Rais Biden ashauriwa kutogombea uraisi wa Marekani, sababu analiaibisha na kulivua nguo taifa lake

Rais Biden ashauriwa kutogombea uraisi wa Marekani, sababu analiaibisha na kulivua nguo taifa lake

Kuna maraisi huwa wanawekwa mbele kama picha yenye spika ila mamlaka yanatoka somewhere else. Kuna umri binadamu akifikisha hawezi kuwa na control hata ya familia yake anajiachia tu mitoto iamue lolote sembuse nchi, ucontrol mifumo ya wizara zote na kuzitolea maamuzi?.
Ya chini ya carpet inasemekana kuwa sasa hivi nchi inaendeshwa na Blinken, japo Joe ameendelea kuwepo pale kama raisi kimvuli.
 
Kweli kabisa, muda haitoshi hata kusoma na kurekebisha ulichoandika.

Kuhusu Joe Biden, huyo jamaa ni msanii sana kama hamjamjua. Na ana akili timamu almost all the time.

Ni kweli ana tatizo la uzee, lakini wakati mwingine huwa anafanya makusudi ili kutafuta mkogo wa vyombo vya habari (huku kwetu Bongo tunaita kutafuta kiki).
Kama ni kweli kuwa anafanya hivyo kwa sababu za kisiasa basi atakuwa hajui kuwa anajiaibisha sana yey na nchi yake mpaka muda mungine unaona mkewe akihisi aibu machoni.

Mbona miaka ile ya obama hakuwa hivi au pale uzee na ugonjwa alionao sasa ulikuwa haujazidi?
 
Niaje waungwana,

Kusema ukweli kwa hali aliyofikia raisi wa Marekani mhe. Joe Biden, ni vizuri akashauriwa au akajishauri mwenyewe kuacha kugombea uraisi wa Marekani ili apate muda wa kwenda kupumzika nyumbani kwake na wajukuu zake. Ikiwa ataruhusiwa kuendelea kugombea na pengine akashinda, basi nitaamini kuwa Marekani ni nchi inayoweza kuongozwa hata na Chid Benz kikubwa tu awe mzawa na mwenye ushawishi.

Haiwezekani nchi yenye uchumi mkubwa, teknolojia kubwa na vyombo vyenye ueledi mkubwa wa kijeshi, kiuchumi, kielimu na kiintelejensia waongozwe na mtu ambae husahau jambo kila baada ya dakika 3 au 5 kupita. Inasemekana hufikia mahali hadi ya kuwasahau mawaziri wake mwenyewe. Waziri wake wa mambo ya nje anamwita Obama na muda mungine akikutana na Obama anamwita Clinton.

Juzi alikuwa katika mkutano wa G7 na viongozi wenzake. Wakati wakiwa wamesimama wakiangalia askari wa miamvuli wanavyoshuka kutoka juu, ghafla yeye (Biden) akawatoka wenzake na kuelekea upande ambao haueleweki. Baada ya mkewe kuona hali hiyo ikabidi amuwahi kwenda kumshtua kwamba huko unapoelekea ni kichakani (ni bustan yenye majani marefu mithili ya kichaka) akamuonesha walipo wenzake, ndo akarudi tena pale alipokuwa amesimama na kuendelea na sherehe yao.

Hiyo tisa, kumi na pale alipofanya kituko kingine katika ikulu ya white house. Wakati walipokuwa wanasherekea yeye na viongozi waandamizi wa ikulu, yeye akawa anatoa machoni mithili ya mtoto anaejaribu kufuatilia kitu asichokijua. Ghafla akataka kuwachomoka ili aelekee anapopajua yeye ndo watu wa karibu wakamtuliza, huku yeye akionesha wazi kusahau kinachofanyika pale 😂😂😂

Hizo picha 3 za juu ni za mkutano wa G7 jinsi alivyowatoka na jinsi mkewe alivyomrudisha katika kundi. Na hizo picha 2 za nchini na jinsi alivyotoa macho kuangalia asichokielewa na pia akitaka kuwatoka watu waliokuwepo katika sherehe hizo.

Nina imani kwa haya anayoyafanya Biden kama yangefanywa na raisi wa nchi yoyote ya Afrika, basi raisi huyo angeandamwa na vyombo vyote vya kimataifa. Ni kama alivyodhalilishwa raisi wa Sudan kwa kuambiwa kuwa kajikojolea hadharan nk.

View attachment 3019615View attachment 3019616View attachment 3019617View attachment 3019618View attachment 3019
 
Trump huwa anamtania sana Biden huwa nacheka kweli[emoji3]

Ila kiukweli naungana na wewe Biden apumzike kwa usalama wa afya yake I wish Blinken aingie mzigoni kwenye kuufukuzia Urais binafsi nafikiri anafaa kabisa kuwa Rais wa U.S
Kuna video Moja anamuigizia anayotoka jukwaaani then anazulula bila kujua anakwenda

Kisha anawaambia watu kwenye mkutano
"Yeye mwenyewe BIDEN akitoka jukwaaani ajui aelekee wapi anabaki kung'aang'aa macho ajielewi kama zombie(huku akimuigilizia anavyokosa direction akitembea kama zombie mikono akiwa ameiweka dizaini mazombie yanavyotembea sura kaibenjua)
Sasa unadhani mtu kama huyu anaweza kujua analipeleka wapi taifa letu"

Basi watu na waandishi wa habari wanacheka
Huwa nacheka kishenzi trump amiwa anamuigizia biden
 
Kama ni kweli kuwa anafanya hivyo kwa sababu za kisiasa basi atakuwa hajui kuwa anajiaibisha sana yey na nchi yake mpaka muda mungine unaona mkewe akihisi aibu machoni.

Mbona miaka ile ya obama hakuwa hivi au pale uzee na ugonjwa alionao sasa ulikuwa haujazidi?
Kadiri umri wake unavyoenda ndivyo hali hiyo inazidi pia, kujumlisha tatizo lake la kigugumizi.

Ila mbali na hilo, Joe Biden ni kati ya watu wenye akili sana na anajua kucheza na saikolojia ya watu, hususan kwa vile vyombo vya habari asilimia kubwa ya ripoti zao ni hasi dhidi yake.

Kuhusu kujiharibia taswira ya taifa, sidhani kama hicho kinaweza kuwa suala zito kwa sababu kwa mujibu wa tathmini ya afya yake, yuko imara kutekeleza majukumu yake.

Fuatilia intavyuu yake anayozungumzia tatizo lake la kigugumizi na jinsi alivyosaidiwa kitaalamu na daktari wake hadi akamudu kwa kiasi kikubwa.

Bottom line, Joe Biden ni msanii sana. Akili nyingi ndizo zinakuwaga hivyo. Laiti angeupata mapema urais alioutafuta muda mrefu sana, huenda angekuwa maarufu mno.

Baada ya kusema hayo, Wamarekani wajitahidi kumrudisha Trump madarakani mwaka huu ili dunia itulie kidogo kwenye amani ila ichangamke katika utendaji na uwajibikaji.
 
Us inaongozwa "Deep state" kule hata maiti inaweza kuongoza nchi ili mradi hiyo maiti iweze kusoma na kuongea kilichoandikwa na hiyo deep state...Iko siku USA itakuja kuongozwa AI technology na binadamu tusiligundue hilo, tatizo muda tu..
 
Kuna video Moja anamuigizia anayotoka jukwaaani then anazulula bila kujua anakwenda

Kisha anawaambia watu kwenye mkutano
Yeye mwenyewe BIDEN akitoka jukwaaani ajui aelekee wapi anabaki kung'aang'aa macho ajielewi(huku akimuigilizia anavyokosa direction)
Sasa unadhani mtu kama huyu anaweza kujua analipeleka wapi taifa letu

Basi watu na waandishi wa habari wanacheka
Huwa nacheka kishenzi trump amiwa anamuigizia biden
Biden amekuwa kama robot linaloongozwa na remote kufanya majukumu yake. Ni aibu kwa taifa lenye watu makini kama Marekani kuendelea kuongozwa na yeye.
 
Kadiri umri wake unavyoenda ndivyo hali hiyo inazidi pia, kujumlisha tatizo lake la kigugumizi.

Ila mbali na hilo, Joe Biden ni kati ya watu wenye akili sana na anajua kucheza na saikolojia ya watu, hususan kwa vile vyombo vya habari asilimia kubwa ya ripoti zao ni hasi dhidi yake.

Kuhusu kujiharibia taswira ya taifa, sidhani kama hicho kinaweza kuwa suala zito kwa sababu kwa mujibu wa tathmini ya afya yake, yuko imara kutekeleza majukumu yake.

Fuatilia intavyuu yake anayozungumzia tatizo lake la kigugumizi na jinsi alivyosaidiwa kitaalamu na daktari wake hadi akamudu kwa kiasi kikubwa.

Bottom line, Joe Biden ni msanii sana. Akili nyingi ndizo zinakuwaga hivyo. Laiti angeupata mapema urais alioutafuta muda mrefu sana, huenda angekuwa maarufu mno.

Baada ya kusema hayo, Wamarekani wajitahidi kumrudisha Trump madarakani mwaka huu ili dunia itulie kidogo kwenye amani ila ichangamke katika utendaji na uwajibikaji.
Mficha maradhi kifo humuumbua. Mtaendelea kusema kuwa Biden anaingiza ili ajipatie umaarufu kumbe mzee wa watu ndo anajiishia hivyo kimya kimya.
Ki ukweli kwa nchi kama Marekani haiitajiki raisi kuishi kama robot ili kujipatia umaarufu wa kisiasa. Nina imani kuwa Biden ni mgonjwa ila media za upande wake zinajaribu kuficha ukweli huu ili kulilindia heshima taifa isionekane kuwa wameruhusu robot litawale nchi.

Ongea yake, tembea yake na matendo yake vyote kwa pamoja vinaonesha clear kuwa yule mzee ana matatizo makubwa yanayofichwa fichwa na mamlaka yake.
 
Niaje waungwana,

Kusema ukweli kwa hali aliyofikia raisi wa Marekani mhe. Joe Biden, ni vizuri akashauriwa au akajishauri mwenyewe kuacha kugombea uraisi wa Marekani ili apate muda wa kwenda kupumzika nyumbani kwake na wajukuu zake. Ikiwa ataruhusiwa kuendelea kugombea na pengine akashinda, basi nitaamini kuwa Marekani ni nchi inayoweza kuongozwa hata na Chid Benz kikubwa tu awe mzawa na mwenye ushawishi.

Haiwezekani nchi yenye uchumi mkubwa, teknolojia kubwa na vyombo vyenye ueledi mkubwa wa kijeshi, kiuchumi, kielimu na kiintelejensia waongozwe na mtu ambae husahau jambo kila baada ya dakika 3 au 5 kupita. Inasemekana hufikia mahali hadi ya kuwasahau mawaziri wake mwenyewe. Waziri wake wa mambo ya nje anamwita Obama na muda mungine akikutana na Obama anamwita Clinton.

Juzi alikuwa katika mkutano wa G7 na viongozi wenzake. Wakati wakiwa wamesimama wakiangalia askari wa miamvuli wanavyoshuka kutoka juu, ghafla yeye (Biden) akawatoka wenzake na kuelekea upande ambao haueleweki. Baada ya mkewe kuona hali hiyo ikabidi amuwahi kwenda kumshtua kwamba huko unapoelekea ni kichakani (ni bustan yenye majani marefu mithili ya kichaka) akamuonesha walipo wenzake, ndo akarudi tena pale alipokuwa amesimama na kuendelea na sherehe yao.

Hiyo tisa, kumi na pale alipofanya kituko kingine katika ikulu ya white house. Wakati walipokuwa wanasherekea yeye na viongozi waandamizi wa ikulu, yeye akawa anatoa machoni mithili ya mtoto anaejaribu kufuatilia kitu asichokijua. Ghafla akataka kuwachomoka ili aelekee anapopajua yeye ndo watu wa karibu wakamtuliza, huku yeye akionesha wazi kusahau kinachofanyika pale 😂😂😂

Hizo picha 3 za juu ni za mkutano wa G7 jinsi alivyowatoka na jinsi mkewe alivyomrudisha katika kundi. Na hizo picha 2 za nchini na jinsi alivyotoa macho kuangalia asichokielewa na pia akitaka kuwatoka watu waliokuwepo katika sherehe hizo.

Nina imani kwa haya anayoyafanya Biden kama yangefanywa na raisi wa nchi yoyote ya Afrika, basi raisi huyo angeandamwa na vyombo vyote vya kimataifa. Ni kama alivyodhalilishwa raisi wa Sudan kwa kuambiwa kuwa kajikojolea hadharan nk.

View attachment 3019615View attachment 3019616View attachment 3019617View attachment 3019618View attachment 3019620
Daah kweli we maandazi! Unachukua Habari kutoka magazeti ya propaganda unaleta huku, hiyo picture hapo ilikuwa ni video na wameikata ili aonekane naongea mwenyewe ila alikuwa naongea na huyo komamdo aliyeshuka na parachute. Na huyo si mke wake
 
Back
Top Bottom