Bepari2020
JF-Expert Member
- Nov 7, 2020
- 2,072
- 2,453
T̶a̶n̶z̶a̶n̶i̶a̶ Ni mahali salama na kimbilio la kila mtu
Zanzibar
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
T̶a̶n̶z̶a̶n̶i̶a̶ Ni mahali salama na kimbilio la kila mtu
Kuunga mkono udikteta wa jiwe kumekuponza , Mungu hataniwiView attachment 2357892
Aliyekuwa Mgombea Urais wa Azimio la Umoja Raila Odinga alieleza kwamba alisafiri kwenda Zanzibar pamoja na familia yake yote ili kupata nafuu baada ya kushindwa Uchaguzi wa Agosti 9, 2022.
Waziri Mkuu huyo wa zamani alibainisha kuwa safari ya nje ya nchi ilikuwa muhimu kuwezesha familia yake kupata nafuu kutokana na mshtuko wa kupoteza uchaguzi.
Raila amezungumza wakati wa hafla ya kuapishwa kwa Gavana wa Mombasa Abdulswamad Nassir mnamo Alhamisi, Septemba 15.
"Nilienda kufanya mazoezi Zanzibar. Nilimtoa mke wangu, watoto na wajukuu wangu kutokana na mshtuko walioupata. Nimerudi asubuhi ya leo kutoka Zanzibar, sikuweza kuwa nanyi wakati wa kuapishwa (kwa Abdulswamad), lakini niko hapa," Raila alisema.
Kabla ya kuapishwa kwa William Ruto kuwa Rais, Raila alitoa taarifa iliyoashiria kuwa atakosa hafla hiyo kwa vile alikuwa amesafiri nje ya nchi.