Raha na Vioja vya disko na mikusanyiko ya kidini shule za bweni(Boarding Schools)

Raha na Vioja vya disko na mikusanyiko ya kidini shule za bweni(Boarding Schools)

Old is Gold Disko nimeanza ingia nipo shule ya msingi nyimbo zilizobamba ni za Awilo lolongomba,wenge bcbg na nk sekondari ndo ikawa zaidi kwenye kuhudhuria mambo ya TYCS hasa zile za kikanda ambazo mnaweka kambi na kukutana na shule mbalimbali hapo usipong'oa mwanamke we ni kilaza(baba jesca voice) huku tukinogesha na ile kauli mbiu ya "Mapendo" watu mnaitikia "Daima" huku taratibu viuno mmeviweka sawa kwa ajili ya kuyarudi
 
Me sikusoma zamani sana, hivyo shule yetu watu walikuwa na simu. Nakumbuka disco moja ile mida ya nyimbo za mwisho ndo muda wa kupeana namba za simu.. msichana mmoja akampa jamaa namba ya baba yake.. kilichofuatia.......
 
Kuna mambo yanaenda na umri tenda haki kwa umri wako ukijibana bana xana ukiwa shule/chuo ukimaliza chuo ndo unajiona sasa uko huru kufanya mambo yako kumbe unakuwa ndo umeshachelewa hayo ilitakiwa uwe umeyafanya huko ulipotoka huko n ukubwan kupambana na majukum ili kuwa mama au baba bora kwa wale waliomaliza michezo huwa na dspln
 
Dah.. Hii inanikumbusha sana EASTER CONFERENCE za TYCS tulikuwa tunafanyia Marangu Sec. YCS toka Sekondari schools za Moshi tunakutana pale.. Ushindani mkubwa ulikwa kwa Umbwe High school na giants wengine kama St. James Seminary, Old Moshi, Tarakea high school, Lyamungo na wenyeji wenyewe Marangu sec..
Sitasahau siku nlivochana pale RAP ya Yesu nliyoiita Son of God beat ya break yo neck by Busta Rhymes nkajipatia mtoto mmoja mkali sana kutoka Kiraeni Sec.
Plus nawakumbuka sana watoto wazuri wa Visitation na msala wa boksi la takataka kwenye Jenga YCS ile siku ya mwisho wa mkutano..
Old days are truly the Golden ones
 
Daaaah UKWATA walinitenga sana ikafika kipindi tunakaribia kupga pepa la six UKWATA ikabakiwa na viongozi tu km 6 ikabidi waanze kutuomba turudi kundini.
Ishu ilikuwa siku ya graduation full vituko yaani njemba zinabana pua kuimba kwaya na kata k kubwaaaah, daaah nikikumbuka those days raha saaana
 
Aisee mkubwa uzi wako umenikumbusha maisha ya Tanga Technical School aka Kiungani aka wazee wa Kwanjeka chini ya Disco la Mwl Kijazi,uzi umetulia sana aisee mkuu.....
 
Umenikumbusha mbali sana, wakati wa maulid ilikuwa kama fashion kuvaa khanga mbili, sasa wakati ule nilinunuliwa pair ya khanga mama alidhibiti ninapewa kipande kimoja kuendea shule mpaka term nyingine. Likizo hiyo niliweka ngumu kuwa lazima nipate pair ya khanga, niliulizwa unahitaji pair kwaajili gani? Nilijibu "baba wenzetu wakifa inabidi tuvae khanga kwenye msiba" mzee uso ulimbadilika lakini hakuhoji zaidi alininunulia tu pair ya khanga.
 
Nakumbuka enzi hizo nipo form six Iyunga tech siku ya mahafali yetu tuliwaalika madada zetu wa loleza girls bahati mbaya mnyamwezi sikuwa na pesa ya kuingilia disco basi nikaishia tu kuchungulia mlangoni kesho yake mshikaji wangu akaniambia kuna demu mmoja anakusalimia anaitwa fulani unamjua? nikamwambia ndio namjua tulisoma wote o level basi mshikaji akaniambia nimemtongoza na kakubali basi akaniuliza vp katulia?nikamjibu achana nae huyo demu ni kicheche.NISAMEHE DEVI KWA KUKULUSHIA NDEGE WAKO ZILIKUWA NI HASIRA TU ZA KUTOSWA NA HUYO DEMU O LEVER
 
Shikamoo barafu. Wewe Kama si class mate basi ni school mate. Pesa ilikuwa mwendo wa TMO , zikisomwa hadi karatasi ya mwisho bila jina lako unahsi kuzimia, simu ilikuwa mwendo wa riverse call ama radio kituo cha polisi, mzee umenichosha kwenye viwalo huku ukitishia mademu WA watu Kama una walk man Yuko na headphone basi huambiwi kitu - baadae ya jumamosi ya disco Ukwata mahubiri hutawaliwa na ama kondoo kuwa moto ama baridi Ili mradi wanoko wafikishe ujumbe. You made my day wallah
 
Nakumbuka enzi hizo nipo form six Iyunga tech siku ya mahafali yetu tuliwaalika madada zetu wa loleza girls bahati mbaya mnyamwezi sikuwa na pesa ya kuingilia disco basi nikaishia tu kuchungulia mlangoni kesho yake mshikaji wangu akaniambia kuna demu mmoja anakusalimia anaitwa fulani unamjua? nikamwambia ndio namjua tulisoma wote o level basi mshikaji akaniambia nimemtongoza na kakubali basi akaniuliza vp katulia?nikamjibu achana nae huyo demu ni kicheche.NISAMEHE DEVI KWA KUKULUSHIA NDEGE WAKO ZILIKUWA NI HASIRA TU ZA KUTOSWA NA HUYO DEMU O LEVER
Bhuahahahahaha we jamaa ulitisha asee
 
Ha ha ha nakumbuka kuna Dada nilimkamatia mpaka MGOMBEA AKASIMAMAA, sa kumbe yule kilaza ni mjanjaa akawa anapitisha kidole kiaina hivi ili kuthibitisha kwamba kweli kanidatisha au... Toka hapo nikawa nikiingia disko lazima nimbane yule jamaa kwenye mkanda ili asijezua balaa tena
 
Mkuu umesahau segments ya tv.. baada ya disco kwenye huko ni changanyikeni.. kuna watu walikuwa wakikesha kuangalia tv tangu ijmaa jioni mpaka jumatatu usiku
 
Umenikumbusha sie shuleni disco ilikuwa kila mwisho wa mwezi na kiingilio sh.500 na tulikuwa mchanganyiko yani siku hiyo ilikuwa inasubiriwa kama dhahabu.Nakumbuka tulikuwa tunaita "DEBE"
 
Aiseeee nouma sana, ukiona vyaelea jua vimeundwa............. afu siku hiyo hata menu ni tofauti na katikati ya week........old good days!!
Kulikuwa na UHIMA(CASFETA),UKWATA na TYCS wakati tukisoma.Sisi wengine tulio katikati,wakati mwingine tulienda UKWATA sbb ya kuimba Mapambio na nyimbo za kusifu.Kukesha ktk sala na usiku wa kuabudu.Kule TYCS tulisogea wakati wa mikusanyiko na ibada na kwaya ili kukaa kwa ukaribu na mabinti.Ambao tulikuwa tunawaona kwa msimu.

Hawa wazee wa "Maranatha" wa siku ya saba ya Juma nao walikuwa na Umoja wao.Baada ya machweo ya ijumaa huwezi kumuona na kitabu wala daftari la kukopi notisi.Hakika shule ni mahali sahihi kujifunza tamaduni na mila za jamii tofauti za dunia hii.

Huku UHIMA ilikuwa ni full sala na maombi ya kina na tafakuli za biblia.Wale jamaa wa TYCS walikuwa Liberal sana!Huku Disko unawakuta na kanisani wapo.Vurugu za kutoroka usiku kwenda mtaani wapo na kanisani wapo.Hawakujifunga sana kati ya dini na maisha ya ujana na uanafunzi.Kila jumamosi ya mwisho wa mwezi tuliletewa wasichana wa shule jirani kwa ajili ya disco.(Shule yetu ilikuwa boys tupu)

Wengi tulijichanganya kwa ajili ya "kureflesh mind".Kucheza disko mchana kutwa mpaka jioni ya machweo ilikuwa burudani sana.Ilikuwa siku njema ya kusubiliwa na wengi.Wengine hatukuwa wanafiki..Tulisema hadharani jinsi tunavyopenda disko na namna ilivyotupa burudiko la akili.Katika umri wa miaka 17 hadi 20,kukumbatiwa na mtoto wa kike mwenye konzi kifuani...Huku "West Life" wakitumbuiza na kibao chao cha "The Queen of My Heart".Loooh....ilikuwa barabara sana!Hakika nyakati hazirudi nyuma.

Tumesoma wakati huo usiokuwa na simu za mkononi.Haukuwa wakati wa M-Pesa,Tigo Pesa wala Airtel Money.Ni nyakati za EMS na Telegram,wakati wa barua na kadi za love na best wishes.Siku ya disko ndio ilikuwa makutano na yule umpendaye au wakati wa kutuma barua ya "proposal" kwa yule umtamaniye.

Barua yenye karatasi maalumu,zenye nakshi ya makopakopa na background ya maandishi ya kimapenzi.Ziliuzwa shilingi kumi hadi shilingi wakati wa uhitaji.Looh....We can not turn the days and live again in these memorable moments,but we can turn the memories and share the old good moments!

TAMSA ulikuwa ni Umoja wa Wanafunzi wa Kiislamu.Tuliwaita "Wazee wa Feedback",wengi baada ya disko ni kuja bwenini kusikiliza na kuulizia story za kwenye ukumbi wa disko,nini kilitokea na nani alifanya tukio gani.Wengi walipenda kuhudhuria lkn pindi wakionekana kwenye milango ya kumbi za disko walitengwa na jamii ya wenzao ktk umoja wao.

Wao wakabaki kuwa "Wazee wa Feedback" ya kilichotokea disko.Ukitoka tu disko utasikia "Hebu tupe feedback ya huko mtaalamu".Sehemu ya hekaheka za ujana na uanafunzi wao ni kama "ilidhurumiwa" na mifumo ya imani.Siri ya imani na mifumo yake anayo Mungu...

Hawa TYCS tuliwaita wazee wa "Kiasi".Wao kila kitu ni ruksa ili ufanye kwa "Kiasi".Kwamba kila kitu kina umuhimu wake ktk maisha lkn kifanyike kwa kiasi,kama ni disko nenda,ila cheza na kumbatia wakati wa blues kwa kiasi.Chochote kikizidi ni sumu.Hawa ukimkuta disko anaruka majoka kama Small Jobiso,na kwenye "Easter Conference" anahubiri kama kazaliwa ukoo wa masiah.Haya yote ni mafunzo.Mchangamano huu ukibahatika kuuona maishani,basi itakufanya uheshimu kila jambo ktk jamii.Fikra tofauti ndani ya jamii moja.

Siku ya disko kila mtu alichukua viwaro vyake vya nguvu.Kupulizia pafyumu popote unapoikuta inapuliziwa,kiasi unaweza kujikuta unanuka badala ya kunukia.Hii nayo ilikuwa "experience" nzuri ktk maisha.Mahali palipochezwa disko mchana ndipo usiku palipigwa sala za usiku kwa wanafunzi wa dini na umoja tofautitofauti.Mchana disko na usiku ni sala,na maisha yanaendelea.

Ujana maji ya moto.Habari moja ya kiongozi wa UKWATA kupenda disko mpaka kutengwa.Alikuwa kila disko lazima aingie,lkn hii ilikuwa kinyume na misimamo ya UKWATA.Walimpa machaguo...Kati ya disko na UKWATA...Jamaa hakujiuliza,alichagua raha za disko; na wakati wa mahafali hata cheti cha kutambuliwa kuwa member wa UKWATA hakupata.Sasa ni baba wa familia na watoto watatu,ndani ya ndoa takatifu.Kiongozi aliyemvua "uanachama" kwa kosa la kuingia disko ni baba wa watoto wanne ambao kila mmoja ana mama yake.Hakika mambo ya imani yana mafumbo yake.

Wakati mwingine imani na uchumi binafsi wa mtu vina uhusiano.Maana wale waliosema ni kukosoa uumbaji kusuka,kupaka wanja na hata kuweka lipshine,sasa ndio walimu wa kujiremba.Wakati ule hali "mbaya" ya uchumi wao binafsi waliificha ndani ya imani zao.Akiiulizwa kwanini hajirembi kama wenzake,atasema "Wapendwa ktk bwana huwa hatuhangaiki na urembo wa kidunia".Baada ya "boom" la pili mambo huwa tofauti.Hii inatoa funzo.

Mwingine alivaa "kobasi" na suruali za juu ya enka,kwa msimamo wa imani.Warembo wa Chuo wakamfanya aone ule si uvaaji wa kijana barobaro.Hakika nyakati zinabadirika na mengi tunajifunza kadiri ya tunavyokua.Miaka inaenda,umri unasonga,sasa tunakutana mitaani kama kina baba na kina mama wa familia.Wale wajuzi wa imani ndio sasa tunawashauri jinsi ya kupunguza mipango ya kando na kilaji(pombe) ili kuweka msisitizo wa kutunza familia.Hivi haya mambo ni kwanini?

Hivi kuna uhusiano wowote wa "kuyaonja" mambo fulani ya "utineja" na kuachana nayo na wengine "wasiyoyaonja" maisha hayo kukuta wakiyarudia ktk utu uzima?...

HeadMaster wetu(apumzike kwa amani) alisisitiza sana mahudhurio siku ya disko,akasisitiza kuwa tucheze sana mpaka tutoke jasho,na disko likiisha tuwahi bafuni kuoga kabla miili haijapoa,na tulale bila kugusa daftari mpaka kesho.Haikuwezekana kulala baada ya kuoga,muda huo ilikuwa ni wasaa wa kusimuliana yaliyojiri ukumbi wa disko.Wazee wa "Feedback" wakiongoza kwa maswali na udadisi.


Kuelekea mwishoni mwa disko,DJ machachari hufunga na nyimbo mfululizo za "blues".Hapo itapigwa ya kwanza na atatangaza "one more track"...ikisisika sauti hiyo watu huzidi kukumbatia ya mwisho mwisho.DJ mtukutu ataongeza nyingine moja akibandika juu ya pili,huku walimu wa malezi wakiwa tayari kuhakikisha kila mtu anarejea bwenini bila kuchepuka kizani.

Huu wakati hautarudi tena,sioni tena wakati huu ukirudi hata kwa vizazi vyetu.Ulikuwa ni wakati mtiifu na rafiki kwa utineja wetu.Mikono mifukoni mara baada ya disko na kurudi bwenini..Si kwasbb ya baridi watu wanaweka mikono hiyo mifukoni,bali wakati huo hali ya "maungo" inakuwa si hali tena.Sabuni hujuta kwanini ilitengenezwa kwa kuteleza...Looh!!Wakati huu upo wapi?
 
Back
Top Bottom