Rais Magufuli awachana Kilwa kwa kumchagua mpinzani Bwege. Awataka kutofanya makosa tena uchaguzi ujao

Magu akiongea huwa hana makosa lakini wapinzani wakisema maneno kama haya wataswekwa ndani. Mkuu wa nchi hana nidhamu na heshima kwa viongozi wengine. Hii ni shida na watanzania tuamke. Kampeni za kujenga barabara na stendi zimetwa na wakati sababau baada ya miaka 58 wa UHURU wa Tanganyika mambo hayo yanatakiwa kuwa na mamlaka yake.Leo tuna kampeni ya kuchimba visima wakati wizara ya maji ipo. Tunaongelea habari ya umeme wakati ipo wizara husika. Huu ni ujinga na watanzania bado wapo usingizini.
 
Navyojua Tiss wapo kwa ajili ya watu wanaotishia amani ya nchi!
Kwanini safari hi wako kimya?.
 
Baada ya maneno hayo utasikia maendeleo hayana vyama!

I mean, sijui watu washike lipi
 
Ungekuwa wewe ungefanyaje, kama upinzani unazuia kazi.zinazofanya na CCM kwamba watazidi kung'ara katika majimbo hayo wewe ufanyeje? Si unawaacha wafurahie matunda ya uchaguzi wao?
 
Kuongoza wajinga Kuna Raha yake
 
Ungekuwa wewe ungefanyaje, kama upinzani unazuia kazi.zinazofanya na CCM kwamba watazidi kung'ara katika majimbo hayo wewe ufanyeje? Si unawaacha wafurahie matunda ya uchaguzi wao?
Ebu hakikisha usemi wako kuwa upinzani unazuia kazi.
 
Mbunge anaitwa Bwege ,hajafanya chochote mpk leo.mnataka Rais afanyeje ?
Akasimamie wahandisi kujenga stendi
Hapa Eclat sikuelewagi
Acheni kutetea upuuzi, hii ni chuki ya wazi na ubaguzi! Huko kilosa JPM alitumia kauli hizi hizi akijua jimbo ni la upinzani, alipokuja kujua ni la CCM aliona aibu na kupotezea kiaina! Rais wa hovyo kabisa,Bwege kampa anachostahili mropokaji huyu!
 
Kweli bwege Ni full comedian,..sijui alishindaje kwenye uchaguzi...wana kilwa mna maswali ya kujibu
 
Ungekuwa wewe ungefanyaje, kama upinzani unazuia kazi.zinazofanya na CCM kwamba watazidi kung'ara katika majimbo hayo wewe ufanyeje? Si unawaacha wafurahie matunda ya uchaguzi wao?
Una akili kweli? Unajua kikao cha maamuzi kwenye halmashauri kina wajumbe gani? Msiwe mazezeta kiasi hicho kutetea upuuzi!
 
Sijui Mama yake kajisikiaje, huyu mzee busara zake ni zero kabisa
 
Hili jambo linaanza kuota mizizi na si la kufurahiwa na mpenda maendeleo yoyote.Hii si mara ya kwanza Riasi kuonyesha kukerwa kwake na majimbo yanayoongozwa na upinzani,alikosea Kilosa akiamini jimbo la Prof Jay aliposhtuliwa akabadili gia papo kwa pao na juzi tena karudia.
 
Hatari Sana ktk mfumo wa vyama vingi.
 
Amesema kwasbbu wakikosea anaweza kuwaajibisha ndani ya chama. Sasa hao wa Vyama vingine anawezaje? Hiyo ndo concept yake
Je ni wajibu wa chama kuleta maendeleo? Je "upinzani" wakijibu kauli za aina hiyo WATAWALA WATAWEZA KUUVUMILIA HUO "UTANI" WA KISIASA?
 
Mbona wanaccm tunaowajua hawapo kama yeye ?
Mkuu sifa kuu ya kuwa Ccm ni ubaguzi "ndani na nje ya chama" Kwanini huwa kuna kauli "huyu anatumiwa... huyu si mwenzetu... huyu mdini... WADHANI YANAKUJA PASIPO SABABU?
 
Naomba kujua hali ya Jimbo la Ndugai spika wa bunge na kada sugu wa CCM wanakula bata sana huko?
 
Naomba kujua hali ya Jimbo la Ndugai spika wa bunge na kada sugu wa CCM wanakula bata sana huko?
Yapo majimbo mengi ya CCM hayana maendeleo kabsa hata chato haikuwa na maendeleo mpaka alipoingia ikulu akachukua pesa za Rufiji kwenda kujenga chato Airport na maendeleo mengine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…