Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

CCM ni watu wa jabu sana, Inasikitisha sana kuona jinsi ambavyo wanatengeneza tatizo halafu wanalitatua ili kujitafutia KIKI hasa ktk kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa (2019) na uchaguzi mkuu (2020). Janga yenu tumeing’amua. Huwezi kuwa na wasaidizi wako unawatuma waje waharibu halafu wewe ujitokeze kusawazisha mambo. Ni aibu kubwa sana. Mtu mzima ukijivua nguo kwa makusudi huna sababu ya kuchutama. Tembea wima watu waone uchi wako.
 
"Hivi yeye hakuwa sehemu ya walioipendekeza hiyo sheria? Je, aliyeisaini na kuruhusu ianze kutumika ni nani?"

Create a problem, then solve it....

Halafu mnatuona wafanyakazi kama hatuna akili vile. Tunajua tu, na 2019 ngonjera za mishahara mizuri zitaanza.
 
m nipo tofauti kidogo ...napata mashaka kilichoangaliwa hapa ni uchaguzi serikali za mitaa na uchaguzi wa mwaka 2020...halafu watakuja na kauli kwamba wameshindwa kuelewana so sheria ibaki palepale.....cha muhimu wafanyakazi waendelee kukaza mpaka sheria ifutwe kwanza ...hiyo 2023 waje na muswada mpya.......je 2023 akisema iwe 15% na atakua anaondoka zake madarakani......msiseme hamkukumbushwa........
 
Kama wafanyakazi wenyewe ndo hawa wanaopongeza basi ni halali kupewa 25%.

Ujinga umeshamiri sana Tz kwakweli
 
Hapa kwenye heading sijakuelewa unaposema zawadi una maanisha nini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu mtu wa hovyo sana. Anatengua kitu kwa utaratibu wake badala ya kupeleka hoja bungeni sheria irekebishwe. Ndiyo hivyo tena ukiwa na kikojozi subiri watu washuhudie godoro likianikwa.
 
Full umakaveli. Mchiavelli anasema kuwa mtu akitaka kudannganya hawezi kosa watu wa kuwadanganya.

Pia anasema ki9ngozi mnjanja akipata nafasi anatengeneza tatizo, kisha analitatua na kupata sifa kemkem.
 
TUNDU LISSU anajua kuzipanga vizuri Karata zake
 
Du sasa Zitto sijui ataongea nini ,maana yeye na wenzake walitaka kuifanya issue ya mafao mtaji wa kisiasa kama ilivyo kawaida yao,sasa watabaki kuhangaika na katuni za mwenzao Kipanya za FastJet
 
alizungumzia vizuri sana. Amesema migodini na kwenye contractors, ajira ni za muda wa miaka miwili mitatu, haingii akilini kuambiwa usubiri mafao yako hadi ufikishe umri wa miaka 60!.
P.
Yaaap, basi hapo kalipangua , ina maana lipo Tena
Guuud president
 
Mpaka 2023? ? Baada ya hapo inakuwaje? ? Nyie shangilieni tu kama mazuzu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…