Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

Pongezi nyingi na hongera kwa Mheshiwa Rais kwa kurudishia fao la kujitoa, sasa tutatembea kifua mbele. Magu oyee.
 
Na ndiyo mwajiri namba moja aunaweza kuchukua maamuzi magumu.Nani alikudanya, subiri 2025 ikipendeza hadi 2030
Sina uhakika ulichoquote ulikisoma kabla au ulichoquote sio ulichodhamiria,kwani sioni mahusiano ya karibu kati ya hivyo viwili
Ila kwa kutokuacha mtupu, yy ameahidi mpaka 2023, hiyo 2025-2030 imekupendeza wewe
 
Mbona zipo baadhi ya sekta binafsi zina mishahara mikubwa zaidi ya iyo ya serikali
 
Hivi kwanini ni lazima wanitunzie pesa zangu halafu waanze kuamua namna gani ya kunilipa?

Sent from my WAS-TL10 using Tapatalk
 
Bwanamkubwa kapata la kufungia mwaka. anamaliza mwaka akiwa shujaa anasifiwa. makofi na vigeregere kwake. kama ilivyo kawaida yake anatengeneza tatizo kisha analaumu watangulizi . anatufanya fyatu hatuna akili. kwakuwa tumezoea kusifia tutasifia .... haijawahi kutokea? .... ni raisi wa pekee... hamnazo.
kama nilimsikia vizuri bwana haambiliki alisema kikotoo kimeahirishwa hadi 2020 nasi twashangilia kama kumeza panadol kupunguza maumivu mnashangilia nini?
Mwaka wa tatu baada ya raisi kuingia madarakani 2015 hakuna nyongeza ya mishahara wala maslahi mengine huku hali na gharama za maisha zikiwa zimepanda sana kuanzia kodi ya pango mpaka nauli za kwenda kazini. watumishi wananyanyaswa wanaitwa majina mabaya kila uchao.
swali langu kwa viongozi wa vyama MLIKUWA MNASHANGILIA NINI PALE IKULU?
watumishi wa umma wa Tanzania amkeni hakuna viongozi wanaowajali ni waigizaji tuu
 
Kwani umeambiwa FAO la kujitoa limerudishwa ?!!
.....kama umeelewa hivyo jitakafari upya

Sent using Jamii Forums mobile app
hakuna fao la kujitoa ila kuna kujitoa uanachama na kuchukua michango yako ndio hiyo itaendelea untill 2023 kwa hiyo ni kucheza na hii ngoma tu kabla 2023 πŸ˜›πŸ˜›πŸ˜€πŸ˜€
 
Regardless ya nani kutengeneza tatizo na nani kalitatua, bado tuna kitu cha kupongeza kwa maamuzi haya.

Pia naomba FAO LA KUJITOA liwe nalo limerudishwa.

Ukipitia summary ya aliyoyazungumza lipo no 6.Ni kama kila kitu limerudi kama zamani.
 
Kimsingi Hakuna jimya alilofanya raisi, na hapakuwa na sababu tucta kumshangilia rais kiasi hicho. Hii ni aibu kwa raisi kwasababu tatizo katengeneza mwenyewe na kutatua mwenyewe. Haiingii akilini raisi akasababisha tatizo na kulimaliza mwenyewe!! Hapa kunatatizo la kukurupuka kiutendaji. Kama wapinzani na tucta wasinge lalamika, 25% ingebakia Kama ilivyo.
Rais ameamuaje!
Maana mm singii sana jf sahv
Maana bado nakula Biereee
Vp rais wetu kaamuaje?

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukipitia summary ya aliyoyazungumza lipo no 6.Ni kama kila kitu limerudi kama zamani.

Itakuwa heri sana, ngoja tusubiri.

Ndani ya 2 weeks tutakuwa tumejua. Ila inabidi wajichange sana, maana sasa hivi kuna wana kibao wako mtaani wanaosubiri hii hela.
 
Hii yote ni katika ule mkakati wa kutafuta sifa. Tatizo kalitengeneza mwenyewe sasa anataka alitatue ili asifiwe. Anataka kila mara kuwa live ila bunge kuwa live hataki kusikia kabisa. kiumbe selfish kupitiliza
Unaijua historia ya kikototoo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…