Wazo la Masele ni la kijinga sana Magufuli hana muda wa mwekezaji kuja kuwekeza mabembea
Watanzania wanatakiwa wachape kazi kama kauli mbiu inavyosema
Mkuu Wanasiasa wamekuharibu kichwa.
Dunia ina siri kubwa sana.
Hivi mwezi mzima wanasiasa waliokaa Dodoma wamezalishia nini ?
Hivi Wale Elfu 43 waliokua wanataka Kazi ya kuwakalia Watanzania kama Punda ili wao waishi maisha kama wako Peponi kupitia CCM tuu walikua wanataka kwenda kuchapa kazi au kwenda Kulala Bungeni na kugonga meza ?
Hivi unajua wateule wa nchi hii ni zaidi ya elfu moja achilia Mbali Wabunge watu ambao ndio wanaomaliza kodi kwa asilimia kubwa huku wachapa kazi wakifia vijijini na mitaani wakizalisha kwa jasho na Damu??
Hivi unajua pesa ni makaratasi tu yaliyopewa hadhi na mifumo ya watawala wa dunia na matajiri ili washirikiane kuwatumia maskini wa dunia ambao ni zaidi ya 80% ya wakazi wa Dunia. Kama unabisha angalia mifumo ya fedha na ya kubadilishana fedha utajua kuna akili kubwa imetumika kuwa hadaa watu ili hela ionekane kuwa wanaopaswa kuwa nayo ni wachache na waipate kwa kubeba mamizigo kama Punda na ujira kidogo.
Kama unabisha angalia wasanii wanavyoishi maisha ya kifalme kwa kufanya ujinga ujinga huku wakiwa wanawafurahisha matajiri na watawala majukwaani.
Kama unabisha angalia Wachezaji Ulaya na duniani kote wanavyolipwa mabilioni ya hayo makaratasi yanayoitwa Pesa kwa kazi ya kupiga mateke Gozi la ng'ombe huku muokota makopo akiwa analipwa Sh.250/- kwa kilo moja ya machupa ya maji.
Pesa ni karatasi zilizoidhinishwa na wajanja tuu waliokaa maofisini huko Ulaya wakatengeneza mfumo kupitia watawala na wakauwekea formula wanayoona itanufaisha Ulaya milele.
Kama unabisha jiulize hela (karatasi) ikichakaa mbona inasagwa sagwa na kutupwa tu na mzunguko unaendekea kutengeneza hela mpya?
Kama unabisha kuwa pesa sio makaratasi tu ya wazungu waliyoyapa hadhi kwa siri na vigezo vigumu vya kuwanufaisha wachache muangalie Gwajima ,Kakobe,Marehemu (Hayati) mama Rwakatare, Mwingira, Mzee wa Upako, Shekhe mkuu,Shehe wa mkoa , maustazi wa kutoa kile wanachokiita majini, wabunge wanaokaa na kuongea tu bungeni huku Wakiwapangia bei wakulima na kupanga nani anunue na alipe kodi kiasi gani!! Mchapa kazi na mvuja jasho na Damu hana amri wala mapendekezo kuwa alipe kodi au asilipe na alipe kwa kiasi gani??
Kama unabisha kuwa pesa sio makaratasi tu yaliyopewa hadhi na wazungu weupe na kuwaweka mawakala wao weusi tii ili Ulaya waishi kama Peponi huku wao pesa ikiwa ni haki ya kila MTU kuipata ili anunue chakula nenda ukawaulize Wafanyakazi wa Tanzania ya CCM wanavyoambiwa siwalipi zaidi ya kiasi hiki kinachotosha kula chakula cha mtu mmoja tu kwa mwezi bila familia yake kujua itakula nini na wanasisitizwa kwa mkwala kabisa kuwa kama hamtaki acheni kazi . Wakati huo huo huo Mkoloni na aliyeshiba sheria na kanuni za kikoloni anayewaambia Binadamu wenzake hivyo yeye anaishi kama mungu tofauti tu ni kuwa ipo siku atarejea kwa mola wake kama binadamu wenzake. Na wapiga siasa wanajiwekea maslahi makubwa na kanuni za kuendelea kulipwa mpaka kufa bila kuzalisha chachote .
Na ukiwaambia kama mmeshindwa mbona nyie hamuachi tukawachagua wengune basi wanafanya kila hila upate kuitwa msaliti tena unajua adui mkubwa.
Afrika kiongozi kuzunguka mitaani na misafara ya magari na mapesa mifukoni ,huku kodi za wananchi zikiwa zinateketea kwa kununua mafuta ,vipuri vya magari , posho za mamia ya walinzi na wapambe na miziki na wasanii ,anaitwa mchapa kazi bila kuzalisha Chochote kinachoweza kuuzwa na kuliingizia taifa makaratasi yanayoitwa pesa kwa vigezo vya Elimu ya Mzungu aliyepo huko Ulaya. Hakika Washwahili walisema kuwa Pesa ni makaratasi tuu.
Kama unabisha kuwa pesa sio Makaratasi zunguka vijijini uone jinsi wakulima wanavyolima kwa jembe la mikono kwa miaka nenda rudi bila kustaafu mpaka wanaingia kaburini lakini hakuna anayeidhinisha Pesa ili wazee wote wenye umri zaidi ya miaka 65 walipwe pesa za kujikimu kila mwezi mana hawana uwezo na nguvu ya kufanya kazi mashambani.
Wao wanaachwa tu as if ni binadamu ambao hawakutoa huduma yoyote kwa binadamu wenzao hapa duniani. Yaani MTU anayefyeka tu nyasi za Majumba makubwa kama Ikulu na bunge analipwa mapesa na kiinua mgongo juu bila kuzalisha chchote kinachoweza kuliingizia taifa pato kama korosho ,kahawa,pamba, katani, Mkonge n.k . Huku mkulima akiendelea kuhenyeka kwa kazi tu bila Uhuru wa kuamua chochote cha kitaifa zaidi ya kuamuliwa mpaka kura yake kugeuzwa wanavyotaka wakubwa na mabwana fedha wa nchi .
Kama unabisha kuwa pesa sio makaratasi nenda ukawaulize Wakazi wa Nchi ndogo kabisa Duniani inayoitwa Vatican kama wanachapa kazi gani na wanazalisha nini na maisha wansyoishi ni magumu au ni mepesi au asiyefanya kazi asile inawahusu au ni mpango tu wa kuwafanya wakazi wa Dunia kuwa watumwa wao na wa mawakala wao waliowaweka kila nchi kutimiza malengo ya kuwafanya wazungu kuishi maisha kama Peponi huku waafrika wakiitwa Wavivu na bado hawastahili kupata pesa Hata za kuishi kulingana na mabilioni yanayoingia kutokana na rasilimali za asili zilizopo Afrika.
Yaani Wazungu wanawaita waafrika kuwa ni watu wavivu lakini waliwachukua utumwani kwenda kuwafanyia kazi.
Leo hii ukienda kule umasaini vijana wengi wanasoma Sheria badala ya kusoma digrii za Mambo ya ufugaji na kilimo kwa sababu tu wakoloni weusi wakishirikiana sasa na weupe wameweka hadhi ya mtu mwenye kujua jambo Fulani lililoletwa na mzungu kuwa atalipwa fedha nyingi. Sasa vijana wanapita na Vi NGO s vingi na viofisi vingi vya kutetea maslahi ya wafugaji huku wao wakiwa hawana Hata ndama mmoja au mbuzi mmoja aliyefungwa chini ya mwembe. Wanachotaka ni kupata karatasi inayoitwa Pesa kwa mfumo wa kikoloni unaosimamiwa na serikali zilizorithi mifumo ya kikoloni.
Hivi unajua kuwa siku hizi Mkulima wa nyanya anayelima kwenye karatasi anapata pesa nyingi kuliko Mkulima anayechapa kazi shambani?
Tafakari ndugu.
Kuna mambo Mengi sana ukiyatafakari utagundua kuwa Cheyo hakukosea alipokuja na Sera ya kuwajaza watu mapesa mifukoni.
Kuna Mambo yameletwa duniani na Shetani ili watu waishi maisha Magumu kisha wamkufuru Mungu.
Sio kila slogani inayofurahisha ina uhalisia kwa yule anayeitoa.
Mbunge anayefanya kazi masaa matatu au manne tu kwa mshahara wa walimu zaidi ya 20 anaweza kumfikea Mwalimu kwa kejeli kabisa huku akipigiwa makofi na wazazi walioshindwa hata kulea na kukaa na watoto wao kipindi cha Korona , kuwa hafanyi kazi wakati huo huo anasahau kuwa mwalimu anaingia kazini kuanzia SAA moja asubuhi mpaka SAA kumi jioni na akifika nyumbani bado ana kazi nyingi za kuandaa kwa ajili ya siku inayofuata.
Kuchapa kazi ni jambo la muhimu sana lakini kwa Mifumo ya kikoloni inayotawala dunia wachapa kazi kwa haki na kwa halali wanapata tabu sana.
Mkurugenzi akikaa ofisini kuchapa kazi yake halali na kwa haki kama alivyoapa wakati huu atapata tabu sana mana atakua anachezea kazi yake inayompa riziki kupitia Pesa (makaratasi ya mzungu yanayosimamiwa na walimteua na kumpa gari na ofisi ).
Tafakari Mkuuu!!
Wajanja wajanja kama akina Fulani wanaokimbilia CCM na kupewa ubunge bila kuchapa kazi ya kukubaliwa na wananchi ni tatizo kubwa sana linalowafanya wananchi kuwa watumwa kwenye nchi yao na kukosa raha duniani.