Rais Magufuli aidha amedanganywa kuhusu Barakoa au kuna tatizo sehemu (kwa alichoongea leo Feb 21, 2021)

Rais Magufuli aidha amedanganywa kuhusu Barakoa au kuna tatizo sehemu (kwa alichoongea leo Feb 21, 2021)

Wakuu,

Nimemsikiliza Rais Magufuli akiwa anaongea leo kanisani. Nimeshtuka, Rais anaongea kama layman kabisa. Hii ni hatari kwa Usalama wa Taifa kwa mtu ambaye amepewa dhamana ya juu kabisa hapa nchini.

Rais ni Comforter-in-Chief hivyo kama mfariji mkuu wa Taifa ana mamlaka makubwa aliyobebeshwa na hili inaelekea Magufuli analisahau sana. Huwezi toka huko na kuanza kuwambia watanzania eti “Kufa tutakufa tu”.

Rais ni kama BABA katika familia, na kwa Taifa yeye anasimama kama kichwa cha familia. Huwezi kuwa baba bora ukawa unatishia watu wako (wanao, mkeo, ndugu n.k). Kama baba, unaweza kulaumiwa, unaweza kuliliwa, unaweza kupongezwa, unaweza kuumizwa na hatutarajii kuwa utaitangazia familia kuwa wakome kufanya hivyo! Utakuwa umeshindwa kutekeleza majukumu yako.

Rais ni KIUNGO katika Taifa. Unapotokea mgawanyiko, ana wajibu wa kuhakikisha watanzania wanakuwa wamoja. Hili limekuwa likionekana kuwa tofauti kwa Rais wetu huyu.

Rais anapotoa kauli, ni kauli ya Taifa si yake. Mambo mengi anayoongea Magufuli watanzania walio wengi (wanaojielewa) watakubaliana nami kuwa si yale ambayo kimataifa tungependa kiongozi wetu ayaongee kwa niaba yetu!

Msikilize:



Sasa:

1) Magufuli leo kaongea UONGO mwingi kuhusu barakoa. Alichokiongea ni matusi kwa serikali yake mwenyewe!

- Kama barakoa zilizoingizwa nchini zina virusi au hazifai; kwanini watendaji wake wameziacha ziingizwe sokoni? Anataka kutuambia kuwa TBS na TFDA hawajui kazi yao? Kwanini watendaji wakuu wa taasisi hizi bado wapo kazini?

- Tukubali kuwa tumeingiziwa barakoa zenye kuwa na virusi ambazo zitawaua watanzania: Kwanini Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, IGP na CDF bado wapo kazini? Taifa letu manake usalama wake upo hatarini. Kwa mantiki hiyo, maduka ya madawa yavamiwe mara moja na barakoa zote ziondolewe sokoni

2) Magufuli amekuwa Rais wa kwanza mimi kumuona akiwa anahubiri katika Ibada za Kanisa Katoliki. Huu ni utaratibu wa kawaida kwa wakatoliki? Halafu anawachamba viongozi wa kanisa kwa kuhimiza waumini kujilinda?

3) Rais ametangaza dawa kadhaa kama Bupiji, COVIDOL etc, anataka kuwaaminisha watanzania kuwa Sayansi nyingine haifanyi kazi tena? Kuwa watanzania wasiziamini dawa nyingine zinazotolewa hospitali tena? Haya matangazo ya dawa za asili imekuwaje hadi wasaidizi wake wamwacha hadi ataje baadhi ya dawa moja kwa moja (kwa kutaja baadhi tu)? Ana maslahi nazo? Nasikia mtu aliwahi kuwa RC wa Dar ana mkono kwenye pharmacy chain flani, na kuna tetesi kuwa yupo kwa niaba ya ‘mzee’; hii haoni inazidi kujenga hisia zisizo sahihi?

Nitarejea

cha msingi wasiwe wanapewa nafasi ya kuongea kwenye nyumba za ibada
 
1613938234570.jpeg
 
Ninavyomjua Magufuli hili suala la kutilia shaka usalama wa barakoa lazima atalithibitisha kwa vitendo.

Ninamaanisha ataanzisha "movie" kuonesha kuwa imported masks si salama kama alivyotuonesha mwaka jana kuwa mfumo na teknolojia zinazotumiwa na maabara ya taifa kupima korona hazitoi majibu ya kuaminika ili abaki kuwa mkweli. Tusubiri na tutaona!
 
Inaelekea mheshimiwa saaana rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Muinjilisti John Pombe Magufuli ana ugomvi binafsi na barakoa.

Tatizo ni kuwa ugomvi huo ni ugomvi binafis, na siye wananchi tunasema hivi sisi binafsi hatuna ugomv na barakoa na wala hatuna haja ya kurithi maadui.

Mheshimiwa raisi kama anahisi barakoa ni adui, basi ni adui yake yeye binafsi sisi ni rafiki yetu.

Sasa kwa mfano atatushauri vipi tuone barakoa siyo Issue wakati juzi hapa tumeona walinzi wanamlinda raisi Kikwete wamezivaa, tumemuona makamu wa raisi mstaafu amezivaa, na hata wanajeshi waliobeba jeneza la Maalim wamezivaa?

Huo ushauri wa barakoa za nje kuwa hazifai ni kwa ajili yetu sisi tu malaymen au hata Madaktari wanaotutibia nao waache kuzivaa pindi wawapo theatre?.

Je mheshimiwa raisi pindi akiona madaktari wamevaa barakoa wakati wa kuwatibu wagonjwa kimoyomoyo anawaona kama watu wasio na imani timilifu kwa Mungu ambaye anadhani atawalinda tu bila hata kuvaa hizo barakoa?

Ndiyo maana wananchi mitandaoni wanapendekeza mheshimiwa rais akutanishwe na barokoa ili wamalize tofauti zao.

Wazungu wanasema, We don't have a dog in this fight, kwa maana kwamba ugomvi huu siye wala hautuhusu!

Mheshimiwa raisi, anasema tusiamini barakoa za nje, wakati hizo barakoa zimejaa tele kwenye maduka ya dawa na serikali iishachukua kodi yake kwa walioziagiza, Je vyombo vya uthibiti ubora na forodha havikuwa na taarifa kuwa hizo bidhaa zinaingia nchini?, Kama hilo linajulikanabona hatujaona operesheni ya kufika kwenye maduka hayo kuzikusanya na kuziharibu?

Kwenye ugomvi huu wa mheshiiwa raisi na Barakoa, wananchi tumegoma, tumekataa, hatutaki Sisi hatununui ugomvi binafsi.

Unasema tuchukue tahadhari halafu wakati huohuo unatwambia aulindaye uhai wake ataupoteza!. Mheshimiwa rais unatuconfuse totally!

Mheshimiwa rais kwenye hili jipange wewe na timu yako mje upya, kwa heshima na taadhima kubwa kwa mamlaka uliyonayo napenda kusema kuwa hii double talk ya kudunisha, kudiscredit barakoa wananchi tumeikataa na badala yake tunakushauri umalize tofauti zako na barakoa, na uanze kuivaa ili ujilinde!

Mheshimiwa rais Corona ni hatari jihadhari, wasikilize wataalamu!
 
Kama anasema kuwa tutakufa tu kwa nini yeye amejipiga chanjo and his concubines .
 
Kua uyaone mdogo wangu!
===
Kwa wanaopenda kujua zaidi juu ya nini kiko nyuma ya msukumo wa watu kulazimishwa kuchanjwa kimabavu, karibu kwenye link hii hapa chini ujisomee.


Aisee. Inawezekana Rais anapodai “anayajua mengi” basi ni huku ndiko anakopatia hizo “alternative facts” anazoziamini sana? This is utter trash.

Kama kweli haya ndiyo aina ya maandiko yanayotumika na mkulu katika maamuzi kuhusu masuala muhimu ya kitaifa basi tumepata hasara isiyomithilika. Tusubiri rehema ya Mwenyenzi Mungu tu.
 
Sasa mtu kama huyu anataka Raisi amkalie kimya.

Ujinga tu. Unafanya mambo ya kisiasa kwenye dini,
Raisi akitumia kanisa kuwashambulia nyinyi wenye imani haba mnalalamika eti kachafua madhabahu. Acheni kumchokoza[emoji57][emoji52]
yeye kasema madhabauni kwan??
 
Natamani kumuuliza kwanini ulipokuwa France ulikuwa ukivaa barakoa lakini umerudi nchini huvai? Covid iliyopo France ndiyo hiyo hiyo iliyopo Tanzania kwanini unachezea uhai wako? Unamfurahisha/unamuogopa nani kwa kutovaa barakoa?
Kabudi akirudi atavua barakoa kumfurahisha bosi wake ingawa kwa umri wake yupo kwenye target ya corona virus.
 
Back
Top Bottom