Rais Kikwete kuwasili Houston na msafara wa kitajiri Oktoba 3

Rais Kikwete kuwasili Houston na msafara wa kitajiri Oktoba 3

Kumbe muheshimiwa hakwenda...au alikuwa anawahi Mwanza kwenye maadhimisho ya miaka 100???
Mwanzage,
Mheshimiwa hakuenda Houston. Alikimbilia Arusha. Nways, nimerudi tu kutoka Houston na nitakuwa na mengi ya kusema baada ya kupumzika. Watanzania tusiwe negative mno.
 
Mwanzage,
Mheshimiwa hakuenda Houston. Alikimbilia Arusha. Nways, nimerudi tu kutoka Houston na nitakuwa na mengi ya kusema baada ya kupumzika. Watanzania tusiwe negative mno.

....haya bana tunasubiri kwa hamu kukusoma hayo uliyokutana nayo......
 
....haya bana tunasubiri kwa hamu kukusoma hayo uliyokutana nayo......
Ogah,
Ahadi ni deni. Nimerudi kutoa tathmini yangu kuhusu mkutano wa Houston.
Mimi nilikwenda kama mtazamaji (observer), unajua tena kwa jina kama langu sipendi kupitwa na kitu. Mgeni mwalikwa alikuwa rais Kikwete na nasikia mkutano uliahirishwa kutoka April hadi Oktoba ili kum-accomodate na kwa mujibu wa ombi lake. Kwa hiyo tulishangaa tulipoarifiwa kuwa ameamua kurudi nyumbani mapema kufungua mkutano wa bunge la Commonwealth Arusha. Baadhi tukajiuliza ni nani anayemtayarishia rais ratiba yake? Eniwei hayo yakawa beside the point.
DICOTA ni kundi la Watanzania wa fani mbalimbali waliojikusanya ili kuweza kuchangia na kushiriki katika uwekezaji na biashara nyumbani. Alihutubia Bernard Membe, waziri wa mambo ya nje akimwakilisha rais na pia kulikuwa na viongozi mbalimbali wa serikali ya Tanzania na idara zake kama vile Emmanuel Ole Naiko wa TIC, mwakilishi wa CRDB, Naibu gavana wa BOT, mfanyibiashara maarufu Elvis Musiba na Felix Mosha wa NICO. Wote walihimiza umuhimu wa Watanzania walioko diaspora kuwekeza nyumbani. Siyo lazima uwe na mtaji mkubwa lakini kama kuna Watanzania 10 na kila mmoja akichanga dola elfu moja tayari mnazo elfu kumi ambazo zinaweza kuwekezwa Bongo.
Mbali na uwekezaji na biashara, yalijadiliwa pia masuala ya dual citizenship, ambapo Membe aliwahakikishia wadau kuwa bado linashughulikiwa na yeye anaunga mkono kabisa kutolewa kwa duo citizenship kwa sababu, kama alivyosema, serikali inatambua mchango wa raia wake waliozamia nchi za nje kwa sababu kedha wa kadhaa, na wakati huo huo, kama wamechukua uraia wa nchi nyingine za kimaslahi basi wananyang'wanywa uraia wa Bongo. Hiyo aliiita kuwa ni "contradiction" ambayo serikali inapaswa kuishughulikia na wanalishughulikia. Suala la urasimu ambapo mtu anayetaka kuanzisha kampuni inamchukua hadi miezi sita kukamilisha taratibu pia lilijadiliwa. Suala la madini likagusiwa na inaonekana viongozi serikalini wanatambua kasoro zilizopo katika mikataba. Lakini tuliondoka bila kuhakikishiwa ni hatua gani zinachukuliwa kuondoa kasoro hizo. Niliondoka nikiamini kuwa serikali imepania kuwashirikisha na kuwasaidia raia wa Tanzania walioko nje wanaotaka kuwekeza nyumbani kwa kuondoa adha na kero wanazokumbana nazo wakati wanapotaka kuwekeza nyumbani. Tusubiri tuone kama zilikuwa ahadi hewa au la. Kama nilivyosema, nilienda Houston kama mtazamaji, lakini nimeondoka nikivutiwa na wazo na malengo ya DICOTA. Natumaini wata- update website yao ili sote tuweze kujionea kile wanachojaribu kufanikisha.
 
Hakika nchi itakuwa mufilisi kabisa,na ataondoka lini huyu sindbad?
 
Whoever wrote the heading is clearly biased in every way making anyone who believes this nonsense an imbecile..
 
Ogah,
Ahadi ni deni. Nimerudi kutoa tathmini yangu kuhusu mkutano wa Houston.
Mimi nilikwenda kama mtazamaji (observer), unajua tena kwa jina kama langu sipendi kupitwa na kitu. Mgeni mwalikwa alikuwa rais Kikwete na nasikia mkutano uliahirishwa kutoka April hadi Oktoba ili kum-accomodate na kwa mujibu wa ombi lake. Kwa hiyo tulishangaa tulipoarifiwa kuwa ameamua kurudi nyumbani mapema kufungua mkutano wa bunge la Commonwealth Arusha. Baadhi tukajiuliza ni nani anayemtayarishia rais ratiba yake? Eniwei hayo yakawa beside the point.
DICOTA ni kundi la Watanzania wa fani mbalimbali waliojikusanya ili kuweza kuchangia na kushiriki katika uwekezaji na biashara nyumbani. Alihutubia Bernard Membe, waziri wa mambo ya nje akimwakilisha rais na pia kulikuwa na viongozi mbalimbali wa serikali ya Tanzania na idara zake kama vile Emmanuel Ole Naiko wa TIC, mwakilishi wa CRDB, Naibu gavana wa BOT, mfanyibiashara maarufu Elvis Musiba na Felix Mosha wa NICO. Wote walihimiza umuhimu wa Watanzania walioko diaspora kuwekeza nyumbani. Siyo lazima uwe na mtaji mkubwa lakini kama kuna Watanzania 10 na kila mmoja akichanga dola elfu moja tayari mnazo elfu kumi ambazo zinaweza kuwekezwa Bongo.
Mbali na uwekezaji na biashara, yalijadiliwa pia masuala ya dual citizenship, ambapo Membe aliwahakikishia wadau kuwa bado linashughulikiwa na yeye anaunga mkono kabisa kutolewa kwa duo citizenship kwa sababu, kama alivyosema, serikali inatambua mchango wa raia wake waliozamia nchi za nje kwa sababu kedha wa kadhaa, na wakati huo huo, kama wamechukua uraia wa nchi nyingine za kimaslahi basi wananyang'wanywa uraia wa Bongo. Hiyo aliiita kuwa ni "contradiction" ambayo serikali inapaswa kuishughulikia na wanalishughulikia. Suala la urasimu ambapo mtu anayetaka kuanzisha kampuni inamchukua hadi miezi sita kukamilisha taratibu pia lilijadiliwa. Suala la madini likagusiwa na inaonekana viongozi serikalini wanatambua kasoro zilizopo katika mikataba. Lakini tuliondoka bila kuhakikishiwa ni hatua gani zinachukuliwa kuondoa kasoro hizo. Niliondoka nikiamini kuwa serikali imepania kuwashirikisha na kuwasaidia raia wa Tanzania walioko nje wanaotaka kuwekeza nyumbani kwa kuondoa adha na kero wanazokumbana nazo wakati wanapotaka kuwekeza nyumbani. Tusubiri tuone kama zilikuwa ahadi hewa au la. Kama nilivyosema, nilienda Houston kama mtazamaji, lakini nimeondoka nikivutiwa na wazo na malengo ya DICOTA. Natumaini wata- update website yao ili sote tuweze kujionea kile wanachojaribu kufanikisha.

Nimerudi ukumbini ku-search hii DICOTA. Na nilitaka kuuliza kilichotokea lakini naona umejibu vya kutosha.

Thanks
 
Jasusi,
Mkuu wangu vitu vyote ulivyozungumzia ni vitu ambavyo Watanzania waishio nje wamekuwa wakiahidiwa toka wakati wa Mkapa.. Nakumbuka mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2002 au 03 Mkapa alipotembelea Holland.. Na hadithi imekuwa hiyo hiyo kila ujumbe wa rais, makamu wa rais na waziri wa mambo ya nje wanapotembelea nchi hizi. Sijui ni nchi gani maswali hayo hayakupewa promise kama hii..
Kwa hiyo, kilichofanyika Houston ni marudio tu, nakumbuka hata Lowassa alipokuja hapa tulipewa hadithi hizo hizo hakuna tumaini lolote zaidi ya usanii..

Binafsi nashukuru sana kwamba USA mumeweza kuanzisha chombo hiki lakini trust me hamtafika popote kwa sababu serikali inatakiwa kuwa mbele ya mipango kama hii..Hadi sasa hivi hakuna na nina hakika serikali yenyewe haifahamu chombo hiki kinafanya kazi vipi..Swala la kuvitaarifu vyama vyote vya majimbo ya USA ni muhimu sana na lazima uwakilishi wa vyombo hivi uwepo mpate kujenga sauti moja kubwa, laa sivyo itakuwa hadithi ile ile ya kugawanyika na utengano..Na kama kawaida serikali itarusha juu ua la - Sadaka llahu, mwenye kupata na apate! Haya yametokea Uingereza na bilashaka ni kutokana na serikali kutoelewa umuhimu wa chombo hiki isipokuwa inatazama ni watu gani wanaoshiriki.

Hata hivyo sintapenda kuwavunja nguvu isipokuwa ni muhimu sana mjipange wenyewe kwa nguvu zenu msitegemee serikali yetu hata kidogo..sana sana mtawapa idea ambazo watazitumia wao kwa faida ya familia zao..Mashirika mengi ya Canada ambayo yamewekesha Tanzania yameingia huko kwa kutumia Watanzania waishio hapa..Na trust me, wengi wao hata ofisi za mashirika hayo Bongo hawaruhusiwi kuingia, wala kupewa mkono wa shukran. Na serikali (viongozi) hawafahamu kwamba ni nguvu na sauti za vijana wake waishio nje ndio wamewezesha Wawekezaji wengi toka sehemu moja kuja Tanzania. Wawekezaji ambao hawaja wahi fika wala kufahamu Tanzania ipo wapi ktk ramani ya dunia.

Misafara ya JK na viongozi wetu haivutii kabisa wawekezaji zaidi ya wachache waliohudhuria kupitia Ubalozi au ujumbe wa vyama vya Watanzania. Wafanyabiashara wote ambao huandamana na rais ktk safari zake ni wachache sana wamepata deal za ku supply mali zao, wachache sana na hata ukitazama imports za Tanzania nchini Marekani, Vinyago vina ongoza ktk list. Ni mtanzania Diaspora anayechonga nchini kwetu na kuviisambaza US, lakini hata siku moja sijasikia akisifiwa wala kupewa heshima kwa kazi aloifanya..Bila shaka DICOTA mtaweza kuwatuza watu kama hawa..hasa bibie mwenye kampuni ya vinyago - Out of Africa!..
 
Last edited:
Jasusi,
Mkuu wangu vitu vyote ulivyozungumzia ni vitu ambavyo Watanzania waishio nje wamekuwa wakiahidiwa toka wakati wa Mkapa.. Nakumbuka mara ya kwanza ilikuwa mwaka 2002 au 03 Mkapa alipotembelea Holland.. Na hadithi imekuwa hiyo hiyo kila ujumbe wa rais, makamu wa rais na waziri wa mambo ya nje wanapotembelea nchi hizi. Sijui ni nchi gani maswali hayo hayakupewa promise kama hii..
Kwa hiyo, kilichofanyika Houston ni marudio tu, nakumbuka hata Lowassa alipokuja hapa tulipewa hadithi hizo hizo hakuna tumaini lolote zaidi ya usanii..

Binafsi nashukuru sana kwamba USA mumeweza kuanzisha chombo hiki lakini trust me hamtafika popote kwa sababu serikali inatakiwa kuwa mbele ya mipango kama hii..Hadi sasa hivi hakuna na nina hakika serikali yenyewe haifahamu chombo hiki kinafanya kazi vipi..Swala la kuvitaarifu vyama vyote vya majimbo ya USA ni muhimu sana na lazima uwakilishi wa vyombo hivi uwepo mpate kujenga sauti moja kubwa, laa sivyo itakuwa hadithi ile ile ya kugawanyika na utengano..Na kama kawaida serikali itarusha juu ua la - Sadaka llahu, mwenye kupata na apate! Haya yametokea Uingereza na bilashaka ni kutokana na serikali kutoelewa umuhimu wa chombo hiki isipokuwa inatazama ni watu gani wanaoshiriki.

Hata hivyo sintapenda kuwavunja nguvu isipokuwa ni muhimu sana mjipange wenyewe kwa nguvu zenu msitegemee serikali yetu hata kidogo..sana sana mtawapa idea ambazo watazitumia wao kwa faida ya familia zao..Mashirika mengi ya Canada ambayo yamewekesha Tanzania yameingia huko kwa kutumia Watanzania waishio hapa..Na trust me, wengi wao hata ofisi za mashirika hayo Bongo hawaruhusiwi kuingia, wala kupewa mkono wa shukran. Na serikali (viongozi) hawafahamu kwamba ni nguvu na sauti za vijana wake waishio nje ndio wamewezesha Wawekezaji wengi toka sehemu moja kuja Tanzania. Wawekezaji ambao hawaja wahi fika wala kufahamu Tanzania ipo wapi ktk ramani ya dunia.

Misafara ya JK na viongozi wetu haivutii kabisa wawekezaji zaidi ya wachache waliohudhuria kupitia Ubalozi au ujumbe wa vyama vya Watanzania. Wafanyabiashara wote ambao huandamana na rais ktk safari zake ni wachache sana wamepata deal za ku supply mali zao, wachache sana na hata ukitazama imports za Tanzania nchini Marekani, Vinyago vina ongoza ktk list. Ni mtanzania Diaspora anayechonga nchini kwetu na kuviisambaza US, lakini hata siku moja sijasikia akisifiwa wala kupewa heshima kwa kazi aloifanya..Bila shaka DICOTA mtaweza kuwatuza watu kama hawa..hasa bibie mwenye kampuni ya vinyago - Out of Africa!..
Mkandara,
Unayosema ni kweli kabisa. Kilichonifanya nijinunulie tiketi niende Houston ni kwamba nilitaka kuona mwenyewe "what is different this time." Mbali tu na maneno matamu, this time tumepewa ahadi za mawasiliano ya moja kwa moja na Wizara ya Mambo ya nje, BOT, TIC na CRDB. Sasa ni juu yao kuthibitisha kwamba they meant what they said na ni juu ya DICOTA to hold their feet to the fire, as it were. Na Foreign wameunda kitengo kinachoshughulikia diaspora kwa hiyo nina matumaini this time hatujaingizwa mkenge. But like they say, time will tell.
 
Lo. Mpaka huyu Sind Bad aondoke IKULU, NCHI ITAKUWA IMEFILISIKA! Sijui tufanyeje.
Huyu jamaa tungekuwa na uwezo watanzana wote tungemng'oa lakini hatuwezi maana wengi wetu bado hatuyaoni haya unayosema mheshimiwa. Kimsingi kwa sasa hali siyo nzuri na hadi atoke Tutakuwa nyakanyaka. Unajua! itabidi tukaombe watu waje wajenge nchi upya kama vile tulikuwa na vita
 
Labda ujio wa kina Abromoavich..will smith ..watu kibao kuja bongo pamoja na kanye..

anyways..Mkulu anapenda issue za namna hiyo...alafu kwa wale ambao hamkupata Nafasi ya kumuuliza swali ukimpigia anytime anapokea hasa muda wa jioni...
mi nina maswali kwa mkulu ni PM nipe number yake kiongozi
 
well nchi hii bado ni 'BIKIRA' i can say,tuna vyanzo vingi sana, resources nyingi sana(hapa ni watu pamoja na vitu/malighafi).inakuwaje aende marekani?wamarekani wenyewe watakuja kama mazingira ya kazi yanavutia,sijaona mtu kulazimishiwa kwenda mahali kufanya biashara wakati mwekezaji mwenyewe anafanya market research atatupata tuu.JK abaki nchini kwa 90% ya mua wake,naamini akisimamia miradi ya humu ndani yeye paersonally italeta faida zaidi kuliko kuenda USA personally kwa gharama kubwa bila faida,hakua business man atarisk kuleta hela yake hapa wakati umeme,maji,barabara,elimu vyoote unreliable.Nilisema nchi hii kuna watu wanawaza kuezeka wakati hata ukuta haujajengwa!tujenge kuta na kuimarisha msingi then tutapaua kwa wakati muafaka!Otherwise JK namwona kama lyfist flani hivi!!

Na mwaka huu ndo tutatolewa hiyo bikira
 
Hakuna kitu kipya zaidi ya kufanya safari kama hizi, na pia itakuwa ni busara kwa Jk kubaki na kubuni mbinu nyingine za kupata wawekezaji na kukusanya kodi kubwa sana toka ndani, na pia ni jambo la ajabu kuona kuwa VIcoda ndio wanampeleka huko,Sijakubaliana na jambo hili hata kidogo
Safari za nje ndio zinazoleta fedha na uhusiano mzuri wa kimataifa.

Mtembea bure si sawa na mkaa bure. Kalaga baho!!!!
 
Back
Top Bottom