Raia wa Marekani Wanapenda kuvaa nguo Zinazofanana na Sare za Jeshi, Pia wanaweka Bendera ya Taifa Nyumbani

Jeshi letu limejipotezea heshima lenyewe
 
HABARI ZA LEO WAKUU.....!

Naomba nitoe yangu, ambayo yanaweza kupishana kimtazamo na wengi.

KUHUSU KATAZO LA MAVAZI
Nia ya JESHI kukataza mavazi ni NJEMA TENA NJEMA SANA, NI katika ule msemo maarufu wa TAHADHARI KABLA YA HATARI....
Kwanini tahadhari kabla ya hatari, ama MCHELEA MWANA KULIA HULIA YEYE.....! Kumejitokeza tabia ya UJAMBAZI WA KUTUMIA SILAHA.......!
Na hivyo majambazi hayo kuvaa sare za jeshi na kufanya uhalifu....... kwa watu kuona wanajeshi na bunduki ni kawaida....... hivyo ktk hali ya kupunguza WAHALIFU HAWA WANAOJIFICHA KTK SARE ZA JESHI jeshi limeona lichukue hatua ya kutoa katazo lenye nia njema.....!

KATAZO HILI NI KWA USALAMA WETU NA SI USHAMBA kama ambavyo wengine wanadiriki kusema
 
Kiufupi nguvu ya jeshi na uchumi wa nchi ni simultaneously, yaani ukiona nchi imezidi uchumi basi jua hata nguvu za jeshi imekuzidi, very rare kukuta nchi ina uchumi mdogo ila ikawa na nguvu za kijeshi kubwa kuliko yenye uchumi mkubwa vinginevyo imejiwekeza sana katika sayansi, research na innovations za kijeshi kila Leo kama north Korea, Iran na zingenezo


Yaani haiwezekani eti sisi jeshi letu likawa bora kuliko la saudia, Qatar, UAE, Singapore, India, China, Korea, USA, south Africa, Morocco, misiri, Japan, Iran, Israel sijui namba 6 mmeitoa wapi maana hayo mataifa machache tu niliyoyataja baadhi yao yana financial muscles kubwa zaidi yetu mpaka Mara 20 huko sasa utaweza pigana nao sangapi?
 
Binafsi sioni mantiki ya kuwaiga marekani, wana mifumo yao na sisi tuna ya kwetu. Ninachopinga ni adhabu zisizofata sheria pale unapokamatwa na kosa la kuvaa nguo ya jeshi.
Tuanzie hapa,
Nguo ya jeshi inafikaje kwa raia mtaani?
 
Raia ukivaa nguo za jeshi la Marekani nchini ni kosa kisheria??
 
Kwenye bendera kuna matumizi gani mabaya ikiwa sehemu inayoonekana? Au kwanini wanakatasa kuweka nyumbani
 
Mioyo kazi yake ni kusukuma damu mazee.
 
Marekani ni akili kubwa, hawa wa kwetu, ni akili ndogo Sana, ni watu wasiojielewa
 
Ma swali mazuri sana kiongozi! Lkn hapa tupo Tanzania mkuu Kila nchi Ina Mila destuli,Sheria na taratibu zao, ndiomana hata hao wamarekani wanasumbuliwa na watu wanaomiliki siraha kihorela kwakuwa hata wao Wana madhaifu Yao! Sijapinga hoja yako
 
Kila taifa na utaratibu wao
 
Tuanzie hapa,
Nguo ya jeshi inafikaje kwa raia mtaani?
Mkuu Yoda mm sitaki wala kufanya mambo yawe magumu, jeshi halitaki tuvae sare basi tuvae nguo nyingine ishu hapa ni ukivunja hiyo sheria usiadhibiwe bila kufata sheria.
 
Hivi kila kifanyikacho marekani lazima tu copy?
 
UMESHASEMA MAREKANI BROO,
HUWEZI KUIFANANISHA MAREKANI NA TANZANIA KWA CHOCHOTE, WALE WAMAREKANI WANAJIAMINI NA JESHI LAO WANAJUA LIPO MAKINI NDIO MAANA HAWAHOFII MTU KUVAA NGUO ZAO MAANA KAMA SIO MWANAJESHI UKIZIVAA WATAKUTAMBUA TUU.
NA SIO NGUO TU MAREKANI HATA UKIIGIZA MOVIE YAKO UKIHITAJI KUTUMIA NDEGE, AU MAGARI YAO YA KIJESHI KWENYE MOVIE WANAKURUHUSU TU, ILA SASA JARIBU KWENYE NCHI KAMA ZETU UONE.
 
Jeshi kwao ni jambo la kawaida sana...
 

Raia wa Marekani Wanapenda kuvaa nguo Zinazofanana na Sare za Jeshi,

Kupenda kuvaa nguo zinazofanana na sare za Kijeshi, Ndio hivyo tu, kwamba wanapenda kuvaa nguo hizo sawa na Watanzania wengi wanaopenda kufanya hivyo, haina maana kuwa wanayo ruhusa kikatiba au kwa sheria yeyote ile kufanya hivyo, isipokuwa, kuwa wewe ni Mwanajeshi au una ruhusa ya kuvaa sare hiyo, kama vile ukiwa wewe ni msanii na unayo ruhusa kutoka jeshini.






Itoshe kusema, ni Marufuku nchini Marekani kuvaa sare za Kijeshi au nguo zinazofanana na sare hizo kama wewe sio mwanajeshi.

Tusidanganyane hapa.

Pia wanaweka Bendera ya Taifa Nyumbani​


Bendera katika Nchi yeyote ile ni lazima iheshimiwe, pia, kuna kanuni zinazowezesha raia yeyote yule kuwa na Bendera hiyo, hatahivyo haina maana kuwa unaweza kuzazagaa mjini alimradi tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…