Raia Mwema: Mbowe na Lissu watofautiana kauli


Kwa hiyo kwa mawazo yako cdm iko hai!!!?
😛 😛 😛
 
Polepole na mikopo pia kuna kutofautiana sasa kipya ni kipi kati ya Lissu na Mboye. Timu kujaza sifa imekwisha.
 
Mbowe alisema amechanja Corona woote tukamtukana...ila lile dikteta la chattle likajiua kwa ujinga wake wa kutaka sifa na kupenda kuabudiwa....Samia kaingia kachanja Corona...
Unafuatilia mwenendo wa korona duniani wewe?
-Ni asilimia ngapi ya waliochanja(worldwide) !?
-Matumizi ya barakoa, kunawa mikono na kukaa mbalimbali kukoje??

Baada ya kupata majibu jiulize
Maambukizi yanapanda au yanapungua??

Majibu utakayopata yatakupa picha kamili ya hao pua ndefu unaowaabudu na waliokulisha kinyesi kwamba JPM alikufa kwa korona.
 
Dah!!

Kama hii ni kweli,
Basi Tanzania hakuna mwanasiasa wa kweli.

Wengi ni wababaishaji.
 
Hawawezi kuwa sawa.

Mbowe ameonja uchungu wa uongozi hadi kasota jela miezi nane.

Lissu anaongea akiwa nje ya nchi, hana uhalisia wa chama.

Hata huo uongozi wa chama Lissu aachane nao
Mtahangaika sana kuokoteza mpaka vya kuota.
 
Hata dikteta Mbowe na Lisu wanajitapa wako imara huku nyuma ya pazia wanaomba msamaha kwa kupiga magoti na kufuta dai la katiba mpya!!!
Katiba mpya yaja tafuta tu pa kukimbilia.
 
..wametofautiana wapi.

..Lissu kasema mwenyekiti hajakosea kwenda ikulu kumuona Raisi.

..pia amesema wanabadili mbinu kulingana na jinsi SSH anavyoendesha nchi.

..pia ktk kikao cha Bawacha ambacho Mbowe alihutubia kulifanyika zoezi la michango la join the chain.

..Sasa Mwenyekiti na Makamu wa chama wametofautiana ktk lipi?
 
Unajua huyo Wakudadavuwa kila jambo la Chadema huwa analichukulia negatively. Hivi kutofautiana mawazo ni jambo baya kwa chama chenye watu wanaotumia akili?
Chadema sio CCM ambako eti hata spika wa bunge anatoa mawazo yake kwa vile yako tofauti na mwenyekiti basi hata barua ya kujiuzulu wanamwandikia ili tuu afukuzwe hawamtaki.
Chadema iko imara sana kwa sasa kuliko wakati mwingine wowote
 
Mbowe hapo ataingia Cha kike Kama ndohivyo Lisu ajiendee ccm tu
 
Kuna maneno watu wanawawekea viongozi wa Chadema sijui wanayatoa wapi. Lissu huyu hapa.
 
Kule jela kawakuta na kuwaacha wangapi walikuwa na haki ya kutoka kama Mbowe ila hawajatoka?
Ayo ujibu mwenyewe ,jibu ni MOJA Mbowe hajatotoka KWa hisani ya mtu bali ulikua lazima kufanya hivyo binadam wote ni sawa ila sio sawasawa
 
Ayo ujibu mwenyewe ,jibu ni MOJA Mbowe hajatotoka KWa hisani ya mtu bali ulikua lazima kufanya hivyo binadam wote ni sawa ila sio sawasawa
Ndio ujue kwamba katoka kwa hisani kwa sababu kama sio hisani basi angendelea kusota kama wengine ambao hawajapata hisani.
 
debbug hiki ulichokiandika kilitakiwa kinapaswa kifunguliwe uzi wake umeongea point kubwa Sana Mwamba unatakiwa ujengewe sanamu pale Posta
 
Kamanda jikite kwenye hoja.
 
Ndio ujue kwamba katoka kwa hisani kwa sababu kama sio hisani basi angendelea kusota kama wengine ambao hawajapata hisani.
Nimekwambia mkuu binadam wote ni sawa ila sio sawa sawa ,tumeshudia misamaha mbali mbali ya wafungwa kupitia marais tz ,lin umewaona wanatoka na kwenda Ikulu, ukiachana na babu sea,jiongeze mkuu Kesi ya Mbowe lilisha kuwa zigo kwao , vinginevyo siku zote wasingekua wanaangaika Kama kuku atakae kutaga, Nguvu ya Dunia, nguvu ya umma,nguvu ya Mawakili upande wa utetezi, nguvu ya Mungu imewanyoosha, na wamekoma kweli kweli
 
Siwezi kukuzuia kuamini utakavyo mkuu, huo umma unaouzunguzia hatukuona nguvu yao yeyote wakati Lissu alipomiminiwa risasi mchana kweupe na hadi leo hakuna aliyekamatwa labda tuseme Lissu hakuwa mtu mzito wa kuamsha hiyo nguvu ya uuma.
 
Huu ni mkakati maalum wa kumuandama mbowe kwa lengo la kudhoofisha nguvu ya chadema. Baada ya ile tamthilia ya ugaidi kugonga mwamba sasa wamekuja na mkakati mwingine. Kama kweli Rais na mwenyekiti wa chama tawala ana nia nzuri yakushirikiana na vyama vingine kujenga nchi angeanzia kwa kukemea vyombo vya dola na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa. Baada ya hapo aitishe kikao cha maridhiano kwa kushirikisha vyama vyote na viongozi wao na yeye ashiriki kama mwenyekiti wa chama badala ya kushiriki kama Rais. Lakini kitendo cha kuzungumza kwa nyakati tofauti na viongozi mmoja mmoja kutoka chama kimoja kuna kila dalili ya hujuma dhidi ya chama husikka.
Lakini kwa ukubwa wa akili ya mbowe hili nalo atalitatua na nguvu ya chama chake itaendelea kuwanyima usingizi chama tawala.
Kuna mifano mingi tu yakumdhoofisha mbowe binafsi na kukidhoofisha chama anacho kiongoza, lakini ukiangalia kwa jicho ambalo si la ushabiki utaona mbowe bado adi sasa hivi ni mshindi wa mikakati yote yakumdhoofisha yeye na chama chake.
 
Nilifikiri kwa kukaa kwako bungeni kipindi cha kutosha basi ungeweza kuwa na ufahamu kuwa Rais hana mamlaka ya kumsamehe mtuhumiwa wa kesi yeyote bali anaweza kumsamehe mhalifu aliyehukumiwa tayari.
Kilichomtoa Mbowe ni DPP kuona hana misingi katika kesi yake hivyo kuiondoa mahakamani. Kaiondoa DPP au kaagizwa na Rais yote sawa maana sio msamaha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…