Rais Kikwete amteua Alan Kijazi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA)

Rais Kikwete amteua Alan Kijazi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA)

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,801
Friday, May 27, 2011


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
TAARIFA KWA UMMA
UTEUZI WA MKURUGENZI MKUU WA TANAPA


Rais Jakaya Kikwete

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Alan Kijazi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa (TANAPA).

Bwana Kijazi anachukua nafasi ya Bwana Gerald Bigurube ambaye alistaafu kwa hiari.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Kijazi alikuwa mfanyakazi wa TANAPA kama Mkurugenzi wa Mipango, Miradi ya Maendeleo na Huduma za Utalii.

Bwana Kijazi alisoma katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Norway na kuhitimu Shahada ya Uzamili katika fani ya Uendelezaji wa Maliasili (MSc. Management of Natural Resources). Awali Bwana Kijazi alipata elimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo alihitimu Shahada ya Mipango ya Mazingira (BA. Environmental Planning).

Kabla ya kujiunga na TANAPA Bw. Kijazi alifanya kazi katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, mwaka 1998 hadi 1999. Pia alikuwa Meneja wa Mradi wa Kuendeleza Uhifadhi wa Wanyamapori (African Wildlife Foundation), mwaka 1999 hadi 2003.

Uteuzi huo unaanza mara moja.
 
hongera xana kijazi lakn chunga sana kama we ni fisadi
 
Mkurugenzi mkuu mwenyewe ndio huyu kwenye picha, au?

H+E+Jakaya+Mrisho+Kikwete+Presidential+Image+A.jpg


Hakuna hata ki profile cha uongo na kweli kueleza professional achievements zake zilizoshawishi watu wamteue, yani Juma na Roza yoyote anaweza kuteuliwa chochote Bongo
 
Kazi yako ya kwanza tunataka ukweli wa utoroshaji wa wanyama hai kutoka hifadhini kwenda uarabuni kupitia KIA. Wewe huko sio mgeni, na kwa vyovyote unalijua hili vizuri, ukishindwa kushughulikia hili jitoe mapema aje anayeweza.

Mwinjuma aliimba "mkulima kala mbegu" na " ukipanda bangi utavuna bangi sio mchicha" kwa hiyo hatuwezi hata kidogo kuwaacha hawa watu wachache wale mbegu zetu tukose mbegu za kupanda. Kuiba wanyama hai kuwapeleka nje maana yake ni kuzuia watalii wasije nchini, maana watakuwa wanawaonea wanyama hao hukohuko kwao, huo ni uhujumu mkubwa wa uchumi wa nchi kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho. Tunataka ukweli kuhusu hilo, ukishindwa achia ngazi, kwa maana inawezekana nawe umo kwenye mtandao huo wa wizi wa wanyama wetu hai, kwa kuwa ule wizi uliotokea ni mtandao, ambao ni mrefu na tanapa ni lazima wawe sehemu ya mtandao huo, kama wewe haumo wenzako wamo.

Chukua hatua haraka.
 
Bwana Kijazi alisoma katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Norway na kuhitimu Shahada ya Uzamili katika fani ya Uendelezaji wa Maliasili (MSc. Management of Natural Resources).

Hivi management = na uendeshaji au ni usimamizi???? hii kurugenzi ya habari ya rais ina matatizo sana ya uelewa wa mambo..
 
Tena mbona huyu hamuulizi iwapo ana uwezo wa kufanya hili au lile kama mlivyouliza kwa yule Internal Auditor?

Wengine udini mnauweka mbele sana Wakuu.
 
Kazi yako ya kwanza tunataka ukweli wa utoroshaji wa wanyama hai kutoka hifadhini kwenda uarabuni kupitia KIA. Wewe huko sio mgeni, na kwa vyovyote unalijua hili vizuri, ukishindwa kushughulikia hili jitoe mapema aje anayeweza. Mwinyijuma aliimba "mkulima kala mbegu" na " ukipanda bangi utavuna bangi sio mchicha" kwa hiyo hatuwezi hata kidogo kuwaacha hawa watu wachache wale mbegu zetu tukose mbegu za kupanda. Kuiba wanyama hai kuwapeleka nje maana yake ni kuzuia watalii wasije nchini, maana watakuwa wanawaonea wanyama hao hukohuko kwao, huo ni uhujumu mkubwa wa uchumi wa nchi kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho. Tunataka ukweli kuhusu hilo, ukishindwa achia ngazi, kwa maana inawezekana nawe umo kwenye mtandao huo wa wizi wa wanyama wetu hai, kwa kuwa ule wizi uliotokea ni mtandao, ambao ni mrefu na tanapa ni lazima wawe sehemu ya mtandao huo, kama wewe haumo wenzako wamo. Chukua hatua haraka.

Hapo kwenye Blue mkuu, hakuna kitu kama hicho chini ya Serikali ya CCM, lasivyo utang'olewa/shughulikiwa.
 
Sasa naona bora kazi ya uteuzi ifanywe na JF, maana kila anaemteua Rais wanasema ni wale wale tu hakuna jipya.
 
Tena mbona huyu hamuulizi iwapo ana uwezo wa kufanya hili au lile kama mlivyouliza kwa yule Internal Auditor?

Wengine udini mnauweka mbele sana Wakuu.

Wewe kwanini usiulize unataka waulize wengine?! Muulize aliyemteua ndo anajua uwezo wake, halafu una akili finyu sana unawaza udini hata pasipostahili na ujifunze kuwa na subira maana watu wanaendelea kuchangia hoja labda anaweza kutokea mtu mwenye hoja unayotaka!
 
Tena mbona huyu hamuulizi iwapo ana uwezo wa kufanya hili au lile kama mlivyouliza kwa yule Internal Auditor?

Wengine udini mnauweka mbele sana Wakuu.

Maswala ya dini ni wewe na Mungu wako basi hapa tunajadili mambo kwa maslahi ya nchi yetu Tanzania.
Elewa matatizo yanayolikabili taifa letu yanatuathili kwa ujumla wetu bila kujali dini kabila wala itikadi za kisiasa.
Nawashangaa waTanzania wanaochukulia taifa letu kwa misingi ya dini mbili nakusahau kwamba kuna waTanzania wengi ambao hawafungamani na dini za kigeni inakera zaidi inapodhihirika kwamba hata hao mavuvúzela wa dini za kigeni wengi wao ni waumini majina tu au wachumia tumbo maana matendo yao ni kinyume kabisa na mahubili yao.
Haohao wanaolialia oooh kateuliwa mkristo au mwislamu baadae wakienda pembeni wananongonezana sawa ni mkristo au ni mwislamu mwenzetu lakini sio wa dhehebu letu.
Hiyo ni dhana potofu ya ubaguzi ambayo inaendelea kutafuna taifa hili hata baada ya miaka arobaini ya uhuru.
Tanzania ni yetu sote wenye dini za kigeni na wale wasiokuwa na dini yeyote ile.
 
hongera kijazi angalau tanapa imepata kiongozi mahiri hana urasimu yuko karibu na watu kwa kweli uteuzi huu wa mkuu wa kaya umekaa vizuri , Kijazi kumuona haitaji kutumia mwezi au wiki km mtangulizi wake ila idara mbalimbali hasa prm amepata pigo
 
Hongera sana mate kwakuteuliwa, tafadhali usiiangushe taaluma yetu ya interdisciplinary; you were trained to solve problems comprehensively naona humu wameshaanza kukuchakachua kwakukosea hata jina la MSc yako!

Må Gud lede og dirigere hvert skritt i denne nye stillingen, Fred være med dere!
 
Tena mbona huyu hamuulizi iwapo ana uwezo wa kufanya hili au lile kama mlivyouliza kwa yule Internal Auditor?

Wengine udini mnauweka mbele sana Wakuu.

Kama wewe maana inaonekana umeangalia dini yake kwanza kabla ya ku-comment
 
Back
Top Bottom