Ni lazima nimpongeze Raisi Magufuli kwa kukutana na upinzani na kuwasikiliza. Nashukuru kwa washauri wa hili ambao wamemwambia ukweli.
Nilishasema na kuandika huko nyuma faida ya kuwanyima uhuru upinzani hautasaidia CCM wala taifa. Tunavyoongea leo hii pamoja na migawanyiko ambayo haina maana tulikosa $550M kwa sababu ya uchaguzi wa Zanzibar, tumezuiwa kusafiri kwa nchi nyingine, na nimesikia kula list mpya yenye majina ya viongozi ambao wanaingia kwenye list ya Makonda aliyopewa na US lakini inasubiri uchaguzi tu kama hautakuwa wa haki list hii itaongezeka kwa viongozi na familia zao.
Lakini vilevile nina wasiwasi shughuli nyingine za maendeleo.
Ujumbe wa Magufuli unatakiwa uwekwe wazi kwa watendaji ambao ni wafaidi wakubwa wa kugombana CCM na vyama vya upinzani.
Hebu angalieni Mkuu wa Wilaya ya Hai hata siku moja hatujasikia anaongelea kusaidia utalii pake KIA na kuhimizwa ujenzi wa hoteli kwa wasafiri badala yake na majungu kwa mbowe sasa hii inasaidia vipi nchi? lakini kwa ujinga huu hafukuzwi kwasababu za kisiasa!.