Rais Magufuli: Benki ya Dunia wanatoa pesa wakijua Tanzania tuna msimamo gani na tunafanya nini, wapiga kelele wapuuzwe

Rais Magufuli: Benki ya Dunia wanatoa pesa wakijua Tanzania tuna msimamo gani na tunafanya nini, wapiga kelele wapuuzwe

Rais Magufuli akiwa katika hafla ya kuwaapisha mawaziri na mabalozi Ikulu leo, amesema kwamba kuna mambo mengi yamezungumzwa na tuyapuuzie. Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia alikuja hapa, mwaka jana, kwahiyo wanatoa pesa wakijua sisi Tanzania tuna misimamo gani na tunafanya nini, hao wengine ni wapiga kelele tu, wala msiwajibu kwasababu watu wa namna hiyo hawaishi duniani.

Awali wiki iliyopita, zilikuja taarifa kwamba Benki ya Dunia WB imesema inafikiria uwezekano wa kuikopesha Serikali ya Tanzania mkopo wa dola za kimarekani milioni 500 sawa na Trilioni 1.152 za Kitanzania kwa ajili ya kuboresha sekta ya Elimu, mkopo uliokuwa umesimamishwa na benki hiyo kutokana na Rais Magufuli kutangaza kuzuia wanafunzi wanaopata mimba wakiwa shuleni kutoendelea na masomo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, benki ya Dunia imedai kuwa ilipokea barua kutoka wanaharakati kutoka nchini Tanzania ambao walieleza kuwa, Benki ya Dunia kuendelea kutoa mkopo huo ni kuendelea kuwabagua wanafunzi kwa kigezo cha waliojifungua, wenye ujauzito na wasio Wajawazito.

Hivyo walitaka benki hiyo kusitisha mkopo huo tangu mwaka 2018, mpaka serikali itakapobadili sera yake ya kumzuia mwanafunzi aliyepata mimba kuendelea na masomo.

Pia soma > Tanzania yaweza kukosa Mkopo wa Dola Milioni 500 kutoka Benki ya Dunia
Nini chanzo cha mzozo wa huu mkopo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..lakini kununua ndege cash halafu kwenda kukopa kwa ajili ya elimu siyo busara hata kidogo.
NANI AMEKUAMBIA QAMWNUNUA NDEGE CASH? WAMEKOPA KULE WAKA LIPA HUKO CASH. THAT MEANS DENI JUU YA DENI. NA MANDEGE YENYEWE NI KAMA PICHA HAYAINGIZI ANY INCOME AMA KWELI SIFA ZINAUA
 
Ni kweli wapiga kelele wapuuzwe tu hakuna namna, wewe unapiga kelele na bado serikali hiyo hiyo inakuhudumia,unaishi kwa amani pamoja na njaa yako na shida zako lakini bado tu unapiga kelele,usaidiweje sasa?

nitarudi baadae
Serikali ina-exist kwa hisani ya wananchi na wala wananchi hawa-exist kwa hisani ya serikali.

Ukilielewa hilo ndio utakuwa walau na akili kidogo.
 
Ila sasa ule mchezo wa kutudanganya kuwa miradi inafanywa kwa hela za ndani ndio wakome kutwambia uongo kama huo.

Hii nchi ni 100% Donor Dependent, kama hata vitu muhimu kama elimu ambayo mnaiweka mbele kwenye orodha ya vipa umbele vyenu kumbe hamna hata mkakati wa kuushughulikia ni wananchi gani watawapigia kura kuwarejesha madarakani, lazima tu ma-DED wawaokolee jahazi, make hamna namna.
 
Serikali ina-exist kwa hisani ya wananchi na wala wananchi hawa-exist kwa hisani ya serikali.

Ukilielewa hilo ndio utakuwa walau na akili kidogo.

Kushea uraia na akili nyingine ni mzigo. Kuna Mtanzania mahali ana uwezo wa kurusha satellite lakini hatofanikiwa kwa vile tu yuko kwenye nchi moja na Fred mwakitundu
 
Daah Hawa world Bank haya Sasa wameshawasikia wapiga kelele! No mkopo
 
wamesema Tanzana ni donner country sasa mbona bado wananyoosha mkono?
 

Rais Magufuli akiwa katika hafla ya kuwaapisha mawaziri na mabalozi Ikulu leo, amesema kwamba kuna mambo mengi yamezungumzwa na tuyapuuzie. Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia alikuja hapa, mwaka jana, kwahiyo wanatoa pesa wakijua sisi Tanzania tuna misimamo gani na tunafanya nini, hao wengine ni wapiga kelele tu, wala msiwajibu kwasababu watu wa namna hiyo hawaishi duniani.

Awali wiki iliyopita, zilikuja taarifa kwamba Benki ya Dunia WB imesema inafikiria uwezekano wa kuikopesha Serikali ya Tanzania mkopo wa dola za kimarekani milioni 500 sawa na Trilioni 1.152 za Kitanzania kwa ajili ya kuboresha sekta ya Elimu, mkopo uliokuwa umesimamishwa na benki hiyo kutokana na Rais Magufuli kutangaza kuzuia wanafunzi wanaopata mimba wakiwa shuleni kutoendelea na masomo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, benki ya Dunia imedai kuwa ilipokea barua kutoka wanaharakati kutoka nchini Tanzania ambao walieleza kuwa, Benki ya Dunia kuendelea kutoa mkopo huo ni kuendelea kuwabagua wanafunzi kwa kigezo cha waliojifungua, wenye ujauzito na wasio Wajawazito.

Hivyo walitaka benki hiyo kusitisha mkopo huo tangu mwaka 2018, mpaka serikali itakapobadili sera yake ya kumzuia mwanafunzi aliyepata mimba kuendelea na masomo.

Pia soma > Tanzania yaweza kukosa Mkopo wa Dola Milioni 500 kutoka Benki ya Dunia

Sasa kama ni wa kudharauliwa, basi hasingelisema. Yeye mwenyewe angenyamaza. Sasa yeye anawajibu alafu anawaambiwa watu wasiwajibu.
 
Mimi nashangaa sana waandamizi serikalini kwa kurumbana na wanaharakati wakati wanachotakiwa ni kufanya mawasiliano ya karibu na watoa pesa ambao ni Benki ya Dunia!

Kazi ya msingi ya waandamizi serikalini ni kuhakikisha wanafanya linalowezekana ili maombi ya mkopo yakubaliwe. Kukubaliwa kwa maombi yao ya mkopo itakuwa ni jibu lao kwa wanaharakati na sio kupigizana kelele!

Please, focus on the World Bank and the rest will take care of itself!
Serikali yetu inajichanganya, inachanganya washirika wetu wa maendeleo, au watendaji wake wamezoea kauli za uongo na unafiki?
1. Inajinasibu kuwa nchi hii ni tajiri ina inakusanya pesa za ndani za kutosha kutekeleza miradi ya maendeleo bila kutegemea ufadhili kutoka nje ya nchi, na
2. Tunasahau kazi za mabolozi nchini, kama ilivyo kwa mabolozi wetu wanaowakilisha Tanzania nchi za nje, ni zipi.
Hata hivyo viongozi wakuu wa nchi wanaposimama majukwaani na kudai kuwa hakuna ubaguzi katika elimu, wanadanganya na kufurahisha nani?
Waziri wa mambo ya nchi za nje alinukuliwa akidai eti "wanafunzi waliozaa wamewekwa kwenye utaratibu ulio nje ya mfumo rasmi wa elimu"!
 
Mara Oooh hatubabaishwi na mabeberu, Mara Oooh hatutaki pesa za mashoga!

Shwaini.Mbona mnaulilia huo mkopo sasa?
 
wamesema Tanzana ni donner country sasa mbona bado wananyoosha mkono?
Tanzania bado sana!
Shida ni hz:
1. Uongo na unafiki,
2. Kujisifia kupita kiasi, na
3. Kuishi kwa matumaini.
Uongo na unafiki ni tabia za watanzania karibu wote hata viongozi wanazo. Wanasema yasiyo ya kweli na wasiyoyaamini.
Watanzania pia wanapenda wasifiwe kwa mambo madogo madogo na wasiyohusika nayo moja kwa moja.
Siasa za malipo kutokana na fidia za makenikia zilipelekea uchumi wa nchi kutikisika na kutufikisha pabaya tulipodhani tungezipata; tungeamka tumetajirika. Hatukujua kuwa yalikuwa ni matarajio tu kama ya "mateja" wanaojikuta "peponi" ghafla. Tulianza kutumia fedha za mikopo na zisizokuwepo.
 
Back
Top Bottom