Rais Magufuli ameamua nchi ifungue sura mpya ya kimaendeleo kuelekea 2025

Kama wewe mjanja kwanini utumie fake ID kumuogopa MSHAMBA?Kwanza inakuaje unaongozwa na MSHAMBA?

Sent using Jamii Forums mobile app

Wapi nimemuita mshamba, au unadhani mimi ni bendera fuata upepo kama ww? Nimejiunga 2011 hapa jf, alikuwa kashakuwa mkulu mpaka useme najificha? Ww unayemsifia mbona unatumia fake I'd pia, je unaogopa nini? Kama huna hoja piga kimya boss.
 
Hela ya Mloganzila na SGR katafuta nani?Mradi wa REA ungekufa, lawama zingekua kwake ila umefanikiwa sifa ni kwa Jk. Huoni unashida ya akili sehemu?Unataka kusema mradi wenye timeframe ya miaka 5,pesa tayari zinakua zimetengwa na kilichobaki ni kutekeleza tu?Kama jibu ni ndio,hii miradi inayokua inakwama au kusuasua shida huwa nini ukitoa mattz ya mkandarasi?Kama jibu ni HAPANA, Huoni utawala unaokuwepo huwa na mkono wake ktk huo mradi?

JK SGR alimpa mchina, kaja JPM kabadili na kumpa mturuki lkn bado mtu anakuja anasema SGR ni juhudi za JK hahahahahahah. Chuki zikikujaa ni shida sana.Kama kaweza kupiga chini mradi wa Bagamoyo ulioanzishwa na JK alishindwa vipi kupiga chini miradi yote ya Jk aliyoikuta?Kizuri ni JK ila kibaya ni JPM. Mradi wa Bagamoyo umekwama lawama zote ni JPM ila ungefanikiwa sifa angepewa JK hahahahahahah.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya yataendelea kuwa mwiba kwa majuha wa kitanzania wenye chuki binafsi na mpendwa rais wetu Magu na serikali yetu!
 
Mtanzania wewe umesema vema,lakini napata maswali magumu kweli mnapofafanua haya mambo.

1.Umeme wa REA ulipaswa kupigwa chini baada ya kukosekana fedha za WB 2016,kwanini tunakopa hizo pesa wakati tayari kwa kitambo kirefu kulikuwa na tozo kwenye mafuta na umeme kwa ajili ya kukamilisha hiyo miradi?

2.Ujenzi wa bandari bagamoyo,uliafikiwa na serikali ya awamu ya nne,na kutengewa bajeti kuoitia bunge la JMT, na Mh.JPM alikuwa waziri wa ujenzi alisimamia ujenzi wa bandari hiyo hiyo, Ni nini kimefanya mradi aliousimamia kupigwa chini?(ametoa sababu kadhaa zilizipelekea kutupiliwa mbali kwa mradi ambazo nyingi zimeelekezwa kwenye MKATABA, swali ni je,wakati wa kuupitisha mradi huo yeye akiwa waziri,hakuona mkataba?)

3.Kila serikali kuja na mradi wake, ni swala lenye ukakasi,ni muhimu kuzingatia mipango mikakati ya kitaifa katika kuifanya nchi iendelee, lakini tukiangalia moango wa maendeleo ya uzalishaji nishati nchini STIEGLER'S GORGE haikuwepo kabisa,tulikuwa na mkakati mkubwa wa kuzalisha umeme utokanao na gesi,tukaamua kujenga bomba la kusafirishia gesi kutoka Mtwara kuja Dsm,tuliweka pesa nyingi kukamilisha mradi ule,watu waliumizwa sana kuhakikisha hilo linakamilika,lakini leo tumeanzisha mradi mpya kwa gharama mpya,pasipo kuelezwa gharama za mradi wa ujenzi wa bomba ni sh.ngapi, na zitarudishwaje?

4.Mradi huu wa umeme wa maji (stiegler's),kama nakosea naomba nirekebishwe,kwamba utafikia kilele cha uzalishaji wa MW 2150 itakapofika mwaka 2036, je,baaday ya 2020 au 2025 akiondoka JPM,mradi huu utaendelea kutekelezwa mpaka kufikia kilele cha uzalishaji? Au atakayefuata baada yake atakuja na mipango mingine kutuacha tuendelee kulipa deni la mradi uliozimika kama tunavyolipa deni la ujenzi wa bomba la gesi?

5.Fact zote za kusitishwa kwa baadhi ya miradi mikubwa imejengwa katika misingi ya MIKATABA, je, mikataba ya inayosainiwa sasa kama vile ununuzi wa ndege,ujenzi wa reli,Stiegler's gorge HPP tunaijua? Haitaleta taabu tena baadaye? Au tunapaswa kusubiri aondoke kwanza madarakani ndipo tuje tuambiwe udhaifu wa mikataba hiyo na atakayechukua nafasi kwa wakati huo?

Naomba kumalizia kwa kusema,katika kipengele cha mikataba pana mapungufu makubwa ambayo tukiendelea kuifuga itaendelwa kututia umasikini kwa miongo mingi sana ijayo.
 
Waambie Comrade nchi ilikuwa mikononi mwa wajanja wachache wao ndio wamuaji na wanufaikaji wa rasirimali za Taifa Leo hali imebadirika Taifa letu limesimama katika misingi yake
Fahami Matsawili tuheshimu kazi za wengine,unataka kusema enzi za Jk wajanja wachache ndo walikuwa wanaamua? ( any way nikubaliane na wewe kwa hilo) unaweza kutuambia hapa kwamba kwa sasa nchi ipo mikononi mwa wengi?

Unaweza kusema hapa bajeti ya ununuzi wa ndege ilipitishwa na nani? Ujenzi wa kiwanja cha ndege chato ulipitia mchakato unaelekezwa na sheria?

Uamuzi wa kusitisha upandishwaji wa mishahara ya wafanyakazi kwa miaka 4 uliamuliwa na nani?(haijalishi ni kwa nia njema au lah)

Mfumo wetu haujabadilika,bado wanaoamua matumuzi ya rasilimali za taifa ni wachache,usituaminishe kwamba kuna tofauti kati ya tawala zilizopita na huu wa sasa,mfumo wa matumizi ya rasilimali za taifa bado upo mikononi mwa wachache,tena kwa sasa inaweza kuwa mbaya zaidi kwa kuwa baadhi ya miradi fedha zake hata bunge haliidhishi bajeti zake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…