Rais Magufuli aivunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala

Rais Magufuli aivunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala

Tusipotezeane muda na wala tusibishe kwa hili Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli yupo sahihi kwani Ilala ndiyo Dar es Salaam na Tanzania vile vile. Na hata Watoto wa Mjini wote wapo Ilala na siyo Kwingineko ambako kumejaa tu Washamba na Malofa watupu japo wenyewe ( wao ) wanajiona Wajanja.
Mbona huna fact mjomba
 
Yaani Mkazi wa Osterbay, Masaki, Mikocheni na Mbezi Beach wanaishi Manispaa wakati wakazi wa Ulongoni, Gongolamboto, Buguruni kwa Mnyamani, Chanika wako Jiji la Dar[emoji2][emoji2] Tutaelewana tu hata kama itachukua muda ila mwishoni tutaelewana.

Mikumi Sasa siyo Mitano tena.
Hahahahahaha
 
Hamataki mayor wa sasa wa jiji la Dar es salaam sio mtu wa mitandao na mapicha picha kama RC Mpya , inawezekana anataka aweke mtu wake ili wapige ndio Fujo zote hizi za kutualibia Nchi, kama hampendi angemuita wakamlazimisha ajiudhulu sio hizo Fujo jiwe anataka kuleta
 

Attachments

  • D5DF3933-AD75-454A-A802-8EBF6B690390.jpeg
    D5DF3933-AD75-454A-A802-8EBF6B690390.jpeg
    52.4 KB · Views: 1
Hapa nimemuelewa rais alichofanya nikupunguza Gharama za uendeshaji wa iliyokuwa halmashauri ya jiji wakati wanaounda hilo jiji wapo hapahapa ilala ,kinondoni na temeke.
Mkuu una uhakika kwamba uamuzi huu umepunguza gharama ?
 
Binafsi nasema hivi, kama ni kupunguza gharama basi angeongoza hoja ya kubadilisha mfumo wa utawala wa jiji la Dar es Salaam kutoka kuwa chini ya mkoa na kwenda kuwa chini ya meya yaani mayor-council form of government ambapo meya ndiye anakuwa mkuu wa serikali ya jiji na Halmashauri ya jiji.

Nilishawahi kulizungumzia hili huko nyuma. Hii ndiyo njia itakayompa nguvu meya wa jiji la Dar es Salaam na sio kuwa chini ya mkuu wa mkoa kama ilivyo kwa sasa
 
Jiji la daressalaam lilipendeza sana na zile wilaya zake tatu tulizokua tukiziimba tangu tuko shule,
kinondoni, ilala na temeke, kipindi hicho ata uamshwe usingizini uambiwe uchore ramani ya mkoa na wilaya zake unachora,
lilipokuja suala la kuongeza wilaya na hii kuhamisha jiji kwenda wilaya flani ni usumbufu tu kwa wanafunzi
 
Binafsi sioni kama kuna shida yoyote kwa mfano Mbeya ni jiji lakini jiji lenyewe ni pale mbeya mjini yani Mwanjerwa, soko matola, uhindini n.k lakini mkoa wa Mbeya bado una wilaya nyingine ambazo hazipo katika jiji la Mbeya kama Kyela na Chunya

Hivyo mkoa wa Daresalaam kuna wilaya ya Temeke, Kigamboni ,Ilala , kinondoni na Ubungo katika wilaya hizo Ilala ndio yenye hadhi ya Jiji
 
Hivi imekaakaa je Ilala ndo Dar jiji na hizi halmashauri nyingine zitakuwa ndani ya mkoa wa Dar sio? Kwa hiyo ukivuka Salenda au Jangwani unaingia kwa jiji la Dar. Hiiii
 
Tusipotezeane muda na wala tusibishe kwa hili Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli yupo sahihi kwani Ilala ndiyo Dar es Salaam na Tanzania vile vile. Na hata Watoto wa Mjini wote wapo Ilala na siyo Kwingineko ambako kumejaa tu Washamba na Malofa watupu japo wenyewe ( wao ) wanajiona Wajanja.
Kwa vile upo ilala au
 
Back
Top Bottom