Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Shida tume.. Hata kura za wapinzani humpa yeye.. Ndio maana ana kiburi..Dawa wamnyime kura yeye,atoke.tumechoshwa na chuki
Mbona kuna majimbo wapo wabunge wa ccm lakini hali ni mbaya tuILANI ya ccm inatekelezwa na wana CCM,,, ukimchagua mbunge wa chama cha Jahazi Asilia au Tadea basi atatekeleza ILANI ya chama chake
Tafsiri pitofu. Magu ana roho mbaya. Halafu ana jificha nyuma ya kivuli cha kumuomba Mungu. Wakati Mungu hadhihakiwi. Awaukize watumishi wa Mungu maana hata kwenye huu msiba wa Ben haja jifunza kituKwa maneno ya Rais Magufuli andai kama Bwege angekuwa CCM angemfukuza uwanachama ana uwezo wa kumuadabisha.Lakini kwa sasa hawezi walimalize wao wenyewe.
Hainaga ubishi
Ingekuwa hivyo wabubge weng n ccm mbona hali n mbaya achen hozo
Ushanipa na chama tayari mkuu?Jiwe ni mbaguzi, ana roho mbaya na katili! Acha kujifanya mjuaji mwenyekiti wako ndivyo alivyo! Hafai huyu mtu
Kwa wanaccm na mwenyekiti wao kampeni zimeshaanza.nauliza tu ,ivi kampeni tayari?
Nguvu na ubabe mwingiJiwe alikuwa na dhamira njema kabisa ya kurudisha chama cha CCM kama ikivyokuwa zamani,kupendwa na wanachi ila anakosea approach zake za kufanikisha nia yake.
Amen to thatDawa ni kupiga spana asirudi tena, au miujiza itokee tu spana toka juu.
Nilishangaa sanaa hili...hasa pale aliposema jogoo hoyeeee
😂😂😂Nilishangaa sanaa hili...hasa pale aliposema jogoo hoyeeee
Wagombea wote wasiojielewa wapigwe spanaNadhani ameishajua hatarudi, ndo maana amepaniki
Wakuu, MAENDELEO HAYANA CHAMA
Rais Magufuli akiwa safarini kutoka Mtwara, ameombwa na mwanakijiji Jimbo la Kilwa kwamba hawana Stendi ya Magari hivyo anaomba wajengewe. Rais Magufuli amejibu kwamba siku nyingine waangalie wawakilishi wanaowachagua ili waweze kufanya vile yeye anavyowaagiza. Mbunge wa jimbo hili aliyemaliza muda wake ni Seleman Bungara aka Bwege Mzee wa ''Umesikia Wapi'' ambaye alikuwa anatokea chama cha wananchi CUF Habari
Rais amezidi kusema kwamba miradi kama hiyo ni ya wabunge na Madiwani ndiyo wanapaswa kuisimamia hivyo kuwataka wabaki na Bwege wao
Rais Magufuli amesema haya...
Nilikuja hapa nikasema nichagulieni watu nitakaokuwa nawaagiza wanafanya ninayoyataka mkasema hapana, Mkamchagua Bwege basi shauri yenu na bwege wenu mwambie awatengenezee stendi
Kazi ya Stendi ni ya madiwani, wabunge. Ukikosea kuchagua, nafuu ukosee kuoa au kuolewa. Ukikosea kuchagua ni tatizo kubwa.
Na hili ndugu zangu niwaombe, muwe waangalifu katika kuchagua. Mchague watu ambao watakuwa kwa ajili ya watu masikini.
Tunatuma hapa fedha za road fund, tunatuma fedha hapa za halmashauri, zimeshindwa kweli kujenga stendi?
Lakini kwa sababu mnanichagulia, wao wenyewe mastendi unategemea mimi mwenyewe nifanyeje? Huo ndiyo ukweli sitaki kuwaficha mlikosea kuchagua.
Sasa katika uchaguzi wa mwaka huu mjipange vizuri, mchague mtu ambaye mtakuwa mmempa stendi akikataa nitamfukuza hata kwenye chama. Lakini leo nitamfukuza huyo aliyeko kwenye chama sijui hata yuko kwenye chama gani, nitamchukulia hatua gani?
Chama cha ACT Wazalendo kimelaani vikali na kuwahamasisha wananchi kukemea vikali kauli hizi za kibaguzi. Wamedai kuwa kitendo cha kuhamasisha ubaguzi na kuingilia mamlaka ya wananchi katika kuchagua mtu wamtakaye kinakiuka misingi ya Katiba yetu.
Wakuu, MAENDELEO HAYANA CHAMA
Rais Magufuli akiwa safarini kutoka Mtwara, ameombwa na mwanakijiji Jimbo la Kilwa kwamba hawana Stendi ya Magari hivyo anaomba wajengewe. Rais Magufuli amejibu kwamba siku nyingine waangalie wawakilishi wanaowachagua ili waweze kufanya vile yeye anavyowaagiza. Mbunge wa jimbo hili aliyemaliza muda wake ni Seleman Bungara aka Bwege Mzee wa ''Umesikia Wapi'' ambaye alikuwa anatokea chama cha wananchi CUF Habari
Rais amezidi kusema kwamba miradi kama hiyo ni ya wabunge na Madiwani ndiyo wanapaswa kuisimamia hivyo kuwataka wabaki na Bwege wao
Rais Magufuli amesema haya...
Nilikuja hapa nikasema nichagulieni watu nitakaokuwa nawaagiza wanafanya ninayoyataka mkasema hapana, Mkamchagua Bwege basi shauri yenu na bwege wenu mwambie awatengenezee stendi
Kazi ya Stendi ni ya madiwani, wabunge. Ukikosea kuchagua, nafuu ukosee kuoa au kuolewa. Ukikosea kuchagua ni tatizo kubwa.
Na hili ndugu zangu niwaombe, muwe waangalifu katika kuchagua. Mchague watu ambao watakuwa kwa ajili ya watu masikini.
Tunatuma hapa fedha za road fund, tunatuma fedha hapa za halmashauri, zimeshindwa kweli kujenga stendi?
Lakini kwa sababu mnanichagulia, wao wenyewe mastendi unategemea mimi mwenyewe nifanyeje? Huo ndiyo ukweli sitaki kuwaficha mlikosea kuchagua.
Sasa katika uchaguzi wa mwaka huu mjipange vizuri, mchague mtu ambaye mtakuwa mmempa stendi akikataa nitamfukuza hata kwenye chama. Lakini leo nitamfukuza huyo aliyeko kwenye chama sijui hata yuko kwenye chama gani, nitamchukulia hatua gani?
Chama cha ACT Wazalendo kimelaani vikali na kuwahamasisha wananchi kukemea vikali kauli hizi za kibaguzi. Wamedai kuwa kitendo cha kuhamasisha ubaguzi na kuingilia mamlaka ya wananchi katika kuchagua mtu wamtakaye kinakiuka misingi ya Katiba yetu.