Rais Magufuli aagiza Madaktari waliohama Hospitali ya Rufaa mkoani Tabora kwenda Hospitali binafsi kwa kisingizio cha maslahi wafuatiliwe

Sorry to say this but rais hapa umeteleza!!

Unaposema unawasomesha hawachangii kwani hiyo mikopo si inatokana na kodi? je hizo hospitali za private hazilipi kodi?

Unaposema hela yenu wamekula wamekula kivipi? kwani hawalipi mkopo kila mwezi?

Alafu mzee baba hujui mtumishi yeyote anatafuta maslahi? sasa wewe huongezi mishahara unataka waendelee tu kukaa hapo kisa uzalendo?

Mzee huu ni mwaka 2021 na sio mwaka 1970! unapoongea jua unaongea na watu wenye akili zao kichwani!!

Huwezi ukawa mzalendo kama una njaa! HATA WEWE ULIKIMBIA CHAKI UKAENDA KWENYE SIASA!!
 
Unasema vipi daktari kala pesa wakati ni mkopo ulimpa? halafu hiyo mikopo haiwezi kuwazuia watu kutafuta maslahi mazuri zaidi, kwanza mikopo yenyewe mmeweka riba ili kuzidi kuwakamua, wacha wakimbie.
 
Kwani akiwa huko hospitali binafsi, si anarejesha mkopo!? Ama mimi ndiye nimeingia kwenye uwanja wa mpira na shoka!!!
====
Kuna uwezekano mkubwa Rais amenukuliwa vibaya, ngoja nitafute chanzo halisi.
 
Ingekua sahihi kama angaelipa kwanza 100% ya mkopo wa Serikali aliokopa na riba yake ndio atoke
 
kama vile huko private anaenda kutibu mawe sio watanzania. insanity
 
Asante sana Mh. Rais kwa uzalendo wako huo!!

Sasa ninaomba wasaidizi wa Mh. Rais wawe wanamshauli Rais, wasimwachie Rais ahangaike na hizi operational issues peke yake.

Mshaulini Mh. Rais maana ya so called Public-Private Partnership kwamba Public sector inaitegemea pia Private sector, kwahiyo sio mbaya kwa huyo Dr. kwenda kwenye hospitali binafsi. Cha msingi Serikali iangalie maslahi ya hao Dr. ili wasirubuniwe.

Above all, kwani wagonjwa wanaotibiwa kwenye hiyo hospitali binafsi si ni Watanzania??.....tatizo liko wapi hapo?????.....si Serikali bado itasifiwa tu kwa kuweka mazingira bora ya uwekezaji???

Tafadhali wasaidizi wa Rais, msaidieni Mh. Rais katika mambo yanayofanana na hilo pia

Otherwise, nakushukuru sana Mh. Rais kwa uzalendo wako huo.
 
Hivi kumbe kuna watu wanalazimishiwa kazi ili hali hawaitaki dah, hii nchi hata nikifa ikatokea maisha ya pili duniani nitaomba nirudi Tanzania
Tena kasema kuwa wanapata mkopo, ambao wanaulipa kwa interest. Yani hii nchi inafurahisha, kama anataka wasihame basi wawasomeshe bure na kwenye mkataba wasaini kabisa lazima ufanye kazi kwenye hospital za serikali kwa muda flani. Kama ilivyo kwa scholarship baadhi za kwenda kusoma nje, unaambiwa kabisa kuwa baada ya kuhitimu lazima urudi kwenu ukfanye kazi kwa kipindi cha miaka kadhaa.
 
Huu sasa ni Udikteta uliokamilika. Asante Mungu kwa kumfunua Dikteta huyu anayejificha kwenye kisingizio cha uzalendo.
 
Hebu waambie na private sector wachukue mtaani, twende sawa
 
Ingekua sahihi kama angaelipa kwanza 100% ya mkopo wa Serikali aliokopa na riba yake ndio atoke
Kuna watu/ wafanyakazi wakienda masomoni, wanawekeana bond na mwajiri/ serikali tena kwa viapo mbele ya shahidi mwana sheria kuwa akimaliza masomo lazima arudi hapa kwenye kituo cha kazi afanye kazi miaka mitano ndipo ahame kutafuta marisho ya kijani ama aendelee pale. Na wanafanya hivi kwa sababu mfanyakazi wao huyo anakuwa analipwa mshahara akiwa kwenye likizo ya masomo.

Sasa akimaliza masomo na akasema anatafuta marisho ya kijani mbuga nyingine, bond inamlazimisha kulipa gharama/ stahiki zote alizolipwa akiwa masomoni.

Tukirudi kwa ndugu yetu daktari. Je. Alikuwa na bond na serikali !?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…