Raila Odinga: Nilikwenda Zanzibar kuondoa mshtuko wa kupoteza Uchaguzi

Raila Odinga: Nilikwenda Zanzibar kuondoa mshtuko wa kupoteza Uchaguzi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1663247459412.png


Aliyekuwa Mgombea Urais wa Azimio la Umoja Raila Odinga alieleza kwamba alisafiri kwenda Zanzibar pamoja na familia yake yote ili kupata nafuu baada ya kushindwa Uchaguzi wa Agosti 9, 2022.

Waziri Mkuu huyo wa zamani alibainisha kuwa safari ya nje ya nchi ilikuwa muhimu kuwezesha familia yake kupata nafuu kutokana na mshtuko wa kupoteza uchaguzi.

Raila amezungumza wakati wa hafla ya kuapishwa kwa Gavana wa Mombasa Abdulswamad Nassir mnamo Alhamisi, Septemba 15.

"Nilienda kufanya mazoezi Zanzibar. Nilimtoa mke wangu, watoto na wajukuu wangu kutokana na mshtuko walioupata. Nimerudi asubuhi ya leo kutoka Zanzibar, sikuweza kuwa nanyi wakati wa kuapishwa (kwa Abdulswamad), lakini niko hapa," Raila alisema.

Kabla ya kuapishwa kwa William Ruto kuwa Rais, Raila alitoa taarifa iliyoashiria kuwa atakosa hafla hiyo kwa vile alikuwa amesafiri nje ya nchi.
 
Alidanganywa na Uhuru mtoto wa mjini kumbe wamemwingiza choo cha akina mama.
Usinikumbushe jishi nilivyonusurika kipigo Nairobi kwa kuvuta mlango wa choo cha Barclays bank..kwa nguvu nikalivuta limama nene chooni na likapiga ukunga au wanaita nduru🤣🤣🤣🤣🤣
 
😂😂😂😂 mshtuko wa kukosa uchaguzi, familia ilikua ishajiandaa kisaikolojia
 
Wakenya ni ndugu zetu..na mzee anakupenda sana zanzibar hata mara ya mwisho alivyokosa uraisi alienda chill zenji
 
Back
Top Bottom