Rais Magufuli ameguswa na nini hadi kuwakemea waendesha mashtaka kwa kuchelewesha upelelezi kwa watuhumiwa wanaoozea jela?

Rais Magufuli ameguswa na nini hadi kuwakemea waendesha mashtaka kwa kuchelewesha upelelezi kwa watuhumiwa wanaoozea jela?

Hata home mzazi ukiona watoto wanakuja juu kwa hoja nzito - unakunja ndita kutishia ujio wa hoja yoyote ile juu yako...ni moja technique tu za uongozi wa kibabe - hizi hawafundishi kwenye Principals of management..ni wewe tu kujiongeza.
 
Kwahiyo akiwafuta kazi hao uliowataja ndio kesi zitawahishwa na au kuisha mapema?
Huenda ikawa dawa kwa watakaoteuliwa kuzingatia maadili ya kazi zao na kuizingatia katiba kama Sheria mama na au kutoruhusu siasa kuingilia vyombo ya dola na mahakama!
 
Kama kichwa changu cha habari kinavyouliza hivi Rais Magufuli "ameguswa" na nini hadi awakenee waendesha mashtaka wanaochelewesha upelelezi wa kesi zilizoko mahakamani, jambo linalosababisha watuhumiwa wengi kuendelea kupata mateso ya hali ya juu, kwa kuendelea kusota rumande kwa kipindi kirefu sana?

Tunajua kuwa wapo watuhumiwa wengi ambao wako mahabusu kwa kesi za kubambika za utakatishaji pesa, ambazo wao waendesha mashitaka wanajua kuwa hazina dhamana, hivyo kuzitumia kama "fimbo" ya kuwatesea watuhumiwa hao ambao hawana hatia.

Hebu tujaribu ku-imagine kwa mfano kesi ya mwandishi wa habari Erick Kabendera, huu ni mwezi wa 8, kila kesi hiyo inapotajwa hapo mahakamani, waendesha mashitaka hao, wanadai kuwa upelelezi hawajaukamilisha!

Hivi inawezekanaje kwa Polisi kupeleka kesi mahakamani, tena ya utakatishaji pesa, wakati upelelezi bado haukakamilika?

Hivi hiyo siyo njia tu ya kuwakomoa watuhumiwa hao wa utakatishaji pesa, kwa vile hao Polisi wanajua kuwa kesi hizo hazina dhamana?

Sasa Rais Magufuli amesema walaaniwe waendesha mashitaka hao, wanaosababisha mateso makubwa kwa watuhumiwa, kwa kuendelea "kuwasotesha" rumande.

Hata kama kwa mawazo ya wengi kuwa walidhani kuwa Jiwe ndiye "mastermind" wa kesi hizo, sasa keshawaruka futi 10,000.

Kwa hiyo kazi kwenu zigo lote la ubaya kawabakizia nyinyi Polisi waendesha mashitaka na akahitimisha kwa kusema mlaaniwe kwa kuwabambikizia kesi hizo za utakatishaji pesa mkiwa na lengo la "kuwakomoa" watuhumiwa hao ili waozee jela!

Nami niongezee kwa kumwomba Mungu wetu ili awalaani na kuwatia "uzezeta" hao Polisi wote wanaowabambikia kesi za utakatishaji pesa watuhumiwa kwa lengo tu la kuwasotesha kwa kipindi kirefu, watuhumiwa hao wasio na hatia.
Kati ya wale mawakili/ mahakimu watakao kwenda motono Magu yumo.. Akiwa kama mkuu wa nchi ana paswa kukemea hizi kesi za kubambikiza lskini yuko kimya. Sasa nani achomwe wa kwanza?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
POLICE anakubambikia mashtaka, -- Kumfurahisha boss. mwendesha mashtaka anapinga dhamana hata kama kosa lina dhamana -na kuchelewesha kesi kuwa upelelezi haujakamilika ---Kumfurahisha boss-- -. HAKIMU anakubaliana na polisi na mwendesha mashtaka -- Kumfurahisha boss . BOSSS NI NANI ???
JUSTICE DELAYED IS JUSTICE DENIED
 
POLICE anakubambikia mashtaka, -- Kumfurahisha boss. mwendesha mashtaka anapinga dhamana hata kama kosa lina dhamana -na kuchelewesha kesi kuwa upelelezi haujakamilika ---Kumfurahisha boss-- -. HAKIMU anakubaliana na polisi na mwendesha mashtaka -- Kumfurahisha boss . BOSSS NI NANI ???
JUSTICE DELAYED IS JUSTICE DENIED
Well said Mkuu viking

Hivi kwa uzoefu wako ndani ya utawala huu wa awamu ya tano, atawezaje kuliongelea suala hilo ambalo ni very serious issue, halafu IGP aendekee na kazi?

Kama hayo siyo maigizo ya dizaini ya Futuhi
 
Back
Top Bottom