Rais Magufuli ameguswa na nini hadi kuwakemea waendesha mashtaka kwa kuchelewesha upelelezi kwa watuhumiwa wanaoozea jela?

K
Walijipendekeza sana kwa mheshimiwa Rais Magufuli lakini ameshtuka the same as Kangi Lugola case

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna msemo unaosema mwisho wa ubaya aibu

Hiyo ni *wake up call" ameitoa Mheshimiwa Rais, nanyi Jeshi la Polisi inabidi mjitathmini
 
Tuna Rais anayejali mno wananhi.
Pongezi kwa Rais kuona hilo, kwa hakika lilikuwa kikwazo kikubwa kwa upatikanaji wa haki za watuhumiwa kwa wakati.
Yaani serikali inabambikizia watu kesi za utakatishaji hadi wa 500,000 halafu hiyo hiyo inajilaumu halafu wenye Stroke ya akili kama wewe mnakuja kusifu na kuabudu mbambikizaji?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwan siku ile anamsema Sirro kuhusu kutekwa kwa MO we ulielewa nini tuanzie hapo kwanza.
Mkuu Shark mimi nilielewa kuwa Jiwe ni muigizaji wa kiwango cha hali ya juu sana!
 
Nae anahojiwa na wakubwa wa dunia,ni kwanini watu wanaozea gerezani?

So inabidi nae ajikoshe tu.

dodge
 

Sanaa tu anajisafisha
 
Nimependezwa na jinsi aliwaonya jamaa wa mabaraza ya ardhi.

Yani waziri wa ardhi inabidi hili swala alichukue kama mojawapo ya hadidu za rejea na kufanyia kazi.

Kuna shida kule.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee akijamba kwenye kadamnasi.ya watu lazima usingiziwe wewe mtoto uliyepo.karibu na wewe unyamaze tu
 
Niliona baada ya kutamka meza kuu alipo CJ na wenzake, waliangaliana na body language yao ilikuwa inasema kwa uwazi kabisa. Tapeli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ameguswa na kesi ya masheikh wa Zanzibar ambao wapo ndani zaidi ya miaka mitano wapelelezi wakiwa mbiyoni kukamilisha upelelezi.
 
Rais aagize vyombo hivi visikamate mtu bila kuwa na ushahidi..kuna kesi nyingi mno zinalalamikiwa kwamba zinakomoa..kuumiza na kutesa..ni ukweli kwamba unapokamata mtu ana familia unasambaza yale mateso kwa ndg jamaa na familia yake.Jambo linaloleta hali ngumu.Matokeo yake kweli ni laaana .
 
Well said Mkuu Somoche

Ulichoongea kina mantiki ya hali ya juu sana, kuwa hawa mapolisi wasimpeleke mtu mahakamani huku wakijua upande wa ushahidi bado hawajakamilisha ushahidi wao

Hebu imagine kesi ya Erick Kabendera, hivi sasa inaingia mwezi wa 8 na kila wanapoileta mahakamani wanadai kuwa ushahidi haujakamilika!

Unawezaje kuchukia zaidi ya miezi 8 kutafuta tu ushahidi?
 
Mkuu tambua tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu, pia ukiona nyani anamkana na kumtupa mwanaye ujue hali ya usalama Wa maisha yake uko matatani anaamua kujinasua mwenyew na kumtupa mwanaye.

Siasa bila unafiki haiwezi kwenda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kukemea peke yake haisaidii,hilo suala amelizungumza raisi wa TLS kwenye maadhimisho ya wiki ya sheria,sasa kama ameishia tu kusema walaaniwe ndio suluhisho au ndio majibu?
Mfumo wa kisheria uangaliwe upya.

Alichosema raisi wa TLS:

'' Ibara ya 14 ya Katiba ya Nchi yetu inatoa haki ya kuishi na “kupata kutoka kwa jamii hifadhi ya maisha yake kwa mujibu wa sheria”. Aidha, Ibara ya 15 (1) inasema “Kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu huru.” Ibara ya 15(2) inataka mtu asishikwe na kuwekwa ndani au kuhamishwa kwa nguvu na kupoteza uhuru wake isipokuwa mujibu wa sheria na pindi mtu anapokuwa ametiwa hatiani. Ili kukidhi matakwa haya inabidi polisi na waendesha mashitaka kujiridhisha kuwa pale wanatoa tu amri ya kushikwa na kuwekwa ndani pale upelelezi unakuwa umekamilika. Aidha, haki ya kupata dhamana iheshimike. Ni vema pia uamuzi wa Mahakama ya Rufani katika kesi ya Attorney General v. Jeremiah Mtobesya Civil Appeal No 65 of 2016 ambapo ilisema kuwa kipengele kinachompa madaraka Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali kuweka cheti cha kuzuia dhamana hata kwa makosa yanayodhaminika ni kinyume cha katiba ya nchi yetu. Tulitegemea kuwa kutokana na uamuzi huo sheria zote zinazotoa mamlaka hayo zingebadilishwa lakini sivyo ilivyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…