Rais Magufuli azindua umeme wa gesi asilia Kinyerezi II, asema ataendelea kushirikiana na wananchi kulinda amani

Waziri Kalemani yuko kwenye jukwaa anadanganya kwamba pesa zilizotolewa na Magufuli zote ni fedha za ndani. Uongo mkubwa.

Serikali imetoa 15% ya gharama. Zingine zote ni mkopo kutoka benki mbili za Japan, ndio maana ubalozi wa Japan upo jukwaani.
 
Waziri Kalemani yuko kwenye jukwaa anadanganya kwamba pesa zilizotolewa na Magufuli zote ni fedha za ndani. Uongo mkubwa.

Serikali imetoa 15% ya gharama. Zingine zote ni mkopo kutoka benki mbili za Japan.
Hawa watu wako kwenyw kampeni!!
 
Nani angefaa kuwa rais kwa mtazamo wako?
 
Kwani hii miradi ndio imeanza kuzinduliwa awamu hii?

Wewe nawe huenda ni msukuma!!
Mkuu naona kama unataka kuteleza, sijui ni hasira?
Kwahiyo kumbe tatizo ni Wasukuma.
Nilidhani Mheshimiwa Dr.Mashinji nae ni Msukuma, kumbe ni Malaika.
Afadhali leo tumeujua mtazamo wako binafsi 😀😀😀
 
Mimi huwa nashindwa hata kuelewa, kwanini vyama vya UPINZANI visiyachukue mambo haya kama AGENDA, Naamini watakomba wengi ambao hata ukiwaambia kuhusu maandamano watakuwa tayari kuliko kukomalia agenda ambazo hazipeleki Chakula mezani kwa watu kama BUNGE LIVE, MIKUTANO YA SIASA, KATIBA MPYA, TUME HURU YA UCHAGUZI n.k
 
Nani angefaa kuwa rais kwa mtazamo wako?
Anayefaa kuwa Rais ni yule aliyoko bize Ofisini akifanya kazi kwa bidii mno, yaani maneno machache halafu vitendo vingi na misele michache, kazi kwa wingi. Ni lzma tupate Rais mchapa kszi km alivyokuwa MKAPA. Kwa ssa tuna Rais mwenye porojo nyingi na mwenyewe kuamini ktk siasa za uwongo na maigizo wkt uhalisia ni zero!!
 
Unashauri nini katika uchaguzi ujao ili apatikane rais umtakaye?
 
Unashauri nini katika uchaguzi ujao ili apatikane rais umtakaye?
Ushauri mzito, unaelekezwa kwa wapiga kura kwani hao ndiyo walostishaji wakubwa. Watafute Elimu ya Uraia, waelimike na kujifunza kutathmini aina ya kiongozi mzuri kbla ya kupiga kura. Wengi wetu wa TZ, bado tuna weledi na fikra finyu mno, niwapiga vigelegele bila kuifikirisha Akili
 
Mods na mleta mada ibueni uzi wa JK akizindua Kinyerezi II ili twende sawa. Huu ni uzinduzi hewa
 
Rais hajali sheria, cheki anavyosema:

Rais Magufuli: Inaniboa sana kusikia eti mradi umekwama kwa kukosa kibali cha Tanroads, au kibali cha mazingira, au kibali cha TRA, au kibali sijui cha bandarini...

Huyu si alikuwa anasimama barabarani kuzuia vitu vizito visipelekwe kwa barabara? Meli ya kwenda Lake Victoria iliyokuwa ibebwe na barabara kutoka Dar, si alikataa huyu?

Leo anasema hajali kibali cha TANROADS kubeba vitu vizito kupeleka kwenye miradi ya nchi?
 
Kila siku na kila kitu anazindua yeye, wasaidizi wake watafanya nini?
 
Mfumo mpya wa kununulia umeme ni mizengwe tupu
 
Sijaelewa mahali Fulani, yani jiji la daslam mahitaji megawatts 548 sasa wanapokea 754, hongera wananchi wa nchi ya darisalama manake mwenzetu mno umeme wa ziada megawatts 206, nyinyi kwenu mgawo wa umeme mnaosoma kwenye makumbusho ya taifa kwamba palikuwaga na umeme wa mgawo.

Hivi Tanzania tumeshindwa kutafuta chanzo kimoja au viwili vya uhakikia vya kuotoa gigawatts 5 kwa kila kimoja tuache kurukaruka kama hivi, yule alikuja na gesi, huyu kahamia stigilazi, atakuja mwingine atahamia kwenye umeme wa uranium kule songea, mwingine atakuja na wa makaa ya mawe pale nchuchuma, mwingine atakuja na maji ya bahari, atakuja mwingine atakuja na umeme wa kinyesi ya ng'ombe, alimradi kila mtu kapata kizindilio
 
Rais wetu wakati mwingine anakuwa hakumbuki matukio ya nyuma ama kwa bahati mbaya au kwa makusudi maalum.
 
Mbona sioni hapo kuwa kuna raia alingangania raisi mkono, askari wa usalama wamemgawana
 
Mbona sioni hapo kuwa kuna raia alingangania raisi mkono, askari wa usalama wamemgawana
Kunaa yulee alikimbiazana na wanausalamaa ukiacha yule mama aliekomalia mkono
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…