Rafiki yangu ni Wakala wa huduma za kifedha kwa mitandao ya simu ila katapeliwa kwa njia hii

Rafiki yangu ni Wakala wa huduma za kifedha kwa mitandao ya simu ila katapeliwa kwa njia hii

Cancellation ipo ENDAPO umekosea namba ya wakala wa ilo eneo ulilopo ila hapo kwa hapo namba yabwakala ndo iyo you will never ,jaribu kurisk elfu mbili toa andika namba ya wakala wa simiyu alafu fanya cancellation uone kama haijarudi mi imeshanitokea ikarud nikawaza aina iyo ya kuzulumu 2019 ila naona watu ndo wanaijua leo
Ukikosea hela kutoa kwa wakala inarudi ndio ila mpaka wakala adhibitishe kuwa muamala huo haukua halali ukiona umerudishiwa hivyo jua kuwa wakala kashajulishwa pia, ingekuwa ndio hivyo ilivyo rahisi kurejesha muamala si utapeli ungekuwa mkubwa sana? Fikiria mteja anakuja anakuambia anatoa hela anachukua code anamtumia mtu wa mbali anatoa halafu anakuambia tayari na jina anakutajia sasa hapo mhudumu utajulia wapi kuwa hela imetolewa mtu akiwa wapi? Halafu baada ya dk kadhaa anacancel muamala.
 
Unapotuma pesa kwa code ya wakala maana yake ni kwamba pesa umeitoa, na si kwamba umetuma, hivyo huwezi kurudishiwa pesa amabyo umeshachukua cash physically, hiyo haiwezekani, waliofanya huo utapeli ni hao hao voda, otherwise hata mimi si naweza kwenda kwenye kibamda chochote, nikatoa hela napewa cash then nasepa na kucancel muamala, matapeli ni hao voda, akomae nao.
inawezekana endapo mtoaji yupo mkoa mwingine..anapigia simu voda kuwa amekosea kutoa kwenye kuingiza namba za wakala...Voda wakiangalia jamaa yupo Namanga halafu dakika 2 zilizopita pesa katolea ipilinya Mtwara kwahyo wanamrudishia.
Wakala huwezi kulalamika kwasababu hutakiwi kumfanyia mtu muamala bila yeye kuwa na simu.
 
Kiukweli inatakiwa voda waweke mfumo wa kutoruhusu miamala ya mbali automatically ili kuwalinda mawakala.
Otherwise tutaendelea kupigwa.
 
Bob hawez rudisha kienyeji. Na zile logbook kuna kampuni hazina je utaweka wap details za mteja?

Mteja kaja kasema anatoa hela lakini kumbe mtoaji yuko mbali ww utamkaguaje? Lazima kampuni ikupigie simu kuhakiki kama ni kweli kuna mualama umeingia kimakosa kwenye acc yako.
Wabongo ni wabishi na wataibiwa sana hizo ni huduma za ki Bank alafu unataka watu wazifanye kienyeji mwambie mteja akuonyeshe SMS yake ya muamala
 
Ukikosea hela kutoa kwa wakala inarudi ndio ila mpaka wakala adhibitishe kuwa muamala huo haukua halali ukiona umerudishiwa hivyo jua kuwa wakala kashajulishwa pia, ingekuwa ndio hivyo ilivyo rahisi kurejesha muamala si utapeli ungekuwa mkubwa sana? Fikiria mteja anakuja anakuambia anatoa hela anachukua code anamtumia mtu wa mbali anatoa halafu anakuambia tayari na jina anakutajia sasa hapo mhudumu utajulia wapi kuwa hela imetolewa mtu akiwa wapi? Halafu baada ya dk kadhaa anacancel muamala.
Asante
 
siku zote tafrani kama hiyo ikitokea kinachoangaliwa hapo ni location

jamaa alifanya kosa kumpa code mtu aliyeko mbali na ofisi yake atoe pesa, kwasababu huyo mtu akipiga simu kuisitisha hiyo pesa basi wahudumu kwa wateja ni rahisi kuizuia pasipo hata kufanya mawasiliano na wewe uliye pokea kwakua distance inaonesha huyo mteja hakua ofisin kwako probably ni mkoa tofauti na wako
Kodi za wakala zipo wazi kutumiwa mbali hakukwepeki kwani mtu akijafanya anabonyeza simu akamtumia mtu aliyembali akaforwadiwa sms utajuaje
 
Hapo voda ndio wenye makosa
Hapana, sheria ya voda ni hivi, kama aliyetoa pesa yupo mnara mmoja na wewe ,akipiga kusem amekosea pesa hairudishwi hata kama kakosea kweli..

Ila kama aliyetoa yupo mnara tofauti na wewe pesa inarudishwa, na ndiyo maana mawakala wanasisitizwa wahakikishe anayetoa ela ndiyo yule anayekuja kibandani, na sio mtu wa mbali..
 
Transaction za mbali kivipi? Wakati pesa inaweza kutumwa kutoka eneo lolote. Mimi niko Dar, anayenitumia pesa yuko Mara labda, nikaomba code ya wakala aliyeko Dar. Hapo tatizo nn, mpk useme transaction za mbali?
Nani kakwambia kwa wakala unatuma pesa.??

Kwa wakala ni unatoa au unaingiza pesa kwenye simu yako wewe uliyeenda kwa wakala(ndiyo sheria), ..
 
Hapana, sheria ya voda ni hivi, kama aliyetoa pesa yupo mnara mmoja na wewe ,akipiga kusem amekosea pesa hairudishwi hata kama kakosea kweli..

Ila kama aliyetoa yupo mnara tofauti na wewe pesa inarudishwa, na ndiyo maana mawakala wanasisitizwa wahakikishe anayetoa ela ndiyo yule anayekuja kibandani, na sio mtu wa mbali..
lakini pesa hurudishwa baada ya saa 72
 
Halafu huyo rafiki yako ndo wewe sasa, pole sana mkuu bila shaka una la kujifunza hapo.
 
Unapotuma pesa kwa code ya wakala maana yake ni kwamba pesa umeitoa, na si kwamba umetuma, hivyo huwezi kurudishiwa pesa amabyo umeshachukua cash physically, hiyo haiwezekani, waliofanya huo utapeli ni hao hao voda, otherwise hata mimi si naweza kwenda kwenye kibamda chochote, nikatoa hela napewa cash then nasepa na kucancel muamala, matapeli ni hao voda, akomae nao.
Nilishakosea ikarudishwa , nilikosea namba ya wakala
 
inawezekana endapo mtoaji yupo mkoa mwingine..anapigia simu voda kuwa amekosea kutoa kwenye kuingiza namba za wakala...Voda wakiangalia jamaa yupo Namanga halafu dakika 2 zilizopita pesa katolea ipilinya Mtwara kwahyo wanamrudishia.
Wakala huwezi kulalamika kwasababu hutakiwi kumfanyia mtu muamala bila yeye kuwa na simu.
Hahahah, huo bado ni utapeli wa Voda, you know why?, wakati mtoaji pesa wa Ipilinya anatoa pesa kwa wakala aliye Namanga hiyo system ilikuwa imechanganyikiwa hadi ikaruhusu huo muamala wakati hauruhusiwi?!! Hahahahahah. Unajua wateja wengine ni waongo, anakwambia simu ninayo mimi, anakutajia hadi jina na kiasi alichotoa, kumbe aliyetoa yupo nanjilinji huko, sasa hiyo kazi ya kuomba wateja simu zao ili wazikague kama ndio yenyewe aliyetoa na si mtu wa mkoa mwingine ni ngumu sana!!!! Huu ni utapeli, mtu katoa pesa hapaswi kurudishiwa bila kumtaarifu wakala, hata kama yupo mwezini huyo aliyetoa!!!!
 
Aendelee kukatwa mshahara Ili siku nyingine atakuwa na akili.
Mfanyakazi akiingiza shoti usimfukuze mkate mshahara Ili apate pain next time atakuwa makini
 
Hahahah, huo bado ni utapeli wa Voda, you know why?, wakati mtoaji pesa wa Ipilinya anatoa pesa kwa wakala aliye Namanga hiyo system ilikuwa imechanganyikiwa hadi ikaruhusu huo muamala wakati hauruhusiwi?!! Hahahahahah. Unajua wateja wengine ni waongo, anakwambia simu ninayo mimi, anakutajia hadi jina na kiasi alichotoa, kumbe aliyetoa yupo nanjilinji huko, sasa hiyo kazi ya kuomba wateja simu zao ili wazikague kama ndio yenyewe aliyetoa na si mtu wa mkoa mwingine ni ngumu sana!!!! Huu ni utapeli, mtu katoa pesa hapaswi kurudishiwa bila kumtaarifu wakala, hata kama yupo mwezini huyo aliyetoa!!!!
Huo sasa sio utapeli kwa upande wa voda labda useme ni system mbovu ambayo matapeli ndo wanaitake advantage..lakini inawezekana Technicallity za kufanya miamala ikatae kwasababu ya location ni ngumu kuimplement au gharama sana lakini pia Voda kwa maelekezo wanakataza mawakala kutuma hela kwa mteja asiye kibandani Hii nahisi ni ili mapato ya float za sehem husika ziende kwa investors/shops za hiyo sehemu au ni njia ya kujua statistics za mapato ya MPesa....sasa mawakala wakikiuka hiyo sheria Voda wanafanya kama kupurnish kwa kurudisha hela bila kuwataarifu ili wawe waoga na wawe makini kutokiuka hayo maelekezo
 
Huo sasa sio utapeli kwa upande wa voda labda useme ni system mbovu ambayo matapeli ndo wanaitake advantage..lakini inawezekana Technicallity za kufanya miamala ikatae kwasababu ya location ni ngumu kuimplement au gharama sana lakini pia Voda kwa maelekezo wanakataza mawakala kutuma hela kwa mteja asiye kibandani Hii nahisi ni ili mapato ya float za sehem husika ziende kwa investors/shops za hiyo sehemu au ni njia ya kujua statistics za mapato ya MPesa....sasa mawakala wakikiuka hiyo sheria Voda wanafanya kama kupurnish kwa kurudisha hela bila kuwataarifu ili wawe waoga na wawe makini kutokiuka hayo maelekezo
Sijaongelea wakala kutuma pesa kwa mtu asiye kibandani, nimeongelea Voda kurudisha pesa kisa mtu yupo mkoa mwingine, na nimekueleza ni ngumu kwa wakala kukaguansimu kujua kama kweli aliye mbele yake ndie katoa na si mtu wa mkoa mwingine ametoa na anamtumia huyo aliye mbele kudanganya, sasa kuna ugumu upi wa Voda kumtaarifu wakala kabla ya kuirudisha, ugumu uko wapi kama si utapeli tu?
 
Ela ukishatoa kupitia code ya wakala ukiwapigia voda wa cancel au umekosea lazima voda wa mpigie wakala mwenyewe code husika Ku hakiki then ndio wanarudsha mi ni wakala kuna jamaa alikosea akatoa kwangu na ayupo hapo akawapigia voda na voda wakapga kwangu kuhakiki kama ni kweli kakosea au anafanya ujanja
 
Back
Top Bottom