Rais Hussein Mwinyi kuongea na Serikali ya Muungano ili Zanzibar ianzishe mfuko wa kusaidia Waislam

Rais Hussein Mwinyi kuongea na Serikali ya Muungano ili Zanzibar ianzishe mfuko wa kusaidia Waislam

Nimemsikia Rais wa Zanzibar akieleza kwamba eti waombe kibali Serikali ya Muungano ili Zanzibar ianzishe mfuko wa kusaidia waislam wanapoenda Hija.

Nimeshtushwa na hili ombi kwani Zanzibar inazuiwa kujianzishia mfuko? Au ni kanjia ka kuitaka Serikali ya Muungano igharamie ibada ya dini moja?
Umestushwa nini? Kwenda Hijja ni imani yao hata Wakristo huenda Yerusalem na Fatima na Nnamugongo, Wahindu huenda Veranasi kujiua mtoni waende mbinguni. Kwa nini mtu umzuie kuanzisha mfuko kusaidia watu kuhiji? La muhimu ni utaratibu tu, Mfuko utumiwe na Mahujaji na si magaidi wa UAMSHO wala wanaharakati. Ukiwa chini ya Mufti au Baraza la Waislamu wazalendo likatoa Taarifa ya Mapato na Matumizi kama NGO zingine sioni kama kuna shida yoyote.
 
Huyu Mwinyi ndiyo watu wanawaza awe rais wa Tanzania baada ya Samia
 
Umestushwa nini? Kwenda Hijja ni imani yao hata Wakristo huenda Yerusalem na Fatima na Nnamugongo, Wahindu huenda Veranasi kujiua mtoni waende mbinguni. Kwa nini mtu umzuie kuanzisha mfuko kusaidia watu kuhiji? La muhimu ni utaratibu tu, Mfuko utumiwe na Mahujaji na si magaidi wa UAMSHO wala wanaharakati. Ukiwa chini ya Mufti au Baraza la Waislamu wazalendo likatoa Taarifa ya Mapato na Matumizi kama NGO zingine sioni kama kuna shida yoyote.
Mbona umeleta mambo ya uamsho na ugaidi ,kumbe unao ushahidi wa ugaidi wao kwa nini hukuwasaidia polisi na kesi ya kubambikiza ya kuwaonea wanaotetea haki Za Wazanzibari?
 
Nimemsikia Rais wa Zanzibar akieleza kwamba eti waombe kibali Serikali ya Muungano ili Zanzibar ianzishe mfuko wa kusaidia waislam wanapoenda Hija.

Nimeshtushwa na hili ombi kwani Zanzibar inazuiwa kujianzishia mfuko? Au ni kanjia ka kuitaka Serikali ya Muungano igharamie ibada ya dini moja?
Huyo nae Eti ana ndoto za kuwa Rais bara. Apotelee huko huko😠😠😠
 
Huyo nae Eti ana ndoto za kuwa Rais bara. Apotelee huko huko😠😠😠
Huyo ni kijana wenu kutoka Mkuranga . Huku aliletwa na Magufuli kuendeleza ukoloni wa Tanganyika kwa Zanzibar na waliuliwa watu katika kuwekwa hapo.
 
Huyo nae Eti ana ndoto za kuwa Rais bara. Apotelee huko huko😠😠😠
sheria Za uchaguzi Za Zanzibar na Tanganyika/ Tanzania , hazikumruhusu kugombea Uraisi Zanzibar, ni ubabe wa Magufuli na baraka Za baba yake , ndiyo zilizomweka huku sheria zikivunjwa mchana kweupe
 
sheria Za uchaguzi Za Zanzibar na Tanganyika/ Tanzania , hazikumruhusu kugombea Uraisi Zanzibar, ni ubabe wa Magufuli na baraka Za baba yake , ndiyo zilizomweka huku sheria zikivunjwa mchana kweupe
Baba yake aliwahi kuwa pia Rais wa huko. Serikali 3 zingefaa sana .

Wacha tupambanie KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA.
 
Back
Top Bottom