Rais Magufuli aidha amedanganywa kuhusu Barakoa au kuna tatizo sehemu (kwa alichoongea leo Feb 21, 2021)

Rais Magufuli aidha amedanganywa kuhusu Barakoa au kuna tatizo sehemu (kwa alichoongea leo Feb 21, 2021)

Kuna upotoshaji unaendelea. Sijui ni kwa malengo gani... No wonder tunaambiwa Siku ina masaa 48... Na tunakubali.
Ahsante Ndugu yangu kwa kusikia hiyo kauli na akafanya calculation ya barakoa 1 kutumika kwa saa 4 na hivyo kwa Siku zitahitajika 12.Makosa kama hayo yanafutikaje!Video zipo YouTube,kuna uwezekano wa Ku delete?Huyo ni Rais Msomi wa Chemistry mwenye Dr.Itakuwaje?
 
Hapa nilipo leo limepita tangazo korona imerudi.. korona imerudi wananchi mchukue tahadhari.. kila nyumba au duka lazima iwe na ndoo ya maji, marufuku mikusanyiko.. ukikiuka unakamatwa na mgambo. Naomba nisitaje eneo hilo ili kulinda ajira/vyeo vya hawa werevu
 
Anasema watu wanakufa kwa mipango ya Mungu. Anajivua lawama kwamba hata watu wafe wangapi yeye hahusiki, hana uwezo wala jukumu la kuzuia hilo.

Ana uwezo mdogo sana wa kufikiri na anawapa kazi sana wasaidizi wake. Nahisi wameamua wamuache tu!
Huyu aweza kufunga hospitali za umma huyu navyomuona. Kwamba kufa ni mipango ya nani?
 
Mbona hamuhoji wale wa church wanaposahau mpaka wa state ulipo na kuhimiza wananchi wafanye mambo yasiyo ya ki-church bali ya kisiasa shughuli zinazo fungamana na state!? Tukisema mnafanya double standard gestures tutakosea!?
unachangia mada gani?makosa ya watu wengine sio suluhisho la matatizo yako
 
Halafu Utafikiri kuwa hizo barakoa zinavaliwa usiku na mchana.
Ahsante Ndugu yangu kwa kusikia hiyo kauli na akafanya calculation ya barakoa 1 kutumika kwa saa 4 na hivyo kwa Siku zitahitajika 12.Makosa kama hayo yanafutikaje!Video zipo YouTube,kuna uwezekano wa Ku delete?Huyo ni Rais Msomi wa Chemistry mwenye Dr.Itakuwa
 
Wewe uelewa wako ni mdogo sana kama piriton. Spika yupo peke yake kwenye kiti chake,barakoa la nini?
Unalipwa shilingi ngap boss? Mbona unashupaza shingo sana? Ulisoma kweli? Mpaka darasa la ngapi? Matokeo yakawaje???
 
Simply sijaona kosa la Magufuli, bali ninachokiona ni chuki binafsi tu. 2020 alikuwa Rais yeye but hii ni vita, na vita ina mbinu nyingi na ndio maana hata vifaa vya kupimia corona walivishtukia baada ya kuona matokeo yanayotoka yana mashaka. Kumbuka wakati wanashtukia vifaa, of which kipindi hicho bado vifaa vya upimaji vilikuwa vichache kupatikana hata huko wanakotengeneza, tayari kulikuwa na kontena nyingi tu za barakoa zimeingia na zikapimwa kama zimefikia viwango vya kawaida bila kujua hizo ni carier za virus. Ishu ya mapapai ndiyo iliyofungua macho na kujua kumbe hata barakoa zina changamoto kama ambavyo baadhi ya vifaa vya upimaji. Nadhani unajua nini kiliwapata watu wa maabara kuu ya serikali ambapo ndani yake kulikuwa na watu wa usalama wa taifa ambao kiutaratibu sisi wananchi haturuhusiwi kisheria kujua wamechukuliwa hatua gani.
Mkuu hapo mnaniacha njia panda kwenye swala la vipimo kuwa sio vya kuaminika

Kwasababu wakati wizara ya afya inatoa takwimu za idadi ya wagonjwa waliobainika kuwa na corona vile vile kulikuwa na takwimu za watu waliopona huo ugonjwa

Sasa hao watu waliokuwa wanatangazwa kuwa wamepona corona walithibitishwa kupitia vipimo gani? (na ukumbuke hapo ilikua ni kabla ya magufuli hajabaini kuwa vipimo sio vya kuaminika)

Sasa kama vipimo vilikua vinatoa majibu ya uwongo kwa kila sampuli iliyopimwa kua ina virusi, vipi kuhusu idadi ya watu waliokutwa na virusi halafu baada ya matibabu wakaja kupimwa na kukutwa wamepona?
 
Back
Top Bottom