Raila odinga ashambuliwa kwa bakora mkutanoni kwale

Raila odinga ashambuliwa kwa bakora mkutanoni kwale

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Bakora.jpg

Mzee aliyewashambulia kiongozi wa Cord Raila Odinga na gavana wa Kwale Salim Mvurya kwa bakora wakati wa mkutano Kinango, Kwale Septemba 29, 2014. Picha/FAROUK MWABEGE Na FAROUK MWABEGE
Imepakiwa - Monday, September 29 2014 at 16:54Kwa Mukhtasari
Kizaazaa kilizuka leo katika mkutano wa Cord eneo la Kinango kaunti ya Kwale baada ya mwanamume mmoja kumshambulia Raila Odinga na gavana Salim Mvurya kwa bakora.

KIZAAZAA kilizuka katika mkutano wa CORD eneo la Kinango kaunti ya Kwale baada ya mwanamume mmoja kumshambulia Raila Odinga na gavana Salim Mvurya kwa bakora.

Mwanamume huyo alijitosa uwanjani wakati wawili hao walipokuwa wakijiburudisha na ngoma ya kitamaduni ya Sengenya na kuwacharaza kwa bakora migongoni.

Tukio hilo lilitokea kwa kasi mno kiasi cha kuwapata walinzi wa viongozi hao katika hali ya mshangao kwa sababu hawakulitarajia.

Kitendo hicho kilizua patashika ambayo iliwalazimu walinzi kumbeba mwanamume huyo hobela hobela huku wakiwa na nia ya kumuadhibu.

Hata hivyo Bw Mvurya aliingilia kati na kuwarai walinzi hao wasimpige jamaa huyo aliyekuwa ametaharuki si haba.

Baada ya kuponea chupu chupu mwanamume huyo alitimua mbio na kabla ya wanahabari kumfikia na kumdadisi.

Punde waliporudi jukwaani Bw Odinga na Bw Mvurya walionekana kuwa wenye maumivu makali ila walijikaza kisabuni na kuendelea na mkutano huo.

Mbali na jamaa huyo kutoweka duru za kuaminika ziliarifu Taifa Leo kuwa alitenda kitendo hicho kutokana na kughadhabishwa kwake na hatua ya wawili hao kusakata ngoma na mkewe.

Wakazi hao ambao hawakutaka kutajwa walisema kuwa mkewe jamaa huyo alikuwa miongoni mwa wanamitindo waliokuwa wakisaka ngoma katika mkutano huo.

Hata hivyo ilikuwa vigumu kuthibitisha taarifa hizo kwani wengine wao walisikika wakisema kuwa jamaa huyo alikuwa amepagawishwa na ngoma hiyo ya kienyeji iliyokuwa imetia fora.

Baraka

Mkutano huo uliendelea kama kawaida ila baadaye kisa kisichokuwa cha kawaida kilitokea tena pale ajuza mmoja alipomjongelea Bw Raila na kumbusu mkono.

Walinzi waliokuwa macho walitaka kumkamata mwanamke huyo mkongwe ila Bw Odinga alitaka wamuachilie.

"Mwacheni mama aje kwangu hizi ni baraka kutoka kwa mungu na ishara tosha kuwa mola yuko pamoja nasi," Bw Odinga alisikika akisema.


Mwanamke huyo aliyembusu zaidi ya mara tatu alisikika akimwambia Bw Odinga "Tuokoe baba! Tuokoe mwanangu! Taifa hili linakuhitaji!"


 
Last edited by a moderator:
Kama yuko na akili timamu na aadhibiwe hatutaki siasa za kukoseana heshima.
 
Raila Odinga attacked by elderly man at Okoa Kenya rally

PIX1.jpg


Security aides subdue an elderly man at an Okoa Kenya rally in Kinango market in Kwale County on September 29, 2014 after he attacked Raila Odinga and Governor Salim Mvurya. PHOTO | FAROUK MWABEGE | NATION MEDIA GROUP

PIX.jpg


By FAROUK MWABEGE


Cord's Okoa Kenya rally in Kinango market in Kwale County was on Monday briefly interrupted after an elderly man emerged from the crowd and attacked Raila Odinga and Kwale Governor Salim Mvurya using a walking stick.


The man hit Mr Odinga and Governor Mvurya twice on the back each moments after they had joined a dancing troupe for the traditional sengenya dance.

Mr Odinga's aides immediately seized the man, but were prevailed upon to release him.

The rally proceeded after calm had been restored.

At the rally, Mr Odinga said he was ready to appear before a parliamentary committee to back his claims that Sh15 billion were lost during the transition period.



He questioned why governors had not been arrested and taken to court if indeed they had embezzled funds.

"They are claiming that governors are stealing money but unfortunately none of them has been arrested and this is a clear indication that their allegations are baseless," he said.



http://www.nation.co.ke/news/politics/-/1064/2468976/-/ynx0id/-/index.html
 
Railaman30092014.jpg

CORD leader about to be whipped by a man in Kwale

Kwale residents were treated to a rare spectacle on Monday when an elderly man whipped Opposition Leader Raila Odinga during an Okoa Kenya rally at Kinango grounds. The incident which is now trending online has sparked response from users who have posted various reactions to that effect. Many hilarious photos depicting the former Prime Minister with a swollen eye are doing rounds on the various social media platforms.

Railaswolleneye30092014.jpg



The man, who police later released after establishing he was mentally unstable, also turned his cane on Kwale Governor Salim Mvurya as the leaders were enjoying the coastal sengenya dance with traditional dancers. The CORD leader and Kwale Governor both received a stroke each on their back which some online users now refer to as ‘Kiboko Haram’. With some online users claimimng that the old man is a member of the terror group 'KIBOKO HARAM' Security officers were able to restrain the angry man as the leaders stood in bewilderment.


RailaObama30092014.jpg

The leaders, who received a stroke each on their backs, stood in bewiderment as security officers restrained the angry man and whisked him away. The event was part of the Coalition for reforms and Democracy's push for a referendum through which it hopes to open up the Constitution to amendments, in Kinango, Kwale County. Yesterday evening, police confirmed they had released the man but failed to state why police were not at the function. The attacker, who was dressed in grey shorts, a white T-shirt and slippers, was restrained by private security personnel who handed him over to the police. Eyewitnesses said the man was unhappy because his wife was dancing 'suggestively'.
Read more at: Standard Digital News : : Lifestyle - Online users make fun of Raila?s public whipping in pictures
 

Attachments

  • Railaswolleneye30092014.jpg
    Railaswolleneye30092014.jpg
    10.3 KB · Views: 170
Bwahaha, LMAO...video f the year. He should have left the governor though and concentrated on Ogwambo.
 
Saw a lot of memes and such jokes about the former PM on twitter, most of them were humorous but in bad taste. we must learn to respect leaders like Raila, they risked their lives to fight for the 'freedom' that Kenyans are enjoying today.
 
Lakini walinzi wa Raila walikuwa wapi?

Mbona ni kama vile hakuwa na walinzi....

Ila huyo babu kanichekesha kweli.

Nimeona Raila anajishika bega (kama anajikuna hivi)....hiyo ni dalili bakora kumwingia!

Hahahaaaa Kenya kuna vituko sana.
 



Hali ya taharuki iliibuka katika mkutano wa hadhara katika jimbo la Kwale nchini Kenya, baada ya mwanamume mmoja kwenda ukumbini na kuanza kutandika bakora kiongozi wa upinzani Raila Odinga pamoja na wanasiasa wengine.

Raila alikuwa amejiunga na kikundi cha wanawake waliokuwa wanacheza densi ya kitamaduni kuwatumbuiza wageni, pamoja na gavana wa jimbo la Kwale Pwani ya Kenya Salim Mvuruya katika mkutanmo wa kisiasa.

Walikuwa wameambatana na viongozi wengine, wakiwemo, Seneta Juma Boy, Hassan Omar, Agnes Zani, James Orengo, Johnstone Muthama na wengineo.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga

Mwanamume huyo alimshambulia Odinga ambaye ni waziri mkuu wa zamani na kumchapa mara mbili kabla ya kumgeukia gavana wa jimbo hilo na pia kumchapa mara mbili. Hata hivyo mwanamume huyo alishindwa nguvu na walinzi wa Raila Odinga.

Polisi walithibitisha kuwa walimkamata mwanamume huyo na kumwachilia baada ya kugundua kuwa alikuwa na matatizo ya kiakili.

Haijulikani kwa nini mwanammume huyo alimshambulia Raila ila baadhi wabnasema ni kwa sababu alighadhabishwa pale waziri mkuu alipocheza densi na mwanamke aliyesemekana kuwa mke wake ambaye alikuwa katika kikundi cha wanawake waliokuwa wanawatumbuiza wageni waheshimiwa.

Viongozi waliofika walilazimika kusitisha densi hiyo kabla ya mwanamume huyo kushindwa nguvu.


Source:
BBC Swahili

http://www.bbc.co.uk/swahili/habari/2014/09/140930_raila_ashambuliwa
 
Last edited by a moderator:
Raila Odinga yule aliyeshindwa uchaguzi wa uraisi nchini Kenya, amemsamehe Mzee mmoja aliyemtandika bakora katika mkutano wa hadhara.

Source habari magazetini
 
Inawezekana kafanya kama mgombea mmoja alivyovamiwa jukwaani wakati wa kampeni au kuanguka anguka jukwaani.Yote yawezekana.
 
Raila Odinga yule aliyeshindwa uchaguzi wa uraisi nchini Kenya, amemsamehe Mzee mmoja aliyemtandika bakora katika mkutano wa hadhara.

Source habari magazetini

Unajuwa hii ni habari ya lini? Kumbe member wengine hapa JF ni useless kabisa hapa tunahitaji habari mpya na siyo historia.
 
Back
Top Bottom