Rais kuzuia mchakato wa mabadiliko ya Katiba ni kuvunja Sheria

Rais kuzuia mchakato wa mabadiliko ya Katiba ni kuvunja Sheria

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Taifa zima limekuwa likidhani kuwa suala la katiba mpya ni hisani ya CCM au rais aliyeko madarakani. Hili jambo siyo kweli hata kidogo.

Suala la katiba mpya linaongozwa na Sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012.

Katika sheria hii, hakuna mahali rais amepewa mamlaka ya kuzuia mchakato wa katiba mpya kusonga mbele, au kujaribu kuufuta kwa namna yoyote ile.

Ukisoma sheria hiyo, imeweka utaratibu maalum wa namna ya kuunda tume ya kukusanya maoni, ikaweka utaratibuwa kuunda bunge la katiba, ikaweka utaratibu wa kutangaza rasimu pendekezwa kwenye gazeti la serikali, na ikaweka utaratibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuandaa zoezi la kura ya maoni.

Tukumbuke tu kuwa hatua tuliyokuwa tumefikia ni kusubiri Tume ya Taifa ya Uchaguzi iitishe kura ya maoni kuwauliza wananchikama wanaikubali Rasimu Pendekezwa au la.

Rais Magufuli alivunja sheria pale alipozuia mchakato wa katiba mpya kuendelea mbele, hakuwa na mamlaka hayo kisheria. Hatua iliyokuwa inafuata iko mikononi mwa NEC na si Rais.

Sehemu kubwa ambayo sheria ile imempa rais madaraka juu ya hatma ya katiba ni sehemu mbili, ya kwanza ni ile inayompa mamlaka ya kuitisha tena bunge la katiba kuboresha rasimu hiyo hata kama bunge hilo lilishatoa toleo fulani

Sebemu ya pili ni ile inayompa namlaka ya kuchagua siku baada ya Cycle nzima ya mabadiliko ya katiba kuwa imekamilika kuchagua siku ili hiyo katiba mpya ianze kutumika!

Kwa hiyo kama Rais Samia anawaza kupotezea suala la katiba mpya basi ajue tu kuwa anavunja sheria, tena anavunja shetia ya mabadiliko ya katiba, na yeye akumbuke aliapa kulinda sheria.

Kwa hiyo nampa wito Rais Samia, Ama aitishe upya bunge la katiba lipitie ile rasimu yake (ile ya Chenge) liiboreshe, au atimize sheria kwa kuiachia tume ya Taifa ya uchaguzi iitishe kura ya maoni ili sheria ya mabidiliko ya katiba itekelezwe.

Naambatanisha sheria ya mabadiliko ya Katiba
 

Attachments

Sina uhakika na ukweli wa ulichokisema. Ila nina uhakika kuwa sisi wananchi/ Watanzania ni kondoo.

Hatuna ujasiri wa kumpinga kiongozi [ambaye ni mtumishi wetu] wa juu hadharani na kwa vitendo, hata akosee namna gani.

Tutaishia kupiga tu kelele huku tumejificha.

Kama sheria zilizopo zinakiukwa waziwazi, sheria mpya za nini sasa?

Zikikiukwa waziwazi tutafanya nini?

Tubadilike kifikra. Tupo waoga mno!!
 
Sina uhakika na ukweli wa ulichokisema. Ila nina uhakika kuwa sisi wananchi/ Watanzania ni kondoo.

Hatuna ujasiri wa kumpinga kiongozi [ambaye ni mtumishi wetu] wa juu hadharani na kwa vitendo, hata akosee namna gani.

Tutaishia kupiga tu kelele huku tumejificha.

Kama sheria zilizopo zinakiukwa waziwazi, sheria mpya za nini sasa?

Zikikiukwa waziwazi tutafanya nini?

Tubadilike kifikra. Tupo waoga mno!!
At least tutumie haki yetu ya kikatiba kuwaambia ukweli. Tukinyamaza nalo ni tatizo.

Nimeweka pdf hapo ya sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012, Utaona wazi kuwa RAISI KUZUIA MCHAKATO WA KATIBA MPYA ni matumizi mabaya ya madaraka, Sheria hiyo inataka itekelezwe, siyo Isitishwe!
 
Haya tumekusikia!
Kusikia tu haitoshi! Tunataka Katiba Mpya. Katiba ya Wananchi! Hii iliyopo iliandaliwa mahsusi kwa ajili ya ccm! Sasa tunataka Katiba ya Watanzania wote na siyo kwa ajili ya ccm na wafuasi wake pekee.
 
Welll said,nachokiona wtz hutaman sana mazuri kupitia kwa wengne
Sina uhakika na ukweli wa ulichokisema. Ila nina uhakika kuwa sisi wananchi/ Watanzania ni kondoo.

Hatuna ujasiri wa kumpinga kiongozi [ambaye ni mtumishi wetu] wa juu hadharani na kwa vitendo, hata akosee namna gani.

Tutaishia kupiga tu kelele huku tumejificha.

Kama sheria zilizopo zinakiukwa waziwazi, sheria mpya za nini sasa?

Zikikiukwa waziwazi tutafanya nini?

Tubadilike kifikra. Tupo waoga mno!!
 
Kusikia tu haitoshi! Tunataka Katiba Mpya. Katiba ya Wananchi! Hii iliyopo iliandaliwa mahsusi kwa ajili ya ccm! Sasa tunataka Katiba ya Watanzania wote na siyo kwa ajili ya ccm na wafuasi wake pekee.
Haya na wewe wa pili tumekusikia ngoja tusubiri na wengine maoni yao.
 
At least tutumie haki yetu ya kikatiba kuwaambia ukweli. Tukinyamaza nalo ni tatizo.

Nimeweka pdf hapo ya sheria ya mabadiliko ya katiba ya mwaka 2012, Utaona wazi kuwa RAISI KUZUIA MCHAKATO WA KATIBA MPYA ni matumizi mabaya ya madaraka, Sheria hiyo inataka itekelezwe, siyo Isitishwe!
Hivi kwa nini hatuwezi kuwa kama wale Waarabu kipindi cha Arab Spring? Au wa-Ukraine kipindi cha Orange Revolution?
 
Hivi kwa nini hatuwezi kuwa kama wale Waarabu kipindi cha Arab Spring? Au wa-Ukraine kipindi cha Orange Revolution?
Tatizo hatuna Viongozi/watu wa kujitoa kafara kwa manufaa ya wengine.

Yaani hatuna kizazi kama cha yule Mhitimu wa chuo wa Tunisia, aliyeamua kujilipua na petroli mchana kweupe baada ya kukosa ajira, akaamua mwenyewe kujiongeza kwa kuuza matunda barabarani, halafu wale washenzi wakaiharibu biashara yake.
 
Ccm wakisikia neno Katiba mpya,wanadhani ndiyo mwisho wa dunia umefika
 
Tatizo kubwa ni CCM,Kikwete kama Rais alikuwa radhi kutupa katiba mpya yenye serekali 3 hilo lilithibitika katika usemi wake wa kuwataka wanachama wa CCM wajiandae kisaikolojia kupokea serekali 3,CCM kwa kuwa wananufaika na katiba iliopo walimjia juu Kikwete ambaye alilazimika kubadili gia angani na kufuata matakwa ya chama chake.
 
Hapa nina mawazo tofauti kidogo, tatizo sio Rais kuzuia mchakato yani usimlaumu Rais kuzuia upatikanaji wa Katiba Mpya, hapa tatizo ni mfumo tuliojiwekea unaompa Rais mamlaka ya kuingilia kila kitu na kukipeleka vile atakaavyo.

Kama unakumbuka vizuri hili tatizo lilianzia kwa Magufuli, na sasa Samia analiendeleza, na ninaliita tatizo kwetu, lakini kwao sio tatizo kwasababu hii Katiba Iliyopo inawapa kila wakitakacho.

Sasa issue iliyoko hapa ni kwa namna gani tutajinasua kwenye huo mtego, yani tuyaondoe vipi madaraka ya Rais wa JMT yasiingilie mchakato wa Katiba Mpya ya wananchi inayotakiwa huku tukiwa chini ya Katiba hii ya sasa tuliyonayo inayompa Rais nguvu na mamlaka ya kuingilia kila kitu?

Tukiweza kujibu hilo swali hapo juu ninakuhakikishia Katiba Mpya itapatikana, ni lazima pawepo na namna/mbinu/njia itakayotuwezesha kuipata Katiba Mpya bila kusubiri ruhusa toka kwa mwenyekiti wa CCM kwasababu hilo halitawezekana kamwe.
 
Hapa nina mawazo tofauti kidogo, tatizo sio Rais kuzuia mchakato yani usimlaumu Rais kuzuia upatikanaji wa Katiba Mpya, hapa tatizo ni mfumo tuliojiwekea unaompa Rais mamlaka ya kuingilia kila kitu na kukipeleka vile atakaavyo.

Kama unakumbuka vizuri hili tatizo lilianzia kwa Magufuli, na sasa Samia analiendeleza, na ninaliita tatizo kwetu, lakini kwao sio tatizo kwasababu hii Katiba Iliyopo inawapa kila wakitakacho.

Sasa issue iliyoko hapa ni kwa namna gani tutajinasua kwenye huo mtego, yani tuyaondoe vipi madaraka ya Rais wa JMT yasiingilie mchakato wa Katiba Mpya ya wananchi inayotakiwa huku tukiwa chini ya Katiba hii ya sasa tuliyonayo inayompa Rais nguvu na mamlaka ya kuingilia kila kitu?

Tukiweza kujibu hilo swali hapo juu ninakuhakikishia Katiba Mpya itapatikana, ni lazima pawepo na namna/mbinu/njia itakayotuwezesha kuipata Katiba Mpya bila kusubiri ruhusa toka kwa mwenyekiti wa CCM kwasababu hilo halitawezekana kamwe.
Kuhusu ubaya wa katiba hii ya sasa, hilo liko wazi.
Hata hivyo pamoja na ubovu wa katiba hii kuna mambo raisi anazuiwa na sheria kuyafanya, mfano mmojawapo ni kuvunja sheria.
Japo kumshitaki hatuwezi lakini akivunja sheria lazima tumueleze wazi kuwa kavunja sheria.
Mfano mmojawapo ambao rais anavunja sheria ni katika suala hili la mchakato wa mabadiliko ya katiba mpya, hili suala lipo kisheria, kama raisi anagoma kuendeleza mchakato huo basi naye anakuwa anavunja sheria
 
Kuhusu ubaya wa katiba hii ya sasa, hilo liko wazi.
Hata hivyo pamoja na ubovu wa katiba hii kuna mambo raisi anazuiwa na sheria kuyafanya, mfano mmojawapo ni kuvunja sheria.
Japo kumshitaki hatuwezi lakini akivunja sheria lazima tumueleze wazi kuwa kavunja sheria.
Mfano mmojawapo ambao rais anavunja sheria ni katika suala hili la mchakato wa mabadiliko ya katiba mpya, hili suala lipo kisheria, kama raisi anagoma kuendeleza mchakato huo basi naye anakuwa anavunja sheria
Huwa wavunja kwa sababu wanajua hatuwezi kuwashtaki, ndio maana nikasema itafutwe njia ya kuipata Katiba Mpya bila kusubiri ridhaa ya Rais wa CCM, coz hiyo sheria wataendelea kuivunja tu.
 
Samia ni bomu.Takwa la katiba mpya ni takwa la wananchi wala siyo takwa la CCM,wala chadema wala Rais.
 
Back
Top Bottom