Rais kuisuka upya NIDA na RITA, wakwama usajili wa watu

Rais kuisuka upya NIDA na RITA, wakwama usajili wa watu

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
RITA na NIDA wapo mbioni kufumuliwa na kusukwa upya kuendana na Kasi ya awamu ya sita.

Maeneo yanayotegemea kuwekewa mkazo nikudhibiti Watanzania na wageni waliozaliwa nje ya nchi kutokupata cheti cha kuzaliwa kama vile wamezaliwa Tanzania. Mwanya huu unatumiwa Sana kusaidia raia wa kigeni, wahamiaji haramu kupewa kitambulisho cha NIDA.

Eneo la pili ni kupanua wigo wa utoaji huduma ambapo kwa sasa usajili utafanyika hospitalini anapozaliwa mtoto. Kwa wale qanaozaliwa nyumbani viongozi wa serikali za mtaa watawajibika kuweka kumbukumbu zitakazo tumiwa na watumishi wa RITA kutembelea vijiji kutoa vyeti kupitia mobile service.

Eneo la tatu ni kuunganisha mfumo wa RITA na mifumo mingine ya serikali kielekronikia kama ilivyo kwenye ulimwengu wa kwanza.

Eneo la tano ni RITA kupewa jukumu la kutoa unique namba za kila Mtanzania na mgeni aliyezaliwa Tanzania. Namba hizi zitasaidia popote utakapotaka huduma au kusajiliwa.

Swali je, katika kuzisuka hizi taasisi kuna watu wenye modern mind au watarejeshwa wale wale wa analogy? Umofia kwenu.
 
Mimi hadi leo nina namba tu ya Nida bila kitambulisho mwaka wa 4 huu na mimefuatilia sana pale kata ya kirumba naambiwa havijaja😒
 
Safi maana vitambulisho wamekaa navyo miaka tele
 
Back
Top Bottom