Vurugu zilianzia ktk kusengenyana maofisini, vijiweni, sokoni, majumbani
Zikahamia katika kupigana vijembe majukwaani na ktk vikao kwa mafumbo makubwa
Baadaye ktk kuchafuana ktk magazeti navyombo vingine vya habari kwa mafumbo mara chache sana kutaja jina la mtuhumiwa na fitina lukuki ktk vikao mbalimbali kichama na serkali na ktk mashirika mbalimbali ya umma.
Na sasa kukunjana mashati, ngumi njenje, kufukuzana ktk vyeo/uanachama ktk vyama, kuumbuana hadharani kwa kuwataja majina wahusika bila hofu yoyote hata kwa tuhuma za uuaji. Kuchafuana ktk vyombo vya habari waziwazi bila kuficha kitu (Kuanikana)
linalofata ni kuviziana usiku na kibastola, kukatana ulimi kwa nguvu, kutumia magenge ya watu waliochoka na maisha na wenye njaa lakini hawako ktk magazeti, redio, website nk, watu hawa wataunda vikundi vikiwa na silaha zote kama vyombo vya habari vilivyo na siraha zote kwa sasa(maana zinawatetezi mafisadi, sirikali, vyama vya siasa). Watu hawa watatumia nguvu na utetezi wa mafisadi walionao ukiwa nyuma yao kutekeleza amri waliyopewa na vigogo wao kuwamaliza wale wanaowanyima usingizi na ili nao wakizi njaa zao kwa kipato watachopata kama vyombo vya habari sasa. Waandishi ni waj=kati wao sasa kutoka kwa kuwaumiza wengine lakini baadaye hawatakuwa na nguvu tena bali hawa jamaa watashika nafasi yao na utakuwa na wakati wao kutoka kifedha.
Kitakachofata baadaye ni vikundi hivi kuwa sugu na kuongezeka kiidadi na kufanya kuwa vikundi vya kijeshi vyenye kulinda maslahi ya vigogo wao maana wataapa kwao ili wasizidiwe na kundi la wapinzani wao maana watakaposhinwa tu watafutiliwa mbali.
Ndipo patashika nguo kuchanika itakapokuwa kkt nchi yangu ya TZ niipendayo na ninaandika haya huku machozi yakinilengalenga lakini nifanyeje? ndiyo ufunuo huo! asiye na mwana na aeleke jiwe. Nimejaribu kuangalia miaka yangu pengine huo wakati hautanikuta lakini nimeona hata usiponikuta mimi mwanangu kipenzi atakuwepo
Watanzania pesa (Utajiri, Madaraka) tumeyapenda kupita kiasi chake sijui ndiyo ulimbukeni wa kutafuta! mimi sijui lakini hata wazungu walioendelea hawakutumia ujasiliamali tunaoutumia Tanazania na hata Africa yote ndiyo maana tunaishia ktk migogoro.
Kama Mkapa naye ni jasiliamali kweli ndiyo maana yake halisi? si kweli! leo hii mtu akiwa hana pesa anaaambiwa wewe si mjasiliamali aaahh kwa definition ipi ya ujasiliamali? Kama anayotumia Lowasa, Nchimbi, Mkapa, Karamagi? aaa acha waendelee kuniita si mjasiliamali ila hayo siyawezi waliyoyafanya wao.
Watanzania mali ni kitu kizuri sana lakini tusiitafute kwa njia zisizofaa itatufikisha pabaya
Asanteni WanaJF, ni Ufunuo tu