Tetesi: Rais Dkt Magufuli kufanya ziara nchini China

Tetesi: Rais Dkt Magufuli kufanya ziara nchini China

Rais wa China aivyochaguliwa tu akafanya ziara Tanzania... Na sisi Rais wetu ziara za nchi za mbali anaanzia China..!

Mhhhuuu...!Ila tu tunahitaji uwazi kwenye hicho kitakachojadiliwa.
Hivi Rais wa China huchaguliwaje? Maana sijawahi kusikia uchaguzi wa Rais ukifanywa.
 
Akishapewa shahada ya heshima ya kichina, basi tena, atakuwa fake kama bidhaa za kichina. Yale yale

Ni kweli hata daraja walilo tujengea Kigamboni ni fake, uwanja wa Taifa fake, ndege za kivita zinazo ruka kila siku nchini ni fake, mabom ya nuklia nchini mwao ni fake, roketi za kurusha wana anga in outer space ni fake, submarines na ICBMs zao zote ni fake - Watanzania bwana - tunaweza kweli kuwa na ubavu wa kuwabeza beza Wachina wakati sisi hata uwezo wa kutengeza sindano hatuna!!

Unaweza kudhalau Taifa ambalo ni la pili lenye Uchumi Mkubwa Duniani, baada ya miaka kumi na tano China itaipiku Marekani kiuchumi - sio vizuri kuleta dhalau zisizo na mantiki.
 
Kuna ukweli wa baadhi ya unayoyasema, ila umekwenda mbali sana na kuwa extremist. Nakukumbusha tuu urejee kukuwa kiviwanda na kiuchumi kwa China kumesababishwa na nini kama siyo FDI (Foreign Direct Investiment). Uchumi wa China hadi mwaka 1978 ulikuwa wa kudhibitiwa na serikali na ulikuwa ni mdogo kuliko uchumi wa Italy, na kitu kikubwa walichokuwa wana export ni gazeti la Guoz Shudian! Ni kwa kufika kwa Deng Xiaoping na kuufungulia uchumi kwa kuruhusu foreign investment ndipo uchumi ukaanza kukuwa hata kufikia 9.0 kwa miaka zaidi ya 20. Hakuna sababu nyingine yeyote isipokuwa foreign invcestment. Lakini FDI inataka pia kuwepo na discipline, nidhamu, ndiyo ifanikiwe. Wachina walifanikiwa kwa vile walikomesha rushwa kweli kweli, hivyo kila mwekezaji alikuwa anafuata sheria na kulipa kodi kama ipasavyo. Wakati huo huo, Wachina wenyewe wakawa wanatazama na kuiga yale yanayofanywa na wageni katika Nyanja zote. Nakumbuka kuna wakati Uchina ilinunua kiwanda kidogo cha pikipiki Italy mwaka 79-80. Wakapeleka mafundi wao wakakikongoa chote wakakihamishia China. Leo hii hakuna anayemshindwa Mchina kwa ku export pikipiki duniani! Hivyo ni makosa kusema uwekezaji wa kigeni hauna manufaa, bali ni sisi wenyewe ndiyo hatufuati masharti ya kufanya FDI ifaulu. Mtu anayechukuwa 10% na kuacha nchi iwe shamba la bibi...unategemea nini?
Ndiyo maana huu mwanzo wa magufuli unaweza kutupeleka mbali sana kama ukidumishwa kwa miaka mingine 20.

Uko sahihi, ingawa naomba nitahadharishe kuwa kuhusu masuala ya viwanda tayari China walikuwa na teknolojia yao ambayo hata hivyo ilikuwa duni. Kwa hiyo wao kuiga ilikuwa ni rahisi. Wachina walikuwa na uwezo wa kutengeneza jembe, bunduki, nguo, magari na hata ndege na kadhalika. Maana yake ni kuwa wachina walikuwa na base in Industrialization na ilikuwa rahisi wao kuchupa na kusonga mbele. Sisi hatuna hiyo base ya industrialization. Hatuna uwezo huo. Nyerere alijaribu kujenga uwezo huo lakini tukamuangusha. Nyerere alileta Mang'ula, Kilimanjaro Machine Tools, UFI, Urafiki, MUTEX na kadhalika na kadhalika kikiwemo hata kile kiwanda cha magari cha jeshi pale Kibaha. Mabeberu wakaja na liberalization policies wakaua kila kitu. Kulikuwa na viwanda pale Morogoro vingi sana lakini vyote vikafa. Katika miaka ya 1970 na 1980 kule Mlimani (UDSM) wasomi wa uchumi walikuwa wanazungumzia kitu kinaitwa BIS (Basic Industrial Stategey) kuwa ndio kitovu cha uchumi. BIS ndio hiyo iliyozaa Mang'ula na kadhalika.

Kwa hakika kabisa kwetu sisi tuliopiga umande kidogo na ambao angalau tunafahamu stage tuliyokuwa tumefikia wakati wa Mwalimu Nyerere na hasa nia yake nzuri ya kuendeleza nchi hii mtu unaweza kutoa machozi kwa kuangalia namna tulivyorudi nyuma. Hatuwezi kutengeneza hata pini. Viwanda vyote vilivyopo inaonekana ni vya mabeberu wa nje. Hata kiwanda cha BIA ambacho kilikuwa ni chetu nacho tumewauzia Makaburu. Bia ya safari ilibuniwa na Mtanzania lakini sina hakika kama kweli bado tuna haki milki ya bia hiyo.

China iliweza kupiga hatua kwa muda mfupi kwa kuwa iliamua kuchukua hatua madhubuti. Liberalization yao ilikuwa ni kwenye uchumi kwa lengo la ku-transfer teknolojia kutoka nje kuboresha teknolojia yao. Wao walikuwa makini sisi hatukuwa makini. Wachina hawakutaka kabisa kufanya liberalization ya siasa kwa kuogopa vurugu. Chama chao cha Kikomunisti kiliendelea kuwa madarakani na mpaka leo kipo madarakani na ndicho kinachoongoza mabadiliko au mageuzi. Sisi tulikimbilia zaidi kwenye mageuzi ya kisiasa kwa kuleta mfumo wa vyama vingi vya siasa tukidhani kuwa mageuzi hayo ndiyo yatakayochochea maendeleo. Kinachotokea sasa ni kuwa ni kweli tunao mfumo wa vyama vingi vya siasa lakini pamoja na hayoni vurugu tupu. Watu kazi yao kuimba mabadiliko na kutaka maandamano mitaani. Hakuna nidhamu. Wapinzani wapo kupinga kila kitu cha CCM, na CCM nao wako tayari kufanya lolote mradi wabaki madarakani . Kwa hiyo kilichoko nchini kwa sasa ni vurugu na ukosefu wa nidhamu katika jamii.
 
Serikali makini na Rais makini ,hapa ni kazi tu na alishasema anataka viwanda na viwanda dunia nzima wanaangalia.China

Lakini wachina ni wagumu sana kusaidia kwenye sekta za viwanda, tangu utawala wa JK pamoja na ukaribu wake na Wachina waliwahi kujenga kiwanda gani cha naana nchini - hakuna kabisa, leo hii ndio tuwamini kwa misingi gani - binafsi sina imani na watu hawa ingekuwa enzi za utawala wa Mao kweli, we'll be better off tukishirikiana na Wavietnam kuliko Wachina nawambieni.
 
akatazame fursa za kilimo na miundo mbinu na viwanda ,akubali jamaa watusaidia katika hilo,lakini amwambie rais wao kuwa wachina wanafanya kazi za kipuuzi sana nchini kwetu ,na wamekuwa wanaongoza kwa kazi za magendo hapa kwetu amfikishie rais wao wajue kabisa
 
Kwa mujibu wa duru muhim ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje, Mheshimiwa Rais anatarajiwa kufanya ziara rasmi nchini China baadae mwezi huu.

Katika ziara hiyo Pamoja na matukio mengine Mhe Raisi atashiriki mazungumzo na kusaini makubaliano mbalimbali juu ushirikiano wa China na Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Kadhalika Mheshimiwa atatunukiwa Shahada ya juu ya heshma toka chuo kikuu kimojawapo mashuhuri Jijini Beijing.
mikataba tena[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji15] !!!
kwani aliyosaini kikwete haikutosha???

Chinese Nunua Tanzania is Loading........
 
China? Give me a break. Hawa hawawezi kuwa washirika wa maendeleo. Wanatafuta kuchuma zaidi kutoka kwetu kuliko sisi kupata kutoka kwao.
 
We have to be strategically naive.. China hakuna kitu, labda kama tunataka kuendeleza urafiki wa vyama.
 
Hawa wachina si Rais apitie ile mikataba 17 walioisaini ya gesi wkti wa serikali ya jk. Sasa haraka haraka za nini kusafiri kwenda huko wakati nchi ina figisu figisu za kutosha. Yeye akae adili na kina lugumi etc. Si alisema wananchi wamsaidie kutumbua majipu, hayo sasa humu jamii forum.
 
Yeye Mheshimiwa tayari alisha jitolea kuwahudumia watanzania ili tusiendelee kuwa maskini. Apitie ile mikataba ya China atuambie ina maslahi au haina maslahi, ndo aende China. Otherwise, itakuwa ngumu sana kutuaminisha anavyoaminisha wananchi. Tofauti na hapo, nitaendelea kusema CCM ni ile ile
 
Back
Top Bottom