Rais Magufuli amuapisha Jaji Zephrine Galeba kuwa jaji wa mahakama ya Rufaa

Rais Magufuli amuapisha Jaji Zephrine Galeba kuwa jaji wa mahakama ya Rufaa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Jaji wa Mahakama Kuu wa Kanda ya Musoma, Zephrine Galeba alietuliwa kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Rufaa kutokana na kuandika Kiswahili katika moja ya hukumu alizowahi kuzitoa.

Leo Rais Magufuli anamuapisha rasmi Dodoma, kuwa nami kukujuza yanayojiri.

===
10:22 Asubuhi: Jaji Galeba anatia saini kwenye viapo vyake

Jaji Zephrine Galeba: Mheshimiwa Rais, leo ni siku kubwa sana kwangu na familia yangu. Ni jambo la kumshukuru Mungu sana kwa kutujaalia kutuumba sisi kama viumbe wa daraja la juu lakini pia kututunuku uhai.

Mheshimiwa pia kwa unyenyekevu mkubwa na wa kipekee sana, nakushukuru sana kwa dhati ya moyo wangu kwa kuniheshimisha kunipa nafasi ya juu katika mahakama. Mimi sina maneno ya kueleza namna ambavyo nimepokea hii nafasi labda niseme tu kwa ufupi kwamba, nakuahidi kutumikia wananchi wa nchi hii kwa kutenda haki vile ambavyo Mungu anataka tutende haki huku duniani.

MWIGULU NCHEMBA: SHERIA INASEMA LUGHA YA SHERIA NA MAHAKAMA IWE NI KIINGEREZA
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Sheria iliyoko sasa imeelekeza kuwa lugha ya sheria na lugha ya Mahakama iwe ni kiingereza.

Kwa kuwa sasa kiswahili kinabidi kutumika kwa kuwa wanaoandika ni watu wanaofahamu kiswahili na wanaoandikiwa ni waswahili basi wameongea na Mwanasheria Mkuu ili kuangalia namna ya kubadili vipengele hivyo.

Dkt. Nchemba amempongeza Rais Magufuli kwa hotuba yake kuhusu Sheria na Kiswahili aliyoitoa siku ya maadhimisho ya miaka 100 ya mahakama nchini Tanzania.

Ameyasema hayo katika hafla ya kumuapisha Jaji Zephrine Galeba ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa jijini Dodoma.

RAIS MAGUFULI: KISWAHILI KINA MSAMIATI WA KUTOSHA

Rais Magufuli amesema kuna baadhi ya watu huwa wanakosoa juhudi za Kiswahili kutumika wakidai kuwa kina uhaba wa msamiati

Amesema hoja hiyo haina mashiko kwa kuwa Kiswahili kina msamiati ya kutosha ndio maana kinatumika hata kwenye baadhi ya taasisi za kimataifa na vyomb vya habari vya kimataifa kama BBC na DW

Pia amesema Kiswahili ni lugha ya 10 kwa kuzungumzwa duniani, akisisitiza kuwa hata kama wakisema lugha haina msamiati wa kutosha, wataje lugha moja ambayo imejitosheleza kwa msamiati

Rais amesema kutumia Kiswahili katika hukumu yatakuwa ni mapinduzi makubwa

====
RAIS MAGUFULI: NIMEMTEUA JAJI GALEBA MAKUSUDI ILI AKAENDELEZE KISWAHILI

Rais Magufuli amesema aliamua kumtunuku Jaji Zepharine Galeba Ujaji wa Mahakama ya Rufaa kutokana na uthubutu na ujasiri aliouonesha kwa kutumia lugha ya Kiswahili katika kuandika hukumu

Amesema “Ninajua hata kwenye Mahakama Kuu alikuwa ‘very junior’ ni Kijana na inawezekana wale nguli wa Mahakama Kuu Majaji wanajiuliza kwanini Kijana huyu amechaguliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa”

Amefafanua “Nimemteua makusudi ili Kiswahili akakiendeleze kwa Majaji wa Mahakama ya Rufaa. Ili hiki kilichomsaidia kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa asikiachie huko kikawa tu kisingizio cha kupatia kazi, akawe chachu ya Kiswahili kuanza kutumika.”

Aidha, amesema tumeshindwa kutumia Kiswahili Mahakamani kwa kukosa utashi na ujasiri na pia ni ishara ya kuendelea kwa kasumba ya kuendelea kupenda vitu vya nje na kudharau vya kwetu
 
Hope taratibu zote muhimu kuanzia vetting, uteuzi, na uapishaji zitakuwa zimezingatiwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Tumtakie utumishi uliotukuka mtukufu Jaji.
 
Jaji wa Mahakama Kuu wa Kanda ya Musoma, Zephrine Galeba alietuliwa kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Rufaa kutokana na kuandika Kiswahili katika moja ya hukumu alizowahi kuzitoa.
...
... edit hapo Chief! Tunaye Jaji Mkuu mmoja tu! Next ni Jaji Kiongozi then majaji wengine kwa seniority zao kuanzia wale wa Mahakama ya Rufaa.
 
Kuna mtu anasisitiza matumizi ya lugha ya kiswahili lakini wakati huo huo na yeye anatumia maneno ya kiingereza! Challenge, AG, Amendment, East Africa Community, cut and paste, communication, very frustrating, appeal,imagine
 
Kuna mtu anasisitiza matumizi ya lugha ya kiswahili lakini wakati huo huo na yeye anatumia maneno ya kiingereza! Challenge, AG, Amendment, East Africa Community, cut and paste, communication, very frustrating, appeal,imagine
 
Ni matumaini yetu kuwa maagizo aliyo yatoa mhe. Rais kwa Waziri wa Katiba na sheria pamoja na Bunge kufanya marekebisho ya sheria inayo kikwaza kiswahili kutumika kufanya marekebisho ktk bunge hili mara moja kwa masilahi ya watanzania wote.

watanzania tulio wengi tunatamani kuona utaratibu huu unaanza kutumika mara moja bila kuchelewa.
Hongera kwa Jaji aliye apishwa, kikubwa tenda haki usionee walio chini wala usikubali majungu na fitina.chapa kazi kwa masilahi ya wananchi na kwa kumtanguliza Mungu mbele.
 
Watanzania tuzidi Sana kumuombea Mheshimiwa Rais Magufuli,! Tamko lake la kuiomba Idara ya Mahakama kwamba Kesi zote , na kwa ngazi zote za Mahakama ziendeshwe kwa lugha ya Kiswahili na Hukumu kuandikwa Kiswahili , Watanzania tumuunge mkono Mheshimiwa Magufuli na kumpongeza Sana !
 
Watanzania tuzidi Sana kumuombea Mheshimiwa Rais Magufuli,! Tamko lake la kuiomba Idara ya Mahakama kwamba Kesi zote , na kwa ngazi zote za Mahakama ziendeshwe kwa lugha ya Kiswahili na Hukumu kuandikwa Kiswahili , Watanzania tumuunge mkono Mheshimiwa Magufuli na kumpongeza Sana !
Huwa zimaendeshwa kwa Kiswahili but...
records ndio zinawekwa kwa kingereza
 
Jambo jema... ila mbona kwenye katiba mwatumia ile ya mkoloni, pamba masikio kilio cha wananchi hakisiki.. au kwakuwa ina maslahi kwenu
 
... kumbe mteuliwa alivunja sheria kwa kuandika hukumu kwa lugha iliyokatazwa na sheria?
Nchi hii imepatiwa Mwendawazimu. Yaani mtu ukitaka cheo vunja sheria?? Sheria na Miongozo ziliwekwa kwajili gani?

Siku hizi nitaanza ukorofi wa kutotii sheria bila shuruti. Trafik akinipiga mkono hakuna kusimama. Wakifanikiwa kunidaka basi nitajitetea kuwa nilikuwa namuwahisha wife Ofisini kwake akawahudumie wateja.
 
Yaani sababu ya uteuzi ni kuendeleza kiswahili. Wapeleke chuo akafundishe sheria kwa kiswahili.
 
Naona katika ukaaji walizingatia distance pia kwenye kusalimiana wamezingatia kutoshikana mikono.
 
... kumbe mteuliwa alivunja sheria kwa kuandika hukumu kwa lugha iliyokatazwa na sheria?
Labour Court kitengo cha mahakama ya kazi sheria yake inaruhusu kiswahili au kiingereza ila vitengo vingine vya mahakama kuu lugha ya maandishi sheria imeelekeza kiingereza tu. Hivyo alifuata sheria hakuvunja.
 
"#1
Jaji wa Mahakama Kuu wa Kanda ya Musoma, Zephrine Galeba alietuliwa kuwa Jaji Mkuu wa Mahakama ya Rufaa kutokana na kuandika Kiswahili katika moja ya hukumu alizowahi kuzitoa."



Hakuna cheo cha "Jaji Mkuu wa Mahakama ya Rufaa"

Jaji Mkuu ni mmoja na ndiye Kiongozi Mkuu wa Mahakama zote.
 
Mheshimiwa Raisi sio mpenzi kabisa wa mfumo wa seniority katika vyombo mbalimbali vya serikali..
 
Kutumia Kiswahili kwenye hukumu na sheria, itakuwa faida kwa wananchi, ila itaathiri mapato ya Mawakili na Wanasheria.

Ugumu wa lugha ya kisheria (legal language) ni moja ya sababu ya wananchi kuwahitaji Wanasheria.

Sasa sheria zikiwa kwa Kiswahili, kila mwananchi atazielewa, halafu Mawakili na Wanasheria watakosa kazi.

Siri ya kazi itafichuka soon!
 
Back
Top Bottom