Richard, Mkuu Richard, long time no see bro lakini dah, sikubaliani na wewe bhana!!
Mosi, hata watu wanaopigia upatu lockdown, wote ukiwasikiliza wanasema wazi kwamba lockdown kwa watu lakini usafiri wa mizigo uendelee kama kawaida. That being said, hoja yako ya kukosa kodi, hapo haiingii!!
Magu kajificha Chato?! Mi sijui bhana lakini inakuaje mtu ambae alikuwa Chato kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka na kurudi Dar January 09, leo hii tena awe Chato kwa siku zote hizi?! Kwanini asiji-lockdown Ikulu ya Dar au Dodoma ili aendelee na shughuli zake kama kawaida?!
Yaani Chato kuwe na facility bora kwa ajili ya usalama na afya yake binafsi na familia yake, kuliko Ikulu ya Dar es salaam?
#MagufuliTokaChato bhana!
Marekani walileta vurugu siku nyingi?!!
C'mon Rich, hebu fuatilia zile vurugu na maandamano yamefanywa na nani! Kama utakumbuka, Trump amekuwa akibishana na baadhi ya Magavana huku yeye akitaka lockdowns ziondolewe huku magavana wakisema hapana!!
Trump alifikia hadi kusema yeye anayo mamlaka ya kuingilia maamuzi ya kimajimbo!!
In response to that, ndipo watu wakaandamana ingawaje sio wengi kama inavyovumishwai! Kuona hivyo, Trump akazidi kuwa-encourage. Pitia ukurasa wake wa Twitter siku ya April 17 uone tweets zake za "LIBERATE MINNESOTA", "LIBERATE MICHIGAN", LIBERATE VIRGINIA ambapo alikuwa anawa-pump!
Watu wakaamini kwamba Wamarekani wamechoka, polls ikaendeshwa! Kuja kufanya uchunguzi ikaonekana sio tu majority ya Americans wanahofia lockdown kuondolewa mapema lakini pia ikaja kugundulika walioandamana ni wafuasi wa Trump, ambao kimsingi walitaka kumuunga mkono!
Na kundi lingine linalopigia upatu kuondolewa lockdown ni House of Freedom Caucus! Kama unafuatilia US Politics basi bila shaka utakuwa unawafahamu Freedom Caucus, na kwahiyo haishangazi kuona wao ni miongoni mwa watu wanaopigania sana kuondolewa lockdown!!
Nani waliyarusha sana haya maandamano? FOX...
Kwamba Georgia wanataka ku-unlockdown; sawa! Kwani mliambiwa lockdown ni milele? Kama wanaona hali inaruhusu, haishangazi kusikia wanataka kupunguza makali ya lockdown to partial lockdown! Hata Wuhan lockdown iliondolewa baada ya kuona hali inaruhusu!
Khaaa! Nani huyo kasema Rais anatisha watu?!
JPM haitishi watu bhana sema anawajaza watu ujinga!!
Mkuu Rich hebu kuwa honest ndugu yangu!!! Yaani unasema:-
Halafu, wewe wasema kwamba anatisha watu ni vipi anatisha? Ikiwa watu wanapotosha ukweli wa habari na kutoziamini taarifa za wizara husika ya afya wewe wataka upotoshaji wa taarifa uendelee ama?
Hapo sijakuelewa ujue?! Yaani unamaanisha JPM ndie anaweka rekodi sawa dhidi ya wapotoshaji, au?!
JPM huyu huyu aliyesema coronavirus haiwezi kuingia kanisani na msikitini, au JPM mwingine?!
JPM huyu huyu aliyesema baadhi ya barakoa zina coronavirus, au JPM mwingine?
JPM huyu huyu aliyewahi kusema barakoa ni "mavitambaa ya puani" tu na hayasaidii kujikinga na coronavirus except imani kwa Mungu, au JPM mwingine!!
Unamaanisha huyu huyu ambae jana kaja na mpya kwamba mvuke na wenyewe ni tiba (au kinga?) ya coronavirus, au kuna JPM mwingine?!
Hebu ngoja... si ndo huyu huyu ambae mwaka 2015 alisikika akisema ni namna ilivyo rahisi kufanya uchenjuaji wa makinikia cuz' it's a matter of raising the temperature in the furnace, na metal with a lower melting point, itaanza ku-melt na kuiacah nyingine na hivyo kufanikisha ku-separate gold from copper concentrates!!!!
Ndo huyo anayeweka rekodi sawa dhidi ya upotoshaji, au kuna mwingine?!