6 Pack
JF-Expert Member
- Apr 17, 2022
- 2,819
- 5,996
Niaje waungwana,
Kusema ukweli kwa hali aliyofikia raisi wa Marekani mhe. Joe Biden, ni vizuri akashauriwa au akajishauri mwenyewe kuacha kugombea uraisi wa Marekani ili apate muda wa kwenda kupumzika nyumbani kwake na wajukuu zake. Ikiwa ataruhusiwa kuendelea kugombea na pengine akashinda, basi nitaamini kuwa Marekani ni nchi inayoweza kuongozwa hata na Chid Benz kikubwa tu awe mzawa na mwenye ushawishi.
Haiwezekani nchi yenye uchumi mkubwa, teknolojia kubwa na vyombo vyenye ueledi mkubwa wa kijeshi, kiuchumi, kielimu na kiintelejensia waongozwe na mtu ambae husahau jambo kila baada ya dakika 3 au 5 kupita. Inasemekana hufikia mahali hadi ya kuwasahau mawaziri wake mwenyewe. Waziri wake wa mambo ya nje anamwita Obama na muda mungine akikutana na Obama anamwita Clinton.
Juzi alikuwa katika mkutano wa G7 na viongozi wenzake. Wakati wakiwa wamesimama wakiangalia askari wa miamvuli wanavyoshuka kutoka juu, ghafla yeye (Biden) akawatoka wenzake na kuelekea upande ambao haueleweki. Baada ya mkewe kuona hali hiyo ikabidi amuwahi kwenda kumshtua kwamba huko unapoelekea ni kichakani (ni bustan yenye majani marefu mithili ya kichaka) akamuonesha walipo wenzake, ndo akarudi tena pale alipokuwa amesimama na kuendelea na sherehe yao.
Hiyo tisa, kumi na pale alipofanya kituko kingine katika ikulu ya white house. Wakati walipokuwa wanasherekea yeye na viongozi waandamizi wa ikulu, yeye akawa anatoa machoni mithili ya mtoto anaejaribu kufuatilia kitu asichokijua. Ghafla akataka kuwachomoka ili aelekee anapopajua yeye ndo watu wa karibu wakamtuliza, huku yeye akionesha wazi kusahau kinachofanyika pale 😂😂😂
Hizo picha 3 za juu ni za mkutano wa G7 jinsi alivyowatoka na jinsi mkewe alivyomrudisha katika kundi. Na hizo picha 2 za nchini na jinsi alivyotoa macho kuangalia asichokielewa na pia akitaka kuwatoka watu waliokuwepo katika sherehe hizo.
Nina imani kwa haya anayoyafanya Biden kama yangefanywa na raisi wa nchi yoyote ya Afrika, basi raisi huyo angeandamwa na vyombo vyote vya kimataifa. Ni kama alivyodhalilishwa raisi wa Sudan kwa kuambiwa kuwa kajikojolea hadharan nk.
Kusema ukweli kwa hali aliyofikia raisi wa Marekani mhe. Joe Biden, ni vizuri akashauriwa au akajishauri mwenyewe kuacha kugombea uraisi wa Marekani ili apate muda wa kwenda kupumzika nyumbani kwake na wajukuu zake. Ikiwa ataruhusiwa kuendelea kugombea na pengine akashinda, basi nitaamini kuwa Marekani ni nchi inayoweza kuongozwa hata na Chid Benz kikubwa tu awe mzawa na mwenye ushawishi.
Haiwezekani nchi yenye uchumi mkubwa, teknolojia kubwa na vyombo vyenye ueledi mkubwa wa kijeshi, kiuchumi, kielimu na kiintelejensia waongozwe na mtu ambae husahau jambo kila baada ya dakika 3 au 5 kupita. Inasemekana hufikia mahali hadi ya kuwasahau mawaziri wake mwenyewe. Waziri wake wa mambo ya nje anamwita Obama na muda mungine akikutana na Obama anamwita Clinton.
Juzi alikuwa katika mkutano wa G7 na viongozi wenzake. Wakati wakiwa wamesimama wakiangalia askari wa miamvuli wanavyoshuka kutoka juu, ghafla yeye (Biden) akawatoka wenzake na kuelekea upande ambao haueleweki. Baada ya mkewe kuona hali hiyo ikabidi amuwahi kwenda kumshtua kwamba huko unapoelekea ni kichakani (ni bustan yenye majani marefu mithili ya kichaka) akamuonesha walipo wenzake, ndo akarudi tena pale alipokuwa amesimama na kuendelea na sherehe yao.
Hiyo tisa, kumi na pale alipofanya kituko kingine katika ikulu ya white house. Wakati walipokuwa wanasherekea yeye na viongozi waandamizi wa ikulu, yeye akawa anatoa machoni mithili ya mtoto anaejaribu kufuatilia kitu asichokijua. Ghafla akataka kuwachomoka ili aelekee anapopajua yeye ndo watu wa karibu wakamtuliza, huku yeye akionesha wazi kusahau kinachofanyika pale 😂😂😂
Hizo picha 3 za juu ni za mkutano wa G7 jinsi alivyowatoka na jinsi mkewe alivyomrudisha katika kundi. Na hizo picha 2 za nchini na jinsi alivyotoa macho kuangalia asichokielewa na pia akitaka kuwatoka watu waliokuwepo katika sherehe hizo.
Nina imani kwa haya anayoyafanya Biden kama yangefanywa na raisi wa nchi yoyote ya Afrika, basi raisi huyo angeandamwa na vyombo vyote vya kimataifa. Ni kama alivyodhalilishwa raisi wa Sudan kwa kuambiwa kuwa kajikojolea hadharan nk.