== Ulandanifu wa Mambo : Funguo za Hekima ==
Kiuno na ufikirifu mifumo, miundo yote ina asili mbili kwa wakati mmoja na pahala hapo hapo; asili/ontolojia ilivyo ni (1) Mraba wa kwa mfano 'Wakati-Jamii-Machaguo ya Kitaasisi-Matukio', na (2) Konstrakti za Miundo ilivyo ni 'Miongozo' ya ulandanifu wa sura na hadhi za mambo.
Kwa mintarafu ya hivi, Udhahiri wa vitu vyote vyenye kuonekana na visivyoonekana kwa wakati ni ulandanifu wa 'Pumzi za Miraba ya Miundo' na 'Mbegu za U-JUA-ji' kwa namna inayoweza kukadirishwa kana 'Msokotano wa Mawimbi ya Uzima'. Basi ndiyo yawa, msokotano wa pumzi za mawimbi ya uzima ndiyo kile, kwa kiasi fulani katika ulimwengu wa sayansi 1.0, hujitokeza kwa sehemu kama udhanifu wa 'Mawimbi Tashoni'... Tena ndiyo basi, mawimbi tashoni ni jambo lenye kufanania na dhana ya 'Prana/Ki/Chi/Mtetemo wa Eitha'--asili ya elementi ya tano(5) ya 'Ukuwa ama/na Ukuja-kuwa' kitungamo na uzito; yenye uhusiano wa moja kwa moja na Usentienti, Konsanyansi na Nuru ya Ufahamu kwa kiumbe chochote--chenye kuonekana/kutoonekana kwa wakati.
Kiufundi, 'Prana/Ki/Chi/Mtetemo wa Eitha' ni jambo lile lile ambalo kwenye mapokeo ya Ukristo hutajwa ni 'Roho Mtakatifu' kwa kuwa daraja la Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu ni 'Pumzi yenye Uhai na Uzima'; Nuru iliyo ni '
Nishati Nukta Sifuri' kwa yote na vyote na tena asili ya 'Swastika'.
Kwa mintarafu ya hivi, metafizikia ya Elimu ya Yote na Vyote ni Ilimu--Ilimu ilivyo ni muktadha akilifu wa 'Maarifa na Maarifu' ya 'Pumzi Takatifu': 'Roho Mtakatifu'. Basi ndiyo yawa, Rizayati ya Elimu 3.0 ni Sayansi 3.0 ya Intelijensia ya Nafsi-Roho/Sonafi katika sifa, hadhi na madaraja ya kujua na ku-JUA ilivyo ni '
Nia ya Kristu'.
Tena basi, muktadha akilifu wa Uweza, Nguvu na Utukufu ni mambo ya kukadirisha mambo ya mbingu na nchi kwa dhamira ya kudhihiri hata yale yanayoweza kuwa ni 'makuu zaidi' kuliko ujuaji wa kawaida wa 'utofahamu kumbaizi wa jamii'; kwa kuwa
ku-JUA ni mambo ya kuwa 'Nuru na Kweli'; ambavyo mwenye kuwa na mwangaza katika KWELI, awa ni Mtu wa Mwangaza/Iluminata kwa sifa, hadhi na utukufu wa sura na matendo yake na tena kadiri ya
dhamiri sahihi ya kuathiri 'Prana/Ki/Chi/Mtetemo wa Eitha...
Kiufundi, sifa na hadhi ya mtenda-kitendo-tokeo ni jambo pacha na nasibu ya dhahiri mahsusi kwa dhamira na nia jambo lenyewe tarajiwa kiwakati. Kwa mintarafu ya hivi, dhahiri yote ni matokeo ya 'mbegu ya u-JUA-ji' na 'Kujichagulia' kupitia 'Dhamira na Nia' -- dhamira na nia ikuwako katika kiumbe chenye Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu; ambavyo kiumbe huona na kutambua (ma)fahamuni yale tu aonayo kimfumo wa (1) Kujongea ama kubakia pahala, kisupasha, kulingana na msukumo wa kinguvu: Inesha, na (2) Pumzi ya Msukumo wa kinguvu, Mzuto/Momentamu , kuwa sawia kwa nguvu yenyewe na uelekeo/mielekeo yake na basi kuathiri usupasha wa kinachojongea: Uzuto, na (3) Kila kitendo chenye pumzi ya nguvu huakisi kiasi kile kile cha nguvu ya pumzi kukamilishana usimetria wa nguvu na uelekeo wa uweza wa pumzi.
Basi ndiyo yawa, ushuhudiaji wa chochote kwenye ulimwengu fizikali hutawaliwa na
mwingiliano wa trizaniamu ya uono na metafizikia yake ilivyo ni 'Mboni AJNA'; ambavyo metafanusi ya udhahiri na kisichodhahiri ni mbegu ya u-JUA-ji kwa yote yenye nasibu 'Kutokea': AKASHA.
Kiufundi, sifa na hadhi ya mtenda-kitendo-tokea ni fanusi ya 'mambo ya nyakati'; ambavyo wakati unatambulika kwa nasibu ya mawili: (1) Kumbukumbu, na (2) Mabadiliko ya Kikumbukumbu. Kwa mintarafu ya hivi, mabadiliko yoyote ya jambo, kisifa ya muundo na uwepo, ni mwanzo wa 'rajisi ya wakati'--wakati wa hili na wakati wa lile, ambavyo akili na utambuzi hujenga mashauri na mafikara kuhusiana na wakati na mabadiliko.
Basi ndiyo yawa, asili khasa ya wakati ni
infaransi ya 'mabadiliko ya Kikumbukumbu' ambavyo: kama hakuna kumbukumbu ya moja kwa moja ama hakuna hisia/kuyabaini mabadiliko basi 'Hakuna Shauri la Wakati'. Tena basi, inaweza kushangaza: kumbukumbu zote ni infaransi ya vile vinavyoweza kukadirishwa kama zao la
'vituo vya kiwakati' na 'vizio vya khabari'…
== Mafikara na Ufikirifu : Vimvuli vya Uakilifu ==
Kiuono na Ufikirifu Mifumo, infaransi ni mambo ya 'vina vya tafsiri' kiurazini wa mambo ambavyo usentienti, konsayansi na nuru ya ufahamu huchakata 'Khahari' kwa nguvu za kiakili – kwa ajili ya khabari za kimafahamu.
Kwa mintarafu ya hivi, si kila kile ambacho mtu/kiumbe mwanajamii anakishuhudia kwa maneno, fikara ama/na shauri ni 'Ukweli Khasa wa Mambo' bali matokeo ya upeo na vina vya tafsiri katika kuyabanisha yale yote ya mpangilio wa dhana na mawazo/mafikara--dhana na mawazo ilivyo ni pamoja na mahusiano yake kimafikara/ufikirifu.
Basi ndiyo yawa, usentienti-konsayansi-nuru ya ufahamu ni kitovu cha 'uchakataji wa mafahamu kikhabari' kwa misingi ya 'Maarifa na Maarifu'; ambavyo Maarifa ni mafungu ya ujuaji wenye namna fulani ya kujipangilia/kupangiliwa katika akili ya mtu—ujuaji wa kuja kwa ile kawaida yenye kupitia fahamu za kimwili; na maarifu ni vipawa vya utambuzi kwa milango ya fahamu ya ndani kwa ndani ya Usentienti wa Kiumbe kukadirisha muktadha akilifu wa '
Kujua kwa Jinsi ya Rohoni'...
Kiufundi, 'infaransi' na 'maarifu' ni mlango wa mafahamu kuhusiana na 'vituo vya kiwakati' ambavyo hata dhana ya 'Wakati' inaweza kuja kuwa tofauti kabisa na kile kinazoeleka na kusadikika kama 'mkatizo wa muda'; Kuwa kwamba, labda hata 'mkatizo wa muda' si lolote ila mabadiliko/mageuko ya 'Vizio vya Khabari' vyenye kulandana na tena kushahibiana na 'Vituo vya Kiwakati'.
Kwa mintarafu ya haya, 'fizikia ya mambo' hukutana na 'metafizikia ya mambo' kwa 'Metafanusi'--Metafanusi ya (1) Khabari-dhahiri, na (2) Khabari-Templati, na (3) Khabari SHAURI/NIA/DHAMIRA. Basi ndiyo yawa, UAKASHA katika SUPASHA ni daraja la 'Mazingira' na '
Mazingara' ya Yote na Vyote-- ambavyo vyote tuvishuhudiavyo, kuna namna hivi vyote ni 'Viini Macho'--Mambo ya '
Maya' na '
Uono Mifumo'...
Kiufundi, fizikia na metafizikia ya 'vituo vya kiwakati' na 'vizio vya khabari' ndiyo mambo ya wakati kuwa ni 'fumbo la imani' na tena 'kioo' cha akili na kujitambua kwa kiumbe chochote chenye Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu; ambavyo, viumbe vyenye kushiriki 'kianzio kimoja cha vituo vya wakati' hushiriki hili pia basi, kwa kiasi fulani, 'vizio vya khabari' kwa 'mambo shirikishi' ya 'Nyakati'.
Kwa mintarafu ya haya, kila mwanajamii katika jamii ana namna fulani mafungamano ya kiakili na utambuzi kwa yale yote yanayotendeka na kuonwa/kushuhudiwa, kutafsirika hivi ama vile kwa wakati, ijapokuwa kila kiumbe kina wakati/mkondo wakati wake wa kujitegemea. Basi ndiyo yawa, jambo lolote linalodhihiri/kudhahirika na kujumuisha utendaji na dhamiri za viumbe vyenye usentienti linanamna fulani ya kuwa na asili ya 'makubaliano' ya kiakili na kiutambuzi--makubaliano yanayochomozea kutoka kwenye 'ungazi wa Khabari-Templati' ambavyo ndiyo khasa hukadirisha 'vitovu cha kiwakati' na 'vizio vya khabari'...
Kiufundi, jambo lolote linalodhihiri/kudhahirika na kujumuisha utendaji na dhamiri za viumbe vyenye usentienti, lina fizikia na metafizikia yake--fizikia na metafizikia ya 'Uweza, Nguvu na Utukufu' wa 'Kiunishati Khabari' ilivyo ni mazingira na
mazingara ya (1) Ukuwa, na (2) Ukuja-kuwa; kimadhahirisho na Uwepo.
Kwa mintarafu ya hivi, lile jambo linaloweza kuzungumzwa kama
'kusafiri kiwakati' ni uwezekano daima--hili hutegemea fahamu na mafahamu ya fizikia na metafizikia ya (1) Khabari-dhahiri, na (2) Khabari-Templati, na (3) Khabari SHAURI/NIA/DHAMIRA.
Basi ndiyo yawa, mazingira na
mazingara ya muktadha akilifu wa chochote cha mfano wa mtenda-kitendo-Tokeo ni '
maya/viini macho' -- viini macho vinayotegemeana na (a) Khabari-dhahiri, na (b) Khabari
SHAURI/NIA/DHAMIRA kupitia UIMAJINISHI. Na tena, uimajinishi ni 'daraja' kwa mambo ya kudhahirika na mambo yasiyodhahirika…
== Mafikara na Ufikirifu : Vikomo vya Kiutambuzi ==
Kiuono na Ufikirifu Mifumo, Uimajinishi ndiyo jambo linalokutanisha (1) Moto, (2) Upepo, (3) Ardhi/Nchi, na (4) Maji kwenye SHAURI lililo MOJA; ambavyo 'fizikia' kuwa 'metafizikia' ni uwezekano kupitia (1) Msalaba wa Mapana yasiyo na Mwisho, (2) Mwezi na Nyota ya Umbalamwezi wa Fahamu katika Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu, (3) Swastika ya Mashikizano ya Khabari na Utendaji wa Miili ya Uzima/Kosmosi; ilivyo ni daima fanusi ya (i)'Masokotano ya Pumzi : (ii)Ujizungurusho wa Sayari na Nyota na Falaki: (iii)Ugravitali wa Mashauri yaliyofanyika Dhahiri kama Nyota, sayari na Kosmosi, na (4) Mboni AJNA ya mawezekano ya akili na utambuzi kwa yote katika 'Kumbukumbu ya Akili ya Uzima wa Yote'--kinasibu ya namna zote Mbegu za u-JUA-ji.
Kwa mintarafu ya haya, Uono na Ufikirifu Mifumo ni shughuli ya akili na utambuzi wenye kutangamanisha (1) Finati: Yale yenye Mwanzo na Mwisho, na (2) Isifinati: LENYE/yenye kutokuwa na mwanzo wala mwisho. Basi ndiyo yawa, (1) 'Msalaba' na 'Swastika' huwa mahusiano ya 'Kimuundo' na 'Miongozo' ya kiutendaji kuwepo kana pembe mkabala; kama ilivyo pia kwa (2) Mwezi na Nyota huwa pembe mkabala na Mboni AJNA kwenye
YANTRA DHAMMA.
Kiufundi, mambo ya Finati na Isifinati ndiyo ufunguo wa mashauri yanayokutanisha fizikia na metafizikia kwa 'Metafanusi'--Metafanusi iliyo ni 'Uungu' katika vyote na iliyovyote.
Kwa mintarafu ya hivi,
Mungu kama dhana ni udhanifu wa kibinadamu kwa kile kinachopitiliza 'Uimajinishi' wa fahamu na mafahamu yao kuhusu asili, uzima wa miili na mazingira dhahiri; ambavyo namna yoyote ya 'Unafsi' wa 'Mungu' ni ufaraguzi wa kimashauri na simulizi-ngano za kibinadamu kwa ajili ya yale wanayodhani wanafahamu na wasiyoyafahamu kuhusiana na
Mazingira na Mazingara ya akili na utambuzi wao.
Basi ndiyo yawa, hakuna Mungu kama 'Nafsi' khasa; kwa kuwa hata kama binadamu na wanadamu--wanadamu wa Duniani kwa mfano na '
utaasisi wao fulani wa (ki)dini' wangalipenda awepo Mungu wa namna hiyo; na khali kumbe : katika Ulimwengu wa Zilioni kwa Mazilioni, na labda isivyo na idadi kabisa, ya Viumbe hai-- viumbe hai katika Sayari, Mifumo ya Ma-Jua, Falaki na Makundi ya Falaki; maajabu ya mtu mmoja 'kuongea na Mungu' ni kadiri ya Mungu huyo huyo kuwa na uwezo wa kuongea na Zilioni kwa Mazilioni ya viumbe hai kwa wakati ama hata daima(?)
Kiufundi, mambo ya Finati na Isifinati ndiyo ufunguo wa mashauri yanayokutanisha fizikia na metafizikia kwa 'Metafanusi'--Metafanusi iliyo ni 'Uungu' katika vyote na iliyovyote.
Kwa mintarafu ya hivi, 'Metafanusi' ni muktadha akilifu wa mawezekano ya 'Mungu Mmoja' anayeweza kuongea na viumbe zilioni kwa zilioni au ndiyo tuseme viumbe vyote tu kwa wakati mmoja na daima.
Basi ndiyo yawa, Metafanusi ilivyo ni 'Uungu katika vyote na iliyovyote' ni shauri kwa ukweli wa kwamba viumbe vyote vyenye Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu vipo na 'mawasiliano ama/na ukaribu na Mungu' wakati wote kwa namna ambayo labda fahamu na mafahamu ya kibinadamu hayajakaa vema kwa wakati ilikulandana na kumaizi ukweli wa mambo/jambo lenyewe...
Kiufundi, mambo ya Finati na Isifinati ndiyo ufunguo wa mashauri yanayokutanisha fizikia na metafizikia kwa 'Metafanusi'--Metafanusi iliyo ni 'Uungu' katika vyote na iliyovyote.
Kwa mintarafu ya hivi, kiumbe chochote chenye Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu kinahitaji namna fulani ya kujiweka kiakili na utambuzi ili ki-JUE na kumaizi ya Kwamba ipo asili ndani yake inayofanya yote na vyote kuwa 'MOJA'--moja iliyositirika na khali hii inafanya uwezekano wa vitu vyote ulimwenguni kuwa na 'mawasiliano' ya kimiili ya Uzima, Akili na Utambuzi.
Basi ndiyo yawa, kile ambacho kutoka kwenye Vitabu vya Injili kupata kusemwa na Yesu ya kwamba "
Ufalme wa Mbingu U Karibu"; U ndani ya Mtu – Mtu na Vyote... NI UKWELI KHASA WA MAMBO…
== Mafikara na Ufikirifu : Uchakataji Khabari ==
Kiuono na Ufikirifu mifumo, kutaniko la SUPASHA, MAADA, WAKATI na NISHATI katika '
Jicho Mashoto la Horasi' ni Muktadha akilifu wa lugha-alama-picha kwa 'Ufalme wa Mbingu'; ambavyo asili ya Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu hukadirisha yote yenye kuwa finati na Isifinati katika Fahamu na Mafahamu. Kwa mintarafu ya hivi, dhana ya kusema Mungu yupo mahala pote... Mungu hana mwanzo wala Mwisho... na pia Mungu ni yule yule leo, jana na Kesho... ni mbegu ya U-JUA-ji wa Konstrakti za fahamu na mafahamu ya miili dhahiri na miili isiyodhahiri ya miili yote yenye Uzima.
Basi ndiyo yawa, kuna wakati wanadamu 'walifahamishana' ya 'Uungu' kwa simulizi-ngano na khabari zilizo ni ujuaji wa mambo kwa sehemu; ambavyo mtume Paulo alizungumza kinaga ubaga kwenye kumbukumbu ya barua kwa Wakorinto, Waraka wa Kwanza, sura ya 13...
Karne hii ya 21, SASA, tunaingia kujua na kuyafahamu yote kwa miongozo ya ukamilifu wa akili na utambuzi ili KUJIFAHAMU kama vile TUNAVYOFAHAMIKA katika METAFANUSI ya Uzima wote.
Kiufundi, usentienti ni pembetatu ya (1) Upumzi, (2) maingiliano ya pumzi na (3) Msalaba wenye utanuko usiyo na ukomo wa vyote na yote; ambavyo kinyume cha hili ni 'Unukta Sifuri' isiyokadirika kitovu chake cha 'Ukuwa ama Ukuja-kuwa'.
Kwa mintarafu ya hivi, ualama-lugha picha ya (1) Uduara, (2) Msalaba, (3) Isifinati na (4) Nukta; ni analojia miongozo ya kiakili na utambuzi kwa Metafanusi, Fahamu na Mafahamu ya Miili-dhahiri na Miili iliyositirika.
Basi ndivyo yawa, (1) 'Duara na Nukta' ni ualama-lugha-picha ya 'Ontolojia ya Taasisi'; (2) '
Pembetatu yenye Jicho Mashoto la Horasi' ni alama ya 'Usentienti' na basi 'Intelijensia' – uweza, nguvu na utukufu wa kuona yote kadiri vile kuwepo kote na ndani ya yote; (3) Msalaba ni ualama-lugha-picha ya konstrakti za 'Miundo na Miongozo' inayokadirisha kitu kufanyika kutokea kwenye kutofanyika--kufufuka kutoka kwenye mauti--kutoka uzima wa miili kwenda mautini. Tena basi yote ya uzima wa miili na 'malango ya mauti' ni viini macho katika Metafanusi kwa kuwa asili khasa ya Metafanusi ni 'UZIMA WA MILELE'...
Kiufundi, Msalaba kuwa ni ualama-lugha-picha ya konstrakti za 'Miundo na Miongozo' inayokadirisha kitu kufanyika kutokea kwenye kutofanyika ndiyo msingi wa '
TORATI'; ambavyo torati maana yake ni 'MIONGOZO' kwa uweza, nguvu, sura na utukufu wa kiumbe ama chochote chenye
kujikadirishia namna ya kujiwazia utu kwa mfano Jamii/Taifa/Dola/Jeshi n.k.
Kwa mintarafu ya hivi, mambo ya 'uingiliano wa pumzi' ndiyo asili ya 'Uzima wa Miili' ambavyo kila kilicho hai huishi na kustawi kwa kuwa kimo ndani ya kingine chenye kuishi na kustawi 'isivyodhahiri'.
Basi ndiyo yawa, Mtume Paulo kuzungumza kuhusu 'Mwili wa Kristu' ni jambo lililo ni UKWELI KHASA WA MAMBO kwa kuwa
'Mwili wa Kristu' si chochote bali 'Metafanusi' ya fizikia na metafizikia ya 'Umwili wa Nyama, Fizikia ya Miili Sayari/Jua na Namna zake za Akili, Fahamu na Mafahamu'... Tena basi kwenye fahamu na mafahamu, utendaji wa yule anayeishi kufahamu sehemu yake katika 'mafahamu ya mwili wa Kristu' ni mkuu zaidi kuliko yule asiyetambua ama/na kujitambua katika 'Mwili wa Kristu'...
Kiufundi, Urizayati ya KUBU ya MAGEUZI ni ualama-picha-picha wa konstrakti za 'Mageuzi Sura' ya dhahiri zote za kifahamu na mafahamu; ambavyo 'mapana ya umpumzi wa miili' husitirika ndani ya mwingine kwa maingiliano ya Upumzi.
Kwa mintarafu ya hivi, muktadha akilifu wa fahamu na mafahamu ya uweza, nguvu, sura na utukufu wa kiumbe chochote chenye Usentienti ni uhamonifu wa Upumzi wa madhahiri ambavyo Udhamiri wa Duara na Nukta kwa Ukuwa ama/na Ukuja-kuwa kukadirika kwa mlandano wa 'mapana-marefu-kina' ya kitu/jambo 'MOJA' la kifahamu na Mafahamu.
Basi ndiyo yawa, Ulimwengu wote ni Kitu/Jambo moja kimafumbo ya Uzima juu ya Fahamu na Mafahamu ya 'Uono Mifumo'--Uono Mifumo ulivyo ni muktadha akilifu wa kumbukumbu la (1) Kitovu/vitovu vya Wakati, na (2) Vizio vya Khabari…
== Makadirifu ya Utambuzi : Dhahiri na Dhahania ==
Kiuono na Ufikirifu Mifumo -- Mifumo ilivyo ni muktadha akilifu wa kumbukumbu la (1) Kitovu/vitovu vya Wakati, na (2) Vizio vya Khabari ni maajabu na mastaajabu ya 'ukuwa ama/na ukuja-kuwa' wa vyote ambavyo 'miili, akili na Nuru ya Ufahamu' ni maingiliano ya Upumzi kifizikia na tena metafizikia.
Kwa mintarafu ya hivi, wakati ni kioo cha '
Kumbukumbu la Torati' ambavyo udhamirifu wa utu, ukuwa ama/na ukuja-kuwa, na mchakato wa kutafuta 'ukamilifu wa Sheria' ilivyo ni 'Metafanusi'. Basi ndiyo yawa, ule usemi ya kwamba Uzima ni Kristu na Kufa ni faida ni Shauri la '
Hekima katika Ufahamu wa Kimetafizikia' ambavyo hatma za mambo ya 'Miili na Roho' hutenda kwa Uajabu wa 'Uongo na Ukweli' wa ule
uzima khasa wa miili yenye Usentienti, Kosanyansi na Nuru ya Ufahamu...
kiufundi , Uongo na Ukweli wa miili yenye Usentienti, Kosanyansi na Nuru ya Ufahamu ndiyo asili khasa ya lile jambo la 'mafumbo ya kifahamu na utambuzi' yanayoleta nasibu ya '
Majaribu ya Kiutu' inapokuja kwenye mapana ya maisha na kujichagulia--maisha na kujichagulia katika alamu za 'Uisho na Kufanyika'.
Kwa mintarafu ya hivi, asili khasa ya uadilifu wa kiutu, maadili na miiko ni mchakato hai wa Usentienti wenye kudhamiria 'Kutoboa' kutoka kwenye ulimwengu usiyokamilifu wa 'Kiwakati', na kuja-kuwa basi, kitendo cha kutobozea kwenye Metafanusi inayositiri yote--
yote yaliyo katika wakati na kupitiliza konstrakti za wakati wenyewe.
Basi ndiyo yawa,
Uongo ni ile sifa na hadhi ya mtu mwenye udhamirifu pofu wa mahitaji ya kimwili usiyokamilifu, mwili wa udongo;
Ukweli ni sifa na hadhi ya mtu mwenye udhamirifu wa ku-JUA ilivyobora ili ajinasibu kufanyika upya katika mwili usiyovaa kuharibika -- apate '
kuukomboa wakati'...
Kiufundi, Uisho na Kufanyika', ni mambo ya vitendo vya kiwakati ambavyo Usentienti daima unafanania na
pembetatu iliyonasa kwenye mapana yenye kupindua na kujipindua katika konstrakti za miundo na miongozo ya udhamirifu wa utu na tena kushiriki 'vituo vya wakati' na ujumuifu wote wa pumzi muingiliano wa wote na vyote vyenye kujidhahirisha kwenye KUBU shirikifu ya Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu.
Kwa mintarafu ya hivi, maisha na mifumo yote ya maingiliano ya uakili na utambuzi ni alamu za uisho ambavyo utu wowote una kadiri ya uwimbi wa pumzi ya uzima kutoka kwenye 'maji ya uzima'--
miili inayoshiriki 'ulimwengu mmoja' ina uhamonifu wa kasi ya utetema wa Eitha ya 'Maji ya Uzima'. Basi ndiyo yawa, Shauri la Injili ya Yesu kuhusiana na '
Maji ya Uzima na Kiu' ni simile ya metafo ya SUPASHA na UTIMILIFU wa Sura na Hadhi za 'Uhitaji' na 'Kujazia/Kujijazia Uzima Zaidi' --Uhamonifu pitilizi wa utetema wa Eitha, unaoathiri 'Nguvu na Utukufu' wa Uisho na Kufanyika...
Kiufundi, '
Nguvu na Utukufu', ni mambo ya 'Mapinduzi Daima' ambavyo '
Shauri na Uzuri' wa yote na vyote huishi na kufanyika kwa 'Kadiri' na 'Kudra' ya Mawimbi ya Maji ya Pumzi ya Uzima--
'Maji ya Uzima' yaliyo ni bahari ya Chanzo na Nuru ya Ulimwengu wote mzima.
Kwa mintarafu ya hivi, kila kitu kimefanyika kwa pumzi iliyo ni kadiri ya nguvu ya uweza na utukufu wa '
Jina Kuu' ambavyo daraja la mageuzi ya 'nguvu na utukufu' ni 'fanusi ya upatanishi' wa mambo ya '
mbingu na nchi'--Swastika ya ujizungurusho wa mafumo yote ya sura za vitu na mambo yake.
Basi ndiyo yawa, Mapinduzi Daima ni jambo la '
Enzi na Utukufu' wa Ukuwa na Ukuja-kuwa ambavyo Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu unajaa uwezo kutawala mambo ya mbingu na nchi... Na tena, mapinduzi daima ni ufunguo wa 'Maarifa na Maarifu' ilivyo ni
Rizayati ya Elimu 3.0…
== Makadirifu ya Utambuzi : Utaasisi wa Mashauri ==
Kiuno na Ufikirifu Mifumo, 'kadiri na Kudra' ya chochote kilichofanyika ndiyo asili ya
Fizikia ya Unavigati wa Kikwantumu ambavyo dhana za ufundamentali wa nguvu za uweza ni nasibu ya hata yale mawezekano ya 'elektroni' kuruka kutoka kwenye ngazi moja ya unishati na uwepo hata ngazi nyingine pasipo kukatizia popote khasa pa kiusupasha.
Kwa mintarafu ya hivi, Fizikia ya Kikwantumu kwa mashauri ya Sayansi ya Mkondo Mpana, sayansi 1.0,
hugubikwa na vielelezo na vina vya tafsiri vilivyo mushkeli kwa kukusudiwa ama pasipo kukusudiwa kulingana na vikomo vya infaransi za kihisabati, udhanifu na umodelishi wa 'miundo' ya madhanifu ya kitaswira za maasili ya kimaada.
Basi ndiyo yawa, kile ambacho kinaweza kutajwa ni '
Povupovu la Kikwantumu' ama/na '
Mafungamano ya Kikwantumu' ni nasibu ya yote mawili: (1) 'Maji ya Uzima' yaliyo ni bahari ya Chanzo na Nuru ya Ulimwengu, na (2) Utowepo wa umbali ama umahala kwa 'Sifa na Hadhi' ya unamna fulani wa vitendo na miundo ambavyo 'Khabari/mafungu vitendo-miundo' vinaweza 'kusafirishwa' kutoka nukta moja hata ingine pasipo muda/uwakati--kwa sehemu kufanania na
madhanifu ya 'kutandua' usupasha-wakati.
Kiufundi, 'Povupovu la Kikwantumu' na 'Mafungamano ya Kikwantumu' ni jambo lile lile lenye kushahibiana na
'Swastika' na 'Mboni AJNA' kwenye Yantra Dhamma ambavyo kwenye mashauri ya fizikia, sayansi 1.0, yote mawili:
(1)Makiniki ya Relativo ya Makawaida, na (2) Makaniki ya Kikwantumu, Muona huathiriana moja kwa moja na 'Matokeo' ya anachokiona ama mashauri ya infaransi kiakili na utambuzi.
Kwa mintarafu ya hili, Uono una asili ya 'kupangana' na kinachoonwa katika ufundamentali wa dhahiri-miundo-vitendo ambavyo kile ambacho hutajwa ni '
Ujizingurusho' huja kwa 'upacha' wa 'kimiundo-vitendo' vya nasibu kwa lolote lenye asili ya 'upovupovu' wa Kiontolojia.
Basi ndiyo yawa, (a) Mboni AJNA kuwa na Pembetatu Inayotazama chini ni jambo pacha kwa (b) Pembetatu ya uakilifu na utambuzi kwa fahamu na mafahamu ya kiumbe chochote chenye Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu. Tena basi,
asili khasa ya uono na utambuzi ni 'Mfumo' ambavyo lugha-alama-picha ya (1) 'kitendo' ni pembetatu iliyoegama kiutostabali wa 'ulali wa muundo'; (2) 'Dhamira' ni pembetatu iliyondani ya kadiri ya kudra ya uduara wa pumzi, na (3) Ukumbukumbu wa 'mambo yafananiayo/kuakisiana kifizikia na metafizikia'.
Kiufundi, uweza-nguvu-utukufu wa chochote kitokanacho na umawimbi pumzi ya maji ya uzima ni jambo la konstrakti za (1) Uduara, (2) Upembetatu na (3) Umraba ambavyo (a) uduara ni asili ya 'utufe' ama uchembe--uchembe mbegu wa yote na vyote ilivyo asili ya mtanuko usiyo na mwisho mfano wa Sayari, Jua/Nyota, (b) Utetrahedrani wa asili ya kazi/utendaji--mfichamo wa 'nguvu' katika 'miundo na dhahiri', na (c) Ukubu ilivyo ni asili ya usawazishaji wa nguvu za kimpumzi ya madhahiri kifizikia na metafizikia.
Kwa mintarafu ya haya, kila kilichofanyika 'Sura na Sifa ya Kimaumbile' kina asili ya 'pumzi ya kuja' ndani na 'pumzi ya kutoka nje' -- upumzi unayosawazishwa kwa fizikia na metafizikia ya 'UKUBU' ambavyo fumbo la wakati na nyakati ni sehemu ya UKUBU ilivyo ni 'Kumbukumbu la Uzima'.
Basi ndiyo yawa, kila kilichodhahiri na kudumu sura fulani ni zao la pumzi mbili zinazokutana katika (1) Vituo vya wakati, na (2) 'Vizio vya Khabari... Na tena, Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu ndiyo khasa 'Mkuki wa Moto wa mageuzi'-- wenye nasibu ya uweza wa kutenda ilivyo
MUONA KUWA NI MUONWA--Utetrahedrani wa
'Dhamira, Uono na Nia'; uwavyo pacha kwa 'Vina vya tafsiri vya udhamirifu wa shauri, Ujinetifu wa Maumbile hai, na Ushawishi wa mabadiliko ya Sura na Hadhi ya Mazingira na Mazingara ya 'Mapana ya Ustawi'.
Kiufundi, shauri la 'Ujinetifu wa Maumbile hai' ndilo khasa jambo la 'Mbegu ya u-JUA-ji inayofadhili na kuruzuku uadilifu wa 'Kumbukumbu la Uzima wa Miili' ambavyo Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu kupata kitovu cha Ontolojia ya Taasisi kwa kheri ya Milele.
Kwa mintarafu ya hivi, Ujinetifu huja kwa Mbegu ya u-JUA-ji ambayo kwenye khabari za Injili ndiyo hutajwa ni 'NENO'; ambavyo shauri la Ujinetifu linaetimolojia ile ile na Jinesesia: Mwanzo wa yote na Majira ya 'Usiku na Mchana' wa yaliyofanyika kwa mfano wa 'Anayeumba kwa Mfano wake'--
UIMAJINISHI.
Basi ndiyo yawa, kila kiumbe chenye Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu kinaumba wakati wote ule uhali halisi wake wa
'Mazingira' na 'Mazingara' kwa Dhamira/Vitendo/Mafikara iwe kwa 'ku-JUA' ama 'kutokujua'.
== Makadirifu ya Utambuzi : Utaamuli wa Shauri ==
Kiuno na Ufikirifu Mifumo, 'shauri la Ujinetifu wa Maumbile hai' ni lile jambo khasa la '
Uzabibu 13' ilivyo ni asili ya kile kinachoweza kutajwa kama (1) 'UFAHAMU KRISTU' kwa upande wa 'Mkuki wa Moto wa mageuzi' wenye nasibu ya uweza wa kutenda ilivyo
MUONA KUWA NI MUONWA; na (2) Fanusi ya
Metatroni kwa upande wa 'Vitovu vya Wakati' ambavyo viumbe vyote vyenye Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu hujikadirishia 'Udhamiri wa Kujichagulia' ule
Usahihi wa Kimfumo.
Kwa mintarafu ya hivi,
namba 13 ni akitipu ya "MAGEUZI" ambavyo kwa Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu; uwezekano upo wa (1) Kuwa ama/na (2) Kuja-kuwa chochote kwa 'utatu' wa Dhamira, Shauri-Uono na Nia.
Basi ndiyo yawa, Uzabibu 13 hujitokeza kwenye
kradrati ya 'NISHATI' kama 'kiini cha kadiri na kudra ya ujinetifu wa kimsokotano'--msokotano wa 'pumzi za uzima wa kimiili'; hujitokeza kama 'kiini cha Mbegu ya u-JUA-ji' kwa '
Kujisikia' kwenye Trizaniamu... Tena basi,
lugha-alama-picha kwa kujisikia, kwenye Yantra Dhamma hujitokeza kama 'Magharibi ya Maji'...
Kiufundi, 'Magharibi ya Maji' ina 'Mashariki ya Upepo' ambavyo 'Kusini ya Nchi/Ardhi' ina 'Kaskazini ya Moto' kwenye Yantra Dhamma; kuwa kwamba Maisha na Uisho ni Mraba wa (1) Jamii/Mwanajamii, (2) Machaguo ya Kitaasisi, (3) Wakati, na (4) Matukio/Matokeo ya Vitendo.
Kwa mintarafu ya hivi,
noumenoni ya madhahiri yote ni zao la kemia na alkimiya ya 'Neno Kutwaa Mwili' na 'Ushiriki wa Shauri' -- Shauri lilivyo 'Miundo na Miongozo' ya (1) Nuru ya ufahamu kwa akili na utambuzi: Ontolojia ya Taasisi, (2) Mapana ya Kosmosi yenye kufadhili na kuruzuku Jitihada za kiumbe chenye Usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu: Mapenzi katika 'Mbingu na Nchi', (3) Nguvu ya Nia na Nidhamu ya Kujichagulia: Konsayansi, (4) Udhamirifu wa Furaha ilivyo ni ushirika wa Kimiili: Usentienti.
Basi ndiyo yawa, kutoka kwenye Khabari za Injili, Usentienti wa Kristu hujitanabaisha na kupata kuwa (a) Mimi ni
Nuru ya Ulimwengu: Mwangaza Juu ya Mlima Kilimanjaro, (b) Mimi ni
Mkate wa Uzima: Shamba la Ngano Safi na Tumaini la Uhai wa Kisayari Dunia kwa utaswira wa "Mazingira" -- Mbayuwayu Juu ya Nyika na tena pembezoni pa Maji, (c) Mimi ni
Pumzi ya Uzima: Ndovu wawili wenye kusigana nguvu ya uweza katika asubuhi ya '
Nyota Njema ya Asubuhi', na (d) Mimi ni
Maji ya Uzima: Dhamira ya Simba mwenye kuweka Moyoni yote ya Dunia na Usentienti wake iwe kuwa ni Ujasiri kwa Shauri la Upendo na Uhifadhi kwa ujinetifu wa '
Nia ya Kristu'...
Kiufundi, 'Nia ya Kristu' ni lile jambo khasa la kuyashinda 'Majaribu ya Kiwakati' yenye kuja maishani kulingana na dhamira ya kujiwazia utu na utukufu wake; ambavyo
'Ontolojia ya Taasisi', ilivyo ni Uungu --uungu unaojaalia nasibu na mawezekano ya 'Kuushinda Wakati'.
Kwa mintarafu ya hivi, Nia ya Kristu ni
Hekima yenye kutangamanisha 'Lila na Fila' ilivyo ni Uono na Ufikirifu Mifumo ambavyo '
Jiwe la Mfilosofia', Mfilosopfia ni mtu Mwenye Mapenzi na Hekima, ni uweza na ujuzi kugeuza kila kiguswacho 'Kuwa Dhahabu' kwa Dhamiri, Uono ni Nia yenye 'kadiri na kudra' za
USHEKINAHI.
Basi ndiyo yawa, Ushekinahi ni jambo/kitu kile kile ambacho kwenye mapokeo ya Usufii hufahamika kama '
Arshi'--Uweza wa Kienzi wa 'Mja mwema' katika fahari yote ya 'Mbingu na Nchi'--
mbingu na nchi ilivyo ni 'Maandiko'...
Kiufundi, Uweza wa Kienzi wa 'Mja mwema' katika fahari yote ya 'Mbingu na Nchi' ndiyo jambo lile lile kwenye mashauri ya Injili huja na khabari za Yesu kupata kufundisha mambo ya
'Ufalme wa Mbingu' kufananishwa na Shamba -- Shamba la Ngano na Mpanzi; ambavyo Mbegu za Utu, simile ya metafo ya Ngano safi, huanguka kwenye Udongo na kupambana na zahma, Dunia Msongamano, udhamirifu wa ustawi na hatma zake penye mengi, simile ya Magugu.
Kwa mintarafu ya hivi, Usahihi wa Mimfumo huanza na chachu ya mtu mwenye usentienti, konsayansi na Nuru ya Ufahamu ambavyo hatma za 'Dunia Msongamano' na 'Mambo yake ya Nyakati', ambavyo kuna (1) Nyakati za bahati na (2) Nyakati zisizo na Bahati kwa mafungu ya Watu/Wanajamii katika Ujumuishi wa Mambo na tena Kheri za Mambo yake.
Basi ndiyo yawa, nyakati za bahati ni pale ambapo dhamiri za wengi ni zenye kulandani katika Nia ya Utu Wema; ambavyo
Mema na Maovu katika fanusi jamii huiishi 'Hukumu'…
== Visa na Mikasa ya Jamii: Ufukuzia Vimvuli ==
Kiuono na Ufikirifu Mifumo, 'Dunia Msongamano' na 'Mambo yake ya Nyakati', ndiyo jambo lenye kutuleta kwenye Shauri ya Karne hii 21 kuwa ndiyo 'Nyakati za Hukumu'; ambavyo Usahihi wa Kimfumo huanza na chachu ya mtu/watu (m)wenye usentienti, konsayansi na Nuru ya Ufahamu wanakuja kuwa ni 'Wafanya hukumu kwa Wazima na Wafu' kwa jamii za watu/walimwengu --katika Ujumuishi wa Mambo na tena Kheri za Mambo yake.
Kwa mintarafu ya hivi, kutoka kwenye khabari za Injili dhana ya
'Mavuno' na 'Ufalme Kuja/Kurejea kwa Kristu' ndiyo Shauri la
'Malaika' wa kutenganisha 'Ngano na Magugu'; ambavyo hatma za 'Dhamira Nzuri na Mbovu za Utu--Utu Jamii'
hupata hesabu yake. Basi ndiyo yawa, mambo ya mavuno ndiyo khasa Dhamira, Uono na Nia ilivyo ni '
Sala ya Bwana'.
Kiufundi, Shauri la
'Malaika' wa kutenganisha 'Ngano na Magugu' ni jambo lile lile la "
Neno Kutwaa Mwili" ambavyo wanadamu wenye nasibu ya akili na utambuzi wa Ufahamu Kristu, kwa kuzaliwa kuishi na kujichanganyikana na wengine wote; wawa ni watendaji wenye kukadirisha kule kujitenga kwa (1) Mashauri ya Uongo/Yasiyo na ukamilifu na (2) Mashauri ya Ukweli/Yenye Uzima wa Usahihi wa Kiuno na Ufikirifu Mifumo: Uongo ama ukweli kwa yote ya sura, hadhi na mienendo ya mambo ya jamii za 'nyakati za mwisho'.
Kwa mintarafu ya hivi, nyakati za bahati ni nasibu ya '
Mwangaza' wa kumulika njia za wanajamii na basi kutenganisha wale wenye kuwa tayari kujua mambo ilivyo bora na wale wasiotayari kuyaona maisha katika mwangaza bora. Basi ndiyo yawa, nyakati za bahati ni wakati ambapo miundo na miongozo ya wanajamii waliotayari 'kuongozeka', kuongozeka katika njia zenye kheri, hupata kioo cha ung'amuzi kwa wakati wenyewe.
Kiufundi, nyakati za bahati ni sura ya hadhi na utukufu/utabia wa jambo/mambo kujipangilia kwa namna yenye afueni ama/na kufaa 'masafi' ya kiutu, na uhitaji wake kiwakati, ambavyo
UJAZI ni zao la 'Riziki na Haki' ya yeyote mwenye kuishi katika khali ya Neema.
Kwa mintarafu ya hivi, ile namna ya mtu kukipata chochote kile kwa muda muafaka kulingana na 'mafikara na dhamira'--mafikara na dhamira kuakisika kwa namna ya wakati wenyewe kuwa kioo cha 'ukuwa' ama Ukuja-kuwa.
Basi ndiyo yawa,
namba 11 ni namba ya Miakisiko na 'Miongozo' ya Kimuundo, kama ilivyo lugha-alama-picha ya miongozo kuwa msalaba wa 11; ambavyo hata kule
mtu kuona tena na tena majira 11:11, labda tuseme 11:22|11:33|11:44 n.k, kwenye vitu kama saa, ama namba za kujitokeza huku na kule ni 'ishara' ya 'nyakati za bahati'--dalili ya fizikia na metafizikia ya utu, katika Uungu/Metafanusi,
inatengeneza daraja la ku-JUA na Kuji-JUA...
Kiufundi, nyakati zisizo za bahati ni sura ya hadhi na utukufu/utabia wa jambo/mambo kuwa na disonia ya 'miundo na miongozo' ambavyo
sura, hadhi na utukufu wa ujamii wa viumbe hai vyenye usentienti, konsayansi na nuru ya ufahamu vinatawaliwa na mafikara na kujiwazia utu kulikodhibitiwa kulingana na fahamu na mafahamu ya viumbe vyenyewe kwa wakati.
Kwa mintarafu ya hivi, ulimwengu wote ambao usentienti, konsayansi na nuru ya ufahamu – ufahamu wa namna ya akili, utambuzi na kujitambua kufumbwa ama kudhibitiwa ukweli wa hatma yake kimageuzi na utukufu ndiyo mfanyko wa 'Matriksi'.
Basi ndiyo yawa, asili khasa ya matriksi ni '
Kumbukumbu Uzoefu' ambavyo yote mawili ni uwezekano: (1) Fanusi Ibilisi, ama/na (2) Fanusi Kristu; na tena, ukomo wa kimafikara na uimajinishi ni namna ya kudhibiti jamii yoyote, Duniani ama Sayarini kokote, kuwafanya wanajamii wake 'wanase kwenye ulimwengu wa 'mambo ya wakati' na Kheri ama Ubatili wake wowote…
== Visa na Mikasa ya Jamii: Fanusi ya Ukombozi ==
Kiuono na Ufikirifu Mifumo, kinachoweza kuwajaza wanajamii ile nguvu ya usentienti, Konsayansi na Nuru ya Ufahamu kupilitiza mapana na marefu na kina na kimo cha 'Matriksi' ni '
Roho ya Akili na Utambuzi' yenye kutanua nasibu ya mafikara na uimajinishi katika jamii yeyote iliyokwama kwenye mambo ya wakati.
Kwa mintarafu ya hivi, iwe Duniani ama kokote kule 'Hekima ni Uhuru' ambavyo kile ambacho hutajwa ni '
Roho Mfariji' kwenye khabari za Injili ni 'Intelijensia' yenye kuweza kudumu hata katikati ya muktadha akilifu wowote wa 'Wema ama/na Uovu'.
Basi ndiyo yawa, kile ambacho kwenye Injili huzungumzwa ya '
kutumwa katikati ya Kondoo na Mbwa Mwitu wakali' ama pia '
Kuwa Werevu kama Nyoka na tena wapole kama Hua' ni mambo ya 'Intelijensia' na 'Ukesha Macho/Vijilansi' ili kuinasua/kuilinda jamii yoyote kutoka ndani ya hila za kimifumo na usalama wa jamii--kwa kuwa kokote ulimwenguni, kwa wakati hata wakati, 'Kikulacho huwa Kinguoni mwa Jamii Yenyewe' na kisha mapana yake Kiustawi...
Kiufundi, 'Kikulacho kuwa Kinguoni mwa Jamii Yenyewe' ni muktadha akilifu 'Ibilisi' kuwa ni dhamira ya ufitini wa UHURU, UDUGU, HAKI na AMANI ya jamii kulingana na 'Dhamira, Uono na Nia' ya utendaji usiyokheri ya kweli ila ufikirifu pofu wa kimakundi/ujinga katika fahamu na mafahamu ya ukweli khasa wa mambo.
Kwa mintarafu ya hivi,
Ufitini ni fanusi ya uweza na Nguvu ya Mafikara ama Khabari kuweza kuathiri moja kwa moja utendaji wa kiumbe chochote chenye Usentienti, Kosanyansi na Nuru ya Ufahamu--kiwe ni cha asili mtu/mwanajamii ama kufikirika kama taifa/nchi-dola/Jeshi n.k.
Basi ndiyo yawa, isishangaze jamii/mwanajamii yeyote akija kufahamu utundu wa '
kufuta kumbukumbu za ukweli wa mambo na matukio' kwa 'nia njema ama mbaya', ama pia kuchomokea simulizi za uongo na kweli kihistoria, ni kitu kilichopo hapa Duniani hata sasa, kimekuwapo na vile vile kinafanyika/kudhamirika hata kwa jamii nyingine nje ya Sayari ya Dunia--kudhamirika na wale wenye kufahamu sehemu ya ukweli huu wa kimifumo, na tena wenye namna, wakiwa kama 'Taasisi ndani ya Taasisi'...
Kiufundi, kufuta kumbukumbu za ukweli wa mambo na matukio kwa 'nia njema ama mbaya ni utundu na udhamirifu wa kudhibiti 'UIMAJINISHI' wa jamii yeyote inayolengwa kufungiwa mapana, marefu na kina cha fahamu na mafahamu yake kwa kuwa uimajinishi ni ufunguo wa 'Uweza na Uungu' ambavyo ukweli ama ushahidi wa chochote unaweza kufungua akili ku-JUA jambo fulani ambavyo kufahamu jambo moja linaweza kupelekea kufahamu na lingine.
Kwa mintarafu ya hivi, udhibiti wa U-JUA-ji wa mambo hapa Duniani umedhibitiwa kwa 'Mashauri ya Utaasisi wa Dini' kuhusiana na fizikia na metafizikia ya mambo ambavyo khabari, masimulizi na mafumbo ya Imani yanatengenezwa/yametengenezwa kushawishi mafikara ya makundi tofauti ya makundi ya waumini wenye kuja kuridhia 'mafundisho' yake.
Basi ndiyo yawa,
siyo kwa kuwa: huenda yale yote yanayokuja kwa 'Utaasisi wa Dini' ni utundu na ufundi wa kujenga mashauri ya 'Imani' na 'Cha Kudhaniwa ni Ukweli wa Mambo' basi yote ni batili ya 'Uongo Mtupu'; kwa kuwa utundu huu una maana ya hata ule ujuzi wa kusuka mambo ya kufanania ya ukweli wa mambo na tamu tamu ama khofu za '
kuiteka akili' kwa yeyote yule ambaye kimfaacho ni chake…