GENTAMYCINE nami sasa naongezea ( nakazia ) hapo hapo kwa kusema..." Enyi Wakubwa wote ninaowateua katika Nafasi zenu mbalimbali Msijependekeze tu Kwetu Uzanakini Mkoani Mara ( Musoma ) bali naomba sasa mtawanye Maendeleo Tanzania nzima na kwa Kuanzia mnaweza mkaenda Chato Geita pale mkajenga hata Uwanja wa Ndege kwani hawana, na pia kuwepo na Benki kama ya CRDB na kuwa si mbali na Ziwani na kuna Wanyama wengi mnaweza mkaweka na Mbuga ya Wanyama, "
Pelekeni pia Maendeleo huko Kagera kwa Wahaya, Singida kwa Wanyiramba na Warangi, Kigoma kwa Waha, Dodoma kwa Warangi na Mwanza kule Kisiwani Ukerewe kwa Wakara kwani na Wao wanahitaji na wapenda Maendeleo kama haya ' Mnayojipendekeza ' kila Siku kuyaleta hapa mkoani kwangu Mara ( Musoma ) Mimi Rais GENTAMYCINE. Sitaki kila Maendeleo muwe mnayaleta tu hapa Mkoani Mara na mkiendelea na hii tabia ya ' Kujikomba ' Kwangu kuna Siku nitampiga Mtu Ngumi hadharani labda ndiyo mtanielewa.