Rais Kenyatta aruhusu Watanzania kuanza kufanya kazi na biashara Kenya bila kuwa na Work Permit wala Business visa

Rais Kenyatta aruhusu Watanzania kuanza kufanya kazi na biashara Kenya bila kuwa na Work Permit wala Business visa

Mengine magu alikua sahihi kuwanyoosha wakenya,unajua mpaka leo ndege zetu azijaruhusiwa kwenda kenya sababu kenya inahofia italeta ushindani,usidhani kama crdb haiwezi kufungua matawi kenya lkn ni vikwazo vya kikenya,rostam yuko sahihi sana
Mkuu acha kupotosha. Kenya haijazuia ndege za tanzania... ATCL ndii haijaomba kibali cha kwenda kenya
 
Huu uwoga na tumeaminishwa na wana siasa kuwaogopa wa Kenya na unyonge ndio shida kubwa, tunawaogopa nini hasa mbona tumejaza wahindi makampuni yote na kila siku wanaingia tu. Ajira ni ushindani na ufanisi ndio inabidi tujiongeze tuwe waadilifu ili sisi ndio tuwe na thamani kwao siku waombe wa Tanzania katika makampuni yao. Tabia ya kuaminishwa kuwaogopa wa Kenya hata sijui nani aliyeileta, Mimi simuogopi mkenya kwa lipi zaidi? tuache unyonge
Sio unyonge ni utaratibu..kwani hao wachina na wqhindi wanakuja kwa utaratibu au matamko?
 
Kigelegele kwa Kenyatta aruhusu watanzania kuanzia sasa ruksa kufanya kazi na biashara kenya bila kuwa na work permit wala Business visa

Kasema mida hii mkutano wa wafanya biashara

Kuruhusu ilikua lazima sababu

Kwa issue ya ajira kwani zipo basi? Anajitaftia tuu umaarufu....

Na upande wa biashara ni nafuu kwake sababu anahitaji sana mazao toka huku
 
Wakenya wajanja, hata kama huna work permit, wala business visa, kazi hupati Kenya.. Mtanzania hawezi pewa nafasi na wakenya kufanya kazi.. Sisi tusiruhusu hilo, eti wakenya waje free huku, hilo litakuwa kosa kubwa sana kutokea
Kosa gani? Uchumi wa sasa ni kufungua mipaka na kuondoa vikwazo vya biashara na ajira. Kwanza mipaka ni kizuizi cha kisaikolojia tu. Mmasai wa Arusha anamuona mmakonde ni ndugu yake wa karibu kuliko mmasai wa Kenya!!!. Mmakonde naye hivyohivyo, anamuona mmasai wa Arusha ni ndugu yake kuliko mmakonde wa Msumbiji!!!. Tufunguke, kanuni ya Comparative advantage ifanye kazi, tuwauzie mahindi na maharage nao walete hizo bidhaa wanazotengeneza.
 
Kwa nini CRDB isiiue Equity?
That's very good question.

Inawabidi CRDB wafanye hivyo kwa mbinu za kiaina za kibiashara. Mimi Sina uhakika kama Our intelligence is doing somethings on helping us katika maswala ya kiuchumi so if Kenyans does ndio tunapigwa kama hivi

📌Wala mtu asije akam'twisha Mzigo kamanda Magufuli katika hili. He is unfit to be blamed
 
Mkuu unachekelea na yeye mama atafanya the some....uone ajira zote zitachukuliwa na wakenya Hadi uwalimu.....kwasababu wako smart na agressive....time will tell utakujaa kulala Mika hapa tenaa
Mbona hata sasa wakenya hawapo lakini ajira hakuna? Kwanza unaweza shangaa sisi ambao ni cheap tukapata ajira zaidi Kenya.
 
Hapa tumetupiwa ndoano, tukiingia tumenasa na mwisho wake ni mgogoro mkubwa sana...

Labor force ya Tanzania ni unskilled, Kenya wanalabor force kubwa skilled hapa tumeumia.
Makampuni mengi ya kimataifa, kienglish aka kiingereza aka kikristo ndio priority kwenye kutoa ajira, hapa wabongo tutapigwa maana wengi wasomi kiingereza cha kuunga unga...
Kwahiyo dawa ni kujifungia na ufukara wetu? Hii victim mentality ya unyonge tuliyojazwa na viongozi wetu inaghafilisha sana.

Kwanini tusiruhusu ushindani uje..hata kama tukipigika kwa muda mfupi..itatulazimisha kuongeza standards zetu. Labour force yetu itakua skilled kwa haraka ili kushindana na hao wenzetu. Competition always inaongeza viwango vya ubora!
 
Kasema in Public then in Private anawaambia wakazieni hao...[emoji1787][emoji1787]
 
That's very good question.

Inawabidi CRDB wafanye hivyo kwa mbinu za kiaina za kibiashara. Mimi Sina uhakika kama Our intelligence is doing somethings on helping us katika maswala ya kiuchumi so if Kenyans does ndio tunapigwa kama hivi

📌Wala mtu asije akam'twisha Mzigo kamanda Magufuli katika hili. He is unfit to be blamed
Hilo hata mimi sidhani, sidhani kama wana kitengo cha maswala ya uchumi, na kam kipo basi hakielewi kitu.
 
Piga kelele kwa Kenyatta akee[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]

Seriously, EA hatutakiwi kuwa na barrier zozote za kibiashara. Tuna custom union ya maneno tu lakini haifanyi kazi. Tunazuia na kubania biashara za Kenya huku tukijaza masoko kwa bidhaa za India na China. EA inatakiwa kufunguka, iwe kama nchi moja. Hapo ndiyo tunaweza fikia shirikisho la kisiasa
Ila sio kwenye maziwa tutakwama

Sent from my vivo 1915 using JamiiForums mobile app
 
kenyatta anajua ni watz wachache mno wanaenda kufanya kazi kule, wakafanye kazi gani? kwa maisha haya ya hapa tena uende kufanya kazi kenya? hata wao wanakuja hapa kufundisha kiingereza na biashara labda. hata sisi tufanye hivyo, though visa iwe lazima.
 
Mtego huu, anataka na Samia aseme hivyohivyo kwa wakenya
Hakuna mtego wowote hapo, na Rais Samia hana sababu ya kuruhusu wakenya Tanzania kwa sababu mbili ingawa ziko nyingi zaidi. Bidhaa za Kenya ni nyingi kwetu kuliko zetu kwao.

Pili Shirika la ndege la Kenya ndilo pekee linatoa huduma Kati ya Dar na Nairobi, Air Tanzania haijawa na ruhusa hiyo.

Makampuni ya Tanzania kuorodheshwa kwenye soko la Nairobi NSE masharti ni magumu ukilinganisha na Makampuni ya Kenya kwenye soko letu DSE. Mambo ni mengi yanayotakiwa kunyooshwa. Ila kwenye makubaliano yoyote na wakenya tunatakiwa kuangalia kila neno kwa herufi na alama zinazotumika.
 
Kwahiyo dawa ni kujifungia na ufukara wetu? Hii victim mentality ya unyonge tuliyojazwa na viongozi wetu inaghafilisha sana.

Kwanini tusiruhusu ushindani uje..hata kama tukipigika kwa muda mfupi..itatulazimisha kuongeza standards zetu. Labour force yetu itakua skilled kwa haraka ili kushindana na hao wenzetu. Competition always inaongeza viwango vya ubora!

tuanze kuwaandaa watu wetu kuwa washindani kwanza ndio tuingie kwenye contract za namna hii otherwise tutakuwa tumejipiga kitanzi...

tukitegemea wao waje ndio watu wetu wacatch up, tumeliwa jamaa yangu, kifupi watu wetu watakuwa utumwani kwa miaka mingi na kujinasua itakuwa ni machafuko labda...the more you advance the more they will advance..
 
kenyatta anajua ni watz wachache mno wanaenda kufanya kazi kule, wakafanye kazi gani? kwa maisha haya ya hapa tena uende kufanya kazi kenya? hata wao wanakuja hapa kufundisha kiingereza na biashara labda. hata sisi tufanye hivyo, though visa iwe lazima.
Tuna mtihani mkubwa wa kujinasua na hii mentality ya unyonge tuliyojazwa na wanasiasa wetu. Yaani badala ya kuchangamkia opportunity na kuangalia fursa zilizopo kenya... automatically una conclude kwamba hamna kitu unachoweza kufanya kule na wao wana advantage huku? Naililia sana nchi yangu kwa hii mental slavery tuliyonayo
 
Back
Top Bottom