Raila Odinga: Polisi wa Tanzania kama Ulaya. Adai wanaweza kusubiri umalize kazi zako ndio wakukamate

Raila Odinga: Polisi wa Tanzania kama Ulaya. Adai wanaweza kusubiri umalize kazi zako ndio wakukamate

Mohammed wa 5

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2022
Posts
1,215
Reaction score
3,035
Mwanasiasa mkongwe wa Kenya, Raila Odinga anasema kuwa polisi wa Tanzania wanapitia kwenye mafunzo ya kufundishwa utu kwa wananchi hata wakitaka kuja kukukamata lazima waombe Kwanza na wakikuta upo na kazi watakusubiri mpaka umalize ndipo wakuchukue.

Polisi wa Tanzania ni Kama wa ya Ulaya.

Naomba kuwasilisha.

 
Wako peace sana ase, ilishawahi kunitokea ishu moja tumegombana na mtu ghafla kama nusu saa hivi naona bajaji ipo nje kwangu wakashuka na walijitambulisha vizuri kwa kuonesha ID zao kila mmoja.

Next wakanambia tunakuhitaji kituo cha polisi kwaajili ya kutoa msaada wa maelezo, nilipochungulia ndani ya bajaji nikamuona mke wangu. Nikamuuliza mke wangu "umeumia sana kiasi utahitaji uchunguzi wa kitabibu?" akanijibu "hapana naweza kwenda hata asubuhi".

Basi bwana nikawaambia wale jamaa naomba nilipe tu nauli ya bajaji ila nitakuja nikishampeleka mke wangu hosptali, wakaniambia nilipe nauli elfu tano wakarudi zao na kesho yake saa nane mchana nikaenda tukayamaliza.
 
Mwanasiasa mkongwe wa Kenya Raila odinga anasema kuwa polisi wa Tanzania wanapitia kwenye mafunzo ya kufundishwa utu kwa wananchi...

Hawa waliotokomea na Mosses Lijenje?

Fr-BSZqWwAE0aWb.jpeg


Kitanda asichokilalia hawezi kuujua ukali wa kunguni wake.
 
Mwanasiasa mkongwe wa Kenya Raila odinga anasema kuwa polisi wa Tanzania wanapitia kwenye mafunzo ya kufundishwa utu kwa wananchi
Kenya Wanajeshi wale siyo Polisi yaani hakuna customer care Hata kidogo yaani hata akiwa bar kumwagilia Moyo utajua Polisi kaingia bar full Ubabe.

Mbaya zaidi Fika kwa Polisi station kueleza shida yaani hayo Mahojiano tu utafikiri wewe ndiyo mhalifu. Kwa ufupi wao ni Police force Tanzania ni Police service.
 
Hawajui vizuri

Afu ifike mahali tuache kujilanganisha na nchi za wazungu, ni mbingu na ardhi, juzi Kuna mtu nilikua naongea nae yaani police service ya kwetu kuja kufanana na nchi kama USA itachukua miaka 200 Mungu akitusaidia aisee

Kule police wote wana body cameras Kila uwapo kazini unachofanya kinaenda kwenye server! Ole wako uzingue sasa, Kila kitu kinarekodiwa, hii inasababisha wawe waadilifu, ishu ya kumpiga mtu bila sababu za lazima usijaribu utanyea ndoo

Kama haupo kazini huruhusiwi kufanya arrest na shughuli zingine za kiofisi(labda iwe emergency) kiufupi policy Yao inataka ufanye kazi ukiwa na body camera inayorekodi matukio yote

Kuna polisi walienda kufanya eviction mahali walivyo wajinga wakawa wanaiba sijui saa,sijui Nini aisee washafukuzwa kazi na sa ivi kesi ipo mahakamani ni mwendo wa kula mvua tu, huku bongo polisi wakikupiga ambush wakikusachi kama una Mali ni halali Yao, watu wanapekuliwa bila search warrant huku, wenzetu ukimpekua mtu bila warrant hata ukimkuta na Nini ushajichanganya huwezi kumshinda

Niliona clip Moja jamaa kamsimamisha mtu anahisi anaendesha huku kalewa, kufungua mlango anakuta ni bosi wake, jamaa akamkomalia kibishi bosi akawa anamuomba let it go am your captain jamaa akakomaa nafanya kazi yangu, mwisho wa siku yule captain alifukuzwa kwa madai alitaka kutumia madaraka yake vibaya

Sasa huku kwetu unaweza mkomalia mkubwa wako, never!! Bado tuna safari ndefu kwenye kupata haki, bongo ukiingia polisi hata kama Huna kosa huwezi kutoka mikono mitupu
 
Back
Top Bottom