Rais Dkt. Mwinyi amteua Maalim Seif kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Rais Dkt. Mwinyi amteua Maalim Seif kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar

Ama kweli unafiki ni KIPAJI. ACT Wazalendo mmekusanya ushahidi na kupeleka katika taasisi za Kimataifa ICC, UNHRC na kwingineko kuwashtaki madhalimu wa maccm. Hata kabla hamjajibiwa MMEKURUPUKA kudandia madaraka! Chama cha wasaliti na waroho wa madaraka. Haya sasa jipongezeni kwa usaliti wenu. Zitto
Zitto kamaliza kazi yake anaingia bungeni kama mbunge wa kuteuliwa na Rais.
 
aloo! ya wana siasa waachieni wanasiasa, watu walikufa kisa wanasiasa na siasa, leo hii ndo haooo wameungana kula bata kwa pamoja, nadhani siku zingine hakuna atakae kubali kufa au kudhurika kisa mwana siasa au siasa, bila shaka hili ni fundisho na litakuwa ni fundisho tosha kwa watu wote.
Kuna wale masikio ya kufa hayasikii dawa.
 
Sasa kama mlikuwa hamataki kuteseka, kwanini kuwasumbua ccm wakati wanawapa raha?
Kwani sheikh kama wewe uko jela utagoma kula au utajinyonga? Au utapokea chakula na kuvuta muda mbele?
 
Lazima tutazame priority ziko wapi, kwa sasa kugoma au kuandamana haina tija yoyote. Ni kheri kuelekeza nguvu za wazanzibari kwenye umoja na kusonga mbele ivo ivo hata kama wengine wamekatika miguu au kupoteza maisha.

Sioni ulazima wa watu wetu kuteseka kwa miaka 5 bila ya sababu za msingi. Kwa mtazamo wangu mfupi naona kujiunga kunaleta uwezekeno wa kuja na suluhusho za kidiplomasia. The best would be mapanga ya 72, lakini kwa bahati mbaya hayapo.
 
Wawili hawa nawajua vyema sana. Mmoja ni kaka yangu na mmoja ni kama mtoto wangu. Maalim Seif Sharrif Hamad nilimkuta UDSM. Akaniacha miaka kadhaa pale yeye akimaliza mapema. Maalim, kama ilivyokuwa kwangu na kwa Zitto, alikula shavu la kiserikali mara tu baada ya kumaliza Chuo Kikuu. Taratibu tamu kama zabibu zilikamilishwa wakati wa masomo yetu. Na si sisi tu, wengi tu nawajua na wamepita njia hizo.

Kuanzia hapo kwenye kula shavu la kiserikali, Maalim Seif na Zitto hawakuwahi na hawatakuwa wapinzani. Hawana tofauti yoyote na mtani wangu Benard Membe. Kila walifanyalo kwenye maigizo na mwamvuli wa upinzani ni ubatili mtupu. Hivi hamzioni tofauti zao na wengineo? Maalim Seif alikuwa Waziri Kiongozi kule Visiwani na Makamu wa Pili wa Rais. Amerejea tena kwenye Umakamu. Kwanini yeye tu? Yeye ni mtiifu kwa mfumo.

Mnajua kwanini Zitto, pamoja na kutishia na kutangaza mara kwa mara akiwa CHADEMA, hagombei Urais? Hataki kujiharibia. Hataki kugombana na wazazi na walezi wake. Ndiyo maana anajiweka mbali na Urais na kuzuga kama vile anamuunga mkono mgombea mwingine wa upinzani. Nchi ina mambo sana hii. Kitendo cha Zitto na Maalim Seif kukubali kuingia kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa kule Zanzibar, kwangu mimi, hakinishangazi. Nawajua nje ndani hawakuwahi kuwa wapinzani.

Mwaka 2020 hakukuwa na uchaguzi, kulikuwa na uchafuzi!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
1607335439381.jpeg
 
Kwa hiyo Maalim yuko jela? Huu mfano ni irrelevant.
Tuko kwenye ukoloni mweusi wa Tanganyika ambao sioni tofuati na kuwa jela, naona mzee akili yako imechoka kufikiri au?
 
Bora kama umejifunza hilo,vijana wengi mishipa huwa inawavimba humu bila sababu ya msingi......wanapiga miayo wakati wanaowapigania wanakula keki ya taifa....
Wanasiasa nimewavulia kofia leo! Siku nyingine mkipigana siamulii. Nitakamata jembe na kuelekea shambani. Ningefanya hili wakati wa kampeni, leo hii labda ningekuwa navuna.
 
Tuko kwenye ukoloni mweusi wa Tanganyika ambao sioni tofuati na kuwa jela, naona mzee akili yako imechoka kufikiri au ?

Duuu, huo mstari wako wa mwisho nilijua ndio itakuwa hitimisho lako. Kazi kweli kweli.
 
Pongezi kwa CCM kwa ukomavu wa kisiasa, hongera ACT kwa kukubali kwamba maendeleo hayana chama.

Tuliwaasa sana ndugu zetu kwamba hakuna upinzani Tanzania ila kuna wachumia tumbo na vibaraka wakatukatalia, ila nadhani sasa wataelewa.

Mungu ibariki Tanzania
NILIWAHIBKUSEMA VIJANA WA UPINZANI WENGI NI MBOGA SABA WAMEVIMBIWA MAPIZZA NA MABUGGER 🤣😂🤣😂🤣😂😂😂😂😂 HALAFU WANAKAA. KWENYE KIBORD WANADAI DEMOCRACY HAHAH HAYA SASA SEIF RAIS HUKO MDEEE MBUNGE HUKO SWALII ......HIYO ICC INANAHUKUMU NANI NA NINI

ASANTE SANA CCM TUPIGE KAZI UPINZANI UPO ASILIMIA 2% TENA MTANDAON
 
Back
Top Bottom