Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

Hongera sana rais wetu kwa kusimama upande wa watumishi ambao wengi wao walikuwa wameanza kupoteza matumaini.Tunaomba pia ulishughulikie suala la nyongeza ya mishahara.Maneno yako yalidhihirisha nia njema uliyo nayo kwa Tanzania na watu wake wote.Viva JPJM.

Kupinga kila kitu na kusifia kila kitu ni upungufu wa fikra pevu.

Be blessed abundantly my president.

Mheshimiwa Rais tunakupenda sana kwa kutujali sisi Wafanyakazi, lakini kuna tatizo jingine kwa Wafanyakazi waliopo kwenye miradi inayoendelea hivi sasa nchini ikiwemo mradi wa ujenzi wa reli ya Standard Gauge hawa Waturuki hawatulipi mishahara yetu hasa sisi Madereva yapata miezi minne sana hatujalipwa na pia wamekuwa na wakidaiwa maeneo mengi pamoja na watoa huduma mbalimbali kama wanaoleta wanaokodisha magari tunaomba Serikali ifuatilie kwa kina huku Standard Gauge hali si nzuri kwa kweli.
 
Mtaje tu huyo waziri kivuli. Tuwape moyo wenzetu hawa wanaotutetea. Wakifanya vema, tuwape credits zao. Hiyo itatupa haki ya kuwananga pale wanapoboronga au kushindwa kutimiza wajibu wao.

Hata Mh Mnyika pia anastahili pongezi maana naye hakusita kuchagiza kuhusu kikokotoo pale alipopata dk 5 za "kusalimia" (sote tunajua alivyonangwa baada ya hapo!)

Halafu kuna watu wanatamani "upinzani" ufe!!!
Hazikufika dk 5 mkuu!! Zingekuwa hizo wangempokonya mic!! Au angesombwa mzobe mzobe kutolewa ukumbuni. Aaaaah sorry kutolewa jukwaaani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: SMU
maji yalizidi unga,kama ingekua busara zake basi muswada wa sheria iliyoleta kadhia hiyo asingeisani
 
Watu sijui akili zenu mnawekaga wapi? Yeye ndiye aliyepitisha baada ya kuona hali mbaya akaamua kujifanya kama hajui kinachoendelea!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Watu wanashindwa kusoma alama za nyakati kama alivyosoma yeye. Baada ya kuona hii kitu inamkalia vibaya,ndio kaamua kuigeuza icheze upande wake. Hivi sasa anaonekane shujaa ameleta kitu kigeni sana. ”Hii ndio ile unshangilia kulipwa elfu 10 kumbe halali yako ni elfu 2”

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SIKU HIZI WAO NI WATETEZI WA HAKI ZA BINADAMU NA DEMON-KRASIA
 
Hili tatizo lilibarikiwa na bunge bila boss kutia wino??
 
Haha sa hv wanaanza kusema rais anaogopa cheche za Lisu wanahamisha magoli tu a.k.a wanatapatapa
Wakati Mnyika na Bulaya wanakomalia jambo hilo si ni nyie mlikuwa mnawazodoa na kuwarushia vijembe ?! Juzi kwenye uzinduzi wa barabara, Mnyika aligusia swala hili. Alichofanya mh ni kumkrash Mnyika. Na kuwaambia wananchi wasimuamini !!

Leo kalizungumzia Rais mnampandisha chati huku akiwa mwanzilishi wa picha.

Nchi hii ni yetu sote tuheshimiane tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi si ndiye aliye tia sahihi ikawa sheria?

Lawama zirudi kwa bunge, wao ndio wanaamua sheria iwaje. Rais kazi yake ni kuidhisha ianze kazi, wabunge wakiamua kuinadili watabadili any time.
 
Hilo ni tamko halijulikani liatishi muda gani kumbuka sheria bado iko pale pale

Kama angekuwa na nia njema angerudisha sheria bungeni itenguliwe na iundwe upya kwa kushirikiana na wadau wote



Sent using Jamii Forums mobile app
Mtu wa kurudisha bungeni ikatenguliwe yuko wapi?. Anatengua yeye mwenyewe na kuwapekekea tu wapige brash kile kitu ulichokiamua yeye. Wabunge wenyewe wa chochote ndioooooo.... ule uwingi wao wa ndioooo.... tayari ameshawafirisi kifkra,anawaona mambwiga tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NSSF SECTOR BINAFSI NA SISI MTURUDISHIE FAO LETU LA KUJITOA KAMA ZAMANI ,WAKATI TUKIWA KWENYE KIPINDI CHA MPITO HADI 2023,
KAMA KULIVYOFANYIKA KWA KIKOKOTOZI CHA ASILIMIA25
 
Back
Top Bottom