Rais Magufuli amnyooshea kidole Mwele Malecela asema alitumiwa na mabeberu kutangaza ugonjwa 'hewa' wa Zika

alexelias

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2017
Posts
2,032
Reaction score
3,197
Akielezea ni kwa namna gani humpelekea kufanya kazi hadi usiku Rais Magufuli amesema katika vita hasa ya kiuchumi adui mbaya zaidi hutoka ndani kwa maana ndiye huwa kiungo wa maadui wa nje.

Ametolea mfano wa aliyekuwa Mkurugenzi wa NIMR TANZANIA Bi Mwele Malecela alilazimika kumfuta kazi baada ya yeye kutoa taarifa za uongo kwamba wakati ule kulikuwa na ugonjwa wa Zika ilhali haikuwa kweli.'Je huo ugonjwa wa Zika ulionekana tena!?'alihoji Mheshimiwa Rais!

Amesema hali hiyo ya Mwele kuutangazia uongo Ulimwengu kuhusu uwepo wa zika Nchini Tanzania ilimkwaza sana na dhahili alionekana kutumiwa na washindani wa vita ya kiuchumi na Nchi yetu.

'Na ndiyo maana baada ya kumfuta kazi wiki moja baadae waliomtumia walimpa kibarua kingine'alisema Mheshimiwa Rais.
 
Hivi Tanzania mamlaka huwa zinafanyaje kazi?

Mathalani kama kuna mlipuko wa ugonjwa mkubwa kama Zika, si kwamba kabla ya kujulikana kwa wananchi Rais inabidi afahamishwe na waziri husika?

Ilikuaje Mwele kutangaza tamko kubwa kama lile pasipo kuwa na backup ya waziri wake?
 
Bado ana chuki na yule mtoto masikini! Mungu atamlaani Jiwe


Sijui dr Mwele alimkosea nn mh Raisi?! Dr Mwele atumwe na mabeberu ili iweje ? Kwa uchumi upi tulionao adi hao mabeberu waweke vita na Tanzania? 😰😰

Hisije ikawa Lemutuz alimfitinisha dada yake wa kufikia kwa Mh Raisi kwa kupitia Bashite

Lemutuz na watoto halali wa Malecela hawaelewani kwa Sababu ya tabia zake
 
Yule Mwele kwa hakika alitumiwa.
 
Mzee ana chuki na kila mtu, kumfuta kazi kwake ndo alitegemea na Mungu afute ridhiki yake ama,yaan utadhani yeye ndo mtoa ridhiki
 

Mbona naona kama huyu Mzee anataka kuleta hatari ktk nchi??

Ee Mungu tunusuru waja wako na jaribu hili, kila siku kuzungumzia kuhusu visasi badala ya maendeleo!!??? Daaah, hii ni hatari sana.
 
No, please, serology ilionyesha kuwa kuna antibodies against Zika virus! Means kuna infection .. au positive serology had a history of exposure to Zika, sijui kama umesoma immunobiology
Kwa nini Mwele hakufuata utaratibu wa kawaida wa kumuarifu Waziri wa afya kabla hajatoa lile tamko!?
 
Hivi hii vita ya kiuchumi tunapambana na nani hasa?
Kama hata hao mliotangaza kwa mbwembwe wahujumu uchumi unaamrisha DPP awasamehe?
 
Nashauri UDSM muifute Phd fake ya huyu jamaa, akiongea hana tofauti na wanywaji wa mataptapu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…