Rais kutokupokelewa na Rais mwenzake: Tutofautishe kati ya State Visit (Ziara ya Kitaifa) na Working Visit (Ziara ya Kikazi)

Kwahiyo rais wa Marekani akija kwa work visite, Samia atauchuna ikulu hata enda kumpokea??
swali nzuri pia maana mambo yasijekuwa vinginevyo.lkn yanaeza kwa kujikomba sababu ngozi nyeusi ni shida.kuna mzungu mmoja alisema afrika inabidi itawaliwe tena.
 
Mleta uzi ameleta uzi kufanya propaganda, ila ni vyema akafahamu.

Leo hii Uhuru Kenyatta akifika Tanzania hasa Dar es Salaam au Dodoma kwa sababu yoyote ile lazima atafika Ikulu tu kama Rais yupo, vivyo hivyo kwa Samia, akifika Kenya hasa Nairobi lazima atafika Ikulu tu.

Rais wa taifa lingine kutembelea US na kupokelewa na Rais Marekani ni tofauti kwa sababu ya ukubwa wake duniani na wingi wa wageni wanaotembelea kwa siku Washington DC. Rais wa Taifa lingine Kukaribishwa au kuruhusiwa kukutana na Biden White House inahaususha mambo mengi sana ikiwemo mipango na taarifa ya muda mrefu, umuhimu wa Taifa lako kwa US na ukaribu wa kiongozi wenu na Rais wa US.

Sio jambo la ajabu kukuta kuna Marais, mawaziri wakuu au wafalme wa mataifa mengine zaidi ya watano kwa siku Marekani, bado kuna lundo la viongozi wa serikali na nje ya serikali ambao Biden anatakiwa aongee nao kwa simu au video kila siku. Kwa jinsi hiyo ndio maana wa Rais wa Taifa lingine anaweza kufika US na asifike White House au kukutana na Rais wao.

Africa unapozungumzia mataifa yenye kipaumbele kikubwa kwa US ni Misri, South Africa na Kenya. Hayo ndiyo mataifa marais wao wanaweza kuwa wamekwenda US kwa mambo yao mingine wakapata nafasi ya kukutana na Rais wa US kirahisi nje ya ratiba zake rasmi.
 
Umeishia la ngapi? kuna rais wa nchi yoyote aliyewahi kuja hapa akapokelewa na RC? Hapa hadi PM Mstaafu wa UK Tony Blair alikuja mara mbili na kulakiwa na SSH, G. Bush kaja akiwa mstaafu mara karibia mbili kapokelewa na JK, acha kuongea pumba
 
Hoja yako ya msingi ni ya upotoshaji, hiki unachosema ni kwa mataifa machache sana ambayo wageni wa mataifa mengine hawakauki nchini mwao kama Marekani, UK Ufaransa, Ujerumani, na China.
 
Makonda katika ubora wako.
Hivi wewe si ndo ulimpigia chapuo mama kipindi kile kuwa atafaa kuwa makam wa rais? Akaukwaa umakamu na hatimaye urais, halafu amekukaushia amekupandishia tinted.

Sema mkitifuana hivi mi ndo napenda
 
Hata akienda kama work visit, atahesabika kama mgeni wa kitaifa kutokana na umuhimu na nafasi ya taifa lake kwenye taifa la US.

Xi wa China, Boris Johnson, Zelenskyy, Cyril Ramaphosa, Al Sisi, Salman bin Abdulaziz Al Saud wa Saudi Arabia au Macron wakifika US kwa sababu yeyote ile isipokuwa labda kutibiwa, kupokelewa na Biden ni uhakika kwa 99.9%. Rais wa US atakutana nao White House, Camp David au kwenye tukio waliloloendea iwe ni katika kiwanda au mkutano n.k.
 
Mataifa mengi jinsi kiongozi wa nchi nyingine anavyopokelewa Inatokana na umuhimu kati ya mataifa hayo husika kiuchumi, kiusalama, mfumo wa uongozi n.k
 
Ana shobo sana huyu mother. Utazani aja wai kusafiri
 
Pamoja na maelezo yako, haibadilishi maana ya STATE VISIT na WORK VISIT!! Haya ni maneo rasmi ya kikazi katika UWANJA WA KIDIPLOMASIA.

Sijasema kuwa kwenye work visit Rais anayetembelea hawezi kuonana na Rais mwenyeji, ila ni kwamba SI LAZIMA!! Pia sijasema kuwa kwenye work visit Rais mwenyeji hawezi kwenda kumpokea Rais anayetembelea, ila SI LAZIMA!! Anaweza akampokea kwa mapenzi yake mwenyewe lakini SI WAJIBU!. Ila Kwenye State visit NI LAZIMA RAIS AANDAE MAPOKEZI YA RAIS MWENZAKE (maana amemwalika rasmi), ATAENDA KUMPOKEA MWENYEWE KIBINAFSI AU ATATUMA MWAKILISHI WAKE MWENYE UZITO UNAOSTAHILI (ambapo bado itahesabika amepokewa na Rais).

Sijaleta uzi huu kama propaganda kama unavyodai, ila ni mchango wangu kutoa elimu kwa wanaohoji kwa nini kwenye baadhi ya ziara za Rais hakupokeleewa na Rais mwenzake!! Niliyotoa ni elimu ya kidiplomasia na unaweza kuhakiki mwenyewe maana ya STATE VISIT na WORK VISIT. Siku zote kabla hujalaumu kwa nini rais hajapewa heshima uliyoitazamia, mahali pa kwanza pa kujiuliza ni je alienda huko kama state visit au kama work visit!! State visit Rais huwa amealikwa rasmi na Rais mwenzake!! ni Mgeni wake wa kitaifa!! Ni lazima ampokee!!
 
Mataifa mengi jinsi kiongozi wa nchi nyingine anavyopokelewa Inatokana na umuhimu kati ya mataifa hayo husika kiuchumi, kiusalama, mfumo wa uongozi n.k
Bora hizo ziara zisiwepo kama zinamdhalilisha Rais kiasi hicho!
 
Ikitokea Rais wetu akaalikwa rasmi na Biden kutembelea Marekani, mambo yafuatayo yatafanyika:
1. Rais Biden ataandaa mapokezi ya Rais mwenzake kwa kumpokea yeye mwenyewe au mwakilishi wake mwenye uzito unaostahili.
2. Atakagua gwaride la kijeshi
3. Atapigiwa mizinga 21.
4. Atapatiwa malazi na chakula pamoja na usafiri wa ndani pamoja na ujumbe wake wote.
5. atapatiwa zawadi maalumu kama ukumbusho wa ziara hiyo ya kitaifa.

Watu watofautishe kati Rais kwenda Marekani kuhudhuria kikao cha UN na kwenda Marekani kama mgeni wa kitaifa kwa mwaliko wa white house!! Kuhudhuria kikao cha UN ni work visit!!
 
Umeelezea vizuri kabisa kuna state visit, official visit na private visit. Ni kweli state huwa pia anaambatana na watu mbali mbali kama wafanyabiashara wa nchini kwake, official nikama ulivyosema kujifunza na kuangalia fursa mbali mbali na private hata picha unaweza usione kampigwa sababu ni mambo binafsi labda kupumzika .State pia kunakuwa na chakula cha pamoja anachoandaliwa na mwenyeji wake ,official anaweza kufika na kufanya mazungumzo hata VIP airport na kugeuza, private anafika kimya kimya na kuelekea alipotarajia kupumzika.
 
Niwape mfano hapa wa Rais aliyealikwa rasmi na Rais Biden wa Marekani na akaenda huko kama STATE VISIT!




Biden Welcomes Kenya’s Kenyatta to the White House​


Kenya’s president will be the first African leader U.S. President Joe Biden has met at the White House.​

By Colm Quinn, the newsletter writer at Foreign Policy.
Kenyan President Uhuru Kenyatta speaks with then-U.S. President Donald Trump.
Kenyan President Uhuru Kenyatta speaks during a bilateral meeting with then-U.S. President Donald Trump in the Oval Office of the White House in Washington on Aug. 27, 2018. OLIVIER DOULIERY/ POOL VIA GETTY IMAGES
OCTOBER 14, 2021, 6:17 AM

Biden Welcomes Kenyatta to the White House
U.S. President Joe Biden hosts his Kenyan counterpart, Uhuru Kenyatta, today in Washington. Kenyatta is the first African leader to meet with Biden at the White House since he became president.
The two are expected to discuss a range of issues, from economics and security to climate change and human rights.

Yaani hapo alialikwa!! He paid a state visit to USA!!
 
Kenyatta mwaka jana alialikwa rasmi na Biden kutembelea Marekani. Hakukagua gwaride la kijeshi wala hakupigiwa mizinga 21. US anafanya mambo yake tofauti sana na mataifa mengine. Hawana mambo mengi ya kupoteza muda.

Hata kwenye sikukuu ya uhuru wao Rais wao huwa hakagui gwaride la jeshi. Trump ndio alitaka kufanya hivyo ikawa mjadala na jambo la kushangaza sana,.vyombo vya habari vikawa vinafananisha na nchi za kidekteta au kikomunisti jambo kama hilo.
 
Umeishia la ngapi? kuna rais wa nchi yoyote aliyewahi kuja hapa akapokelewa na RC? Hapa hadi PM Mstaafu wa UK Tony Blair alikuja mara mbili na kulakiwa na SSH, G. Bush kaja akiwa mstaafu mara karibia mbili kapokelewa na JK, acha kuongea pumba
Tofautisha kati ya wajibu wa kikazi na mapenzi binafsi au ukarimu binafsi!! Rais kwenda kumpokea rais mstaafu na huyo rais mstaafu HAKUWA AMEALIKWA RASMI hayo ni mapenzi binafsi ya rais mwenyewe wala si wajibu wake wa kikazi! Pia rais kwenda kumpokea rais anayekuja hapa nchini kama work visit si wajibu wa LAZIMA ila anaweza kumpokea kwa mapenzi yake binafsi na kwa kumwonyesha ukarimu!!

Nimeeleza maana na tofauti ya STATE VISIT na WORK VISIT na maana hiyo haikanushiki maana ndivyo ilivyo kidiplomasia!! Sasa usichukulie mazoea yetu tunavyowafanyia marais wanaotutembelea ukadhani NDIVYO INAVYOPASWA KUWA. Ndiyo maana kwa kufikiri hivyo watanzania wengine wanashangaa sana kwa nini rais wetu akienda nje mara nyingine hapokelewi na Rais kama tunavyotegemea au kama sisi tunavyowafanyia marais wanaotutembelea??

Mwisho kwa kuwa umeniuliza umeishia la ngapi, nikujibu tu kwamba nina shahada ya uzamili, lakini sijaishia hapo maana elimu haina mwisho!! Labda utupe wewe maana na tofauti ya state visit na work visit kama ubavu huo unao!!
 
Anaweza kufanya hivyo kwa mapenzi yake mwenyewe na kwa urafiki wao lakini SI WAJIBU WA LAZIMA WA KIKAZI kama wameenda Marekani kama work visit!! Kitu kingine ambacho hukielewi ni kwamba marais wengi huwa hawatembelei nchi nyingine kama work visit maana hilo MARA NYINGI LAKINI SI MARA ZOTE ni eneo la watendaji zaidi kuliko mkuu wa nchi!!
 
Work visit (safari ya kikazi) huwa mtu hajakaribishwa rasmi na mkuu wa nchi husika! lakini yeye anadhani kuna mambo anaweza kuyafanya huko kama majadiliano au kutembelea sehemu mbali mbali kwa ajili ya kujifunza nk!
Hii definition umeitoa wapi? yaani unaenda nchi ya mtu bila kukaribishwa, hiyo work visit unaifanyaje, unaenda kutembelea maonyesho ya nanenane ya huko kujifunza biashara au kilimo, unatuonaje humu ndani aisee?? au ndio unatafuta justificationa mama alipoenda USA kuzindua filamu na hakuwa noticed kama kuna mkuu wa nchi ameingia, yaani alialikwa kama muigizaji wa filamu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…