Raia Mwema: Umoja Party chahusishwa na Team Magufuli

Unakumbuka enzi za

CCJ : ilisemekana kiliundwa na baadhi ya vigogo wa Ccm enzi zile (awamu ya 4) akiwemo Marehemu Sitta na kina Mpendazoe ila baadae chaliiii..

ACT : hiki pia kilisemekana kina msukumo wa baadhi ya vigogo wa Ccm na wafuasi wa Zitto kutoka Cdm, japo bado kipo kwenye ulingo.

Japo vyama vingi ni takwa la demokrasia ila utitiri wa vyama hauna tija.
 
nitaona kweli chama cha wazalendo kama wale woote walioko bungeni na mawaziri watajiuzuru nyadhifa zao halafu ndio wawe busy kukipigania na kukijenga chama chao..

Lakini kama ni hii style ya kukatwa 2025 halafu ndio ujiunge umoja party itakuwa ni ugonjwa ule ule tu NJAA..
 
Tanzania inahitaki chama kipya makini kitachotoa toa challenge sera na serikali mbadala.

Chama cha kuwapigia wananchi na kutatua matatizo na changoto zao.

Chama kitachowaunganisha Watanzania wote, bila kujali kabila,dini,kanda, tabaka, chama, elimu, uwezo.

Wasio na vyama, waliotemwa na kutengwa na vyama, wanachama wa vyama vingine wazalendo wote inabidi waungane kuanzisha chama kipya kwa maslahi ya Taifa.
 
Kushangilia uwepo wa kuanzishwa chama kipya naona ni kuzidi kujichelewesha tu, hivyo ndivyo mwishowe hugeuzwa agents wa CCM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…