Raia wa Marekani Wanapenda kuvaa nguo Zinazofanana na Sare za Jeshi, Pia wanaweka Bendera ya Taifa Nyumbani

Jeshi letu ni la sita (6) duniani, naamini tuko vizuri katika nyanja karibia zote kuanzia teknolojia mpaka kufanya biashara.

Sasa kuna watu ni wabishi hawataki kuamini sijui mpaka walione jeshi lao mwezini na roketi?

We unaambiwa jeshi lako ni la sita duniani, huyo ghafla ushakimbilia google, acheni ujuani aise, hizo data hazijapikwa ni za kuaminika toka katika jeshi letu.
 
Serikali ijitahidi kuajiri (magenius) kila mahali mpaka idara ya maji mana si kwa aibu hizi tunazopata
Mara kuna uhaini mara tutapita mtaani kutafuta vijora vinavyo fanana na sare zetu

Wala hawana habari kwamba nyara za serikali zinipita kia na kwenda kushikiwa austiralia.
 
Basi watakuwa si wazalendo kama sisi.
 
Naamini kati ya majeshi 6 bora duniani ambapo jeshi letu (JWTZ) ni la 6, naamini kwenye ma 5 yajuu jeshi la Marekani litakuwepo. Sasa kwanini raia wa Marekani wanavaa nguo zinazofanana na jeshi na hawachukuliwi hatua?
La sita Kwa ubovu ila Kwa ubora ni la 106
 
umesahau kuhusu ushoga pia
Ushoga hata Tanzania unaruhusiwa ndiyomaana serikali imeruhusu NGO za mashoga kama vile LGBT Voice kufanya kazi na viongozi wake wanafahamika ila hawaguswi.
 
Achaneni nao! Uwezo wao wa kufikiria umeishia hapo!

Kuna watu bado wanaishi kijima zama za giza.
Eti hayo majezi nayo uwazuie watu kuvaa
 
Kwa hiyo kila lifanywalo ni USA ni jambo jema!!

Umewahi kusoma sheria za nchi ya marekani ukaona zinakataza kuvaa sare mavazi yanayofanana na sare za jeshi? Au hujui kwamba kila nchi ina sheria zake. Au kwa sababu unaamini kwamba marekani ndiyo kila kitu hivyo hata katiba na sheria zetu mbalimbali tumezikopi toka marekani!!
 
Binafsi sioni mantiki ya kuwaiga marekani, wana mifumo yao na sisi tuna ya kwetu. Ninachopinga ni adhabu zisizofata sheria pale unapokamatwa na kosa la kuvaa nguo ya jeshi.
 
Ila hili lakuweka bendera Nyumbani wangeturhusu aisee tujivunie utaifa wetu.
 
jeshi letu duniani ni la 6 embu fafanua ndugu…
Afafanue nini wakati aliesema mpaka sasa hajakanusha wala kusema kakosea bali jeshi Zima limekaa kimya maana yake ni la Sita na hao watano hatusemi

Ngoja niweke wababe kumi hapa China, 🇺🇸, Russia, 🇬🇧 India, South Korea, france aah sasa South kaingiaje hapa tena haya tuendelee kuna makosa kidogo hapo halafu japan mmh yaani Israel anachukua mafunzo kwetu
 
Jeshi lenye ndege vita za Kirusi za miaka ya 70 eti ni jeshi la 6 kwa ubora,haya maajabu
Unajua nchi hii ya ajabu sana! Ya sita kwa lipi? Wanatechnoloja gani wanayodevelop jeshini?
Kule kuna vilaza kazi yao kutumia nguvu!
Kwanza jeshini wengi shule ndogo labda juzi hapa ndo wanachukua waliomaliza six na degree!
Ya sita kwa kutumia nuvvu sio akili!
 
Biashara ya kutengeneza na kuuza bendera itakuwa kubwa sana.
 
Sisi Bendera zetu za taifa zinapeperuka kwenye Mioyo yetu

Tunaipenda sana Nchi yetu tena sana ila usiwe mtu wa kukariri kuwa kuonesha upendo lazima tuoneshe kwa njia ya wanaonesha wengine

mbona mie nawapenda sana wake zangu lakini siwalishi Keki hadharan kwa mdomo wala siwaposti kwny mitandao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…