingia chumbani
kwake kwa dhumuni la kumalizia
kujiandaa kwa safari lakini
akajikuta akikaa kitandani
kutokana na mawazo mengi
aliyokuwa nayo
“ Ernest Mkasa .Is this the
president I voted? Kwa ushahidi
huu alionao Irene ni wazi rais
anahusika na mashambulio haya
mawili.Oh my Gosh ! huyu mtu
anaipeleka wapi nchi hii?
Ningekuwa na uwezo kama wa
akina Austin ningehakikisha
anafikishwa mbele ya sheria na
anahukumuwa kifo.Ameua watu
wengi wasiona hatia.I hate him so
much” akawaza Monica