Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

Rais Magufuli: Hakuna Lockdown kwa Dar wala Tanzania, NEVER! Tusiwatishe watanzania, hofu ni ugonjwa mkubwa kuliko Corona

JokaKuu,
Asante sana, hapa kaonyesha weakness kubwa sana, he doesn't deserve to be there. Na ni dhahiri kiatu ni kikubwa sana kwake, tunatakiwa sasa kumpatia iyo nafasi MTU mwingine atakayeweza kusimama nasi kwenye majanga kama haya mstari wa mbele.

Nyumba inavamiwa na vibaka tuu halafu baba unakuwa wa kwanza kukimbilia kujificha uvunguni halafu unawaacha baadhi ya wanao sebleni wanapambana wenyewe, aibu hii. Hii ni corona tu imekuwa hivi sasa sipatii picha ikitokea vita atakimbilia wapi..hahahahahahahahaha.
 
Mfumo mzima wa kupata viongozi wetu una uwalakini....

Tusipolisimamia hili kidete watanzania hasa kwa kuanzia kwenye katiba yetu kuna siku tutajuta!! Tutalia na kusaga meno!!
 
Its more like kafichwa, acha waziri mkuu na waziri wa afya wawe frontline wakifa hao wa bunge ni wengi unachagua tu wengine.
Kama chess tu mbele wanaenda pawns.
Za kuambiwa changanya na zako!Tupige kazi wakati yeye kajificha,chukua hatua!
 
Sote tunashuhudia jinsi Rais wa Cotanza anavyozamisha jahadi kwa kutake advantage ya umasikini wa Cotanza walio wengi na ujinga wao dhidi ya virusi hatari zaidi Corona vinavyosababisha homa kali ya mapafu kwa ugonjwa COVID_19).

Njia za kupunguza kusambaa kwa maambukizi zilithibitiswa na kutumiwa na mataifa karibia yote ulmiwenguni ni kuzuia mikusanyiko ya watu, matumizi ya masks zilizo sahihi, kunawa mikono mara kwa mara na kubwa zaidi ya yote kujitenga.

Haya yote ni majukumu na wajibu wa kila mmoja wetu pamoja na mamlaka ya nchi na yanawezekana bila shaka yoyote.

Wananchi ama RAIA mmoja mmoja ambao kwa hakika hakuna anayependa kupoteza maisha kwa janga hili wamefanya liwezekanalo katika kunawa mikono kwa kadri wawezavyo na kufuata miongozo itolewayo na mamlaka. Kwa babati mbaya ama makusudi jemedari mkuu ile ya Cotanza amekuwa akipotosha sielewi kwa lengo gani ila ni nia iliyo ovu inayopaswa kuingiliwa kati na mamlaka zingine nitaainisha upotoshaji wa wazi wa jemedari mkuu.

1. Tuendelee kwenda makanisani/misikitini ambako anafahamu wazi watu wataendelea kukusanyika na kusababisha usambaaji wa hali ya juu wa virusi hivi. Licha ya mashule kufungwa ila haikuwa na maana kwa sababu bado watoto walewale wanaruhusiwa kukusanyika makanisani na misikitini. Inasikitisha sana.

2. Mteule wake aliwatangazia watu wa Cotanza kuwa waliopona ni 5 mpk jana, ila yeye kutaka kuzidi kuonyesha hakuna tatizo kubwa LA virusi hivi akatutangazia hizo data za waziri wake siyo kweli waliopona ni zaidi ya 1000. Hii ni kutaka kuwaamninisha watu kwamba hata ukiugua utapona jambo litakalopunguza umakini wa watu walio wengi kuendelea kuchukua tahadhari madhubuti.

3. Bwana yule anadai watu watumie hata masks za vitambaa. Hii anajua kabisa hizi masks hazizuii hata kwa 1% maambukizi ya virus na linapaswa kukemewa mara moja. Anafanya hivi akijua kwamba RAIA wengi hawatamudu masks zenye ubora hivyo wataendelea kuambukizana na kufa kwa wingi, badala ya mamlaka kuhakikisha masks hizi zinapatikana kwa wingi na kwa bei ambazo wataweza kumudu. Hapa ni kukwepa kugaramia uhai wa RAIA wake.

4. Kali zaidi ya yote ni kwamba ukiugua jifukize na sijui majani gani.. Hivi kweli tunajali uhai wa RAIA na kwamba ni tiba tosha ya corona. Mpaka hapa alipaswa kushtakiwa kwa makusudio na kupanga kuuwa RAIA wake ambao anapaswa kuwalinda kwa mujibu wa sheria. Imethibitishwa na mamlaka IPI ya kitabibu kwamba kujipiga mvuke utapona corona na machapisho gani yakutuaminisha hili.

Wito wangu ni kwa watu wa dini, taasisi mbalimbali za kiraia na zile za haki za binadamu, wataalam wetu wa afya kuingilia na kutoa elimu kwa usahihi dhidi ya janga hili. Ikibidi muweze kuzuia uendeshaji wa ibada ama kutafuta njia itakazuia mikusanyiko katika mahala penu pa kazi ili kuokoa wamumini wenu.

Tuliko fika kila mmoja ajiokoe yeye na wale anaoweza kuwasaidia walau kwa kuwapa elimu, kuwazuia dhidi ya mikusanyiko na kama unaweza kuwanunulia masks sahihi endapo kuna ulazima wa kutoka.

Jemedari wa nchi ile ya Cotanza amekwama na yeye kaikimbia nyumba yake inayoungua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuweka karantini Dar haitapunguza kuenea kwa ugonjwa, sababu kubwa ni kwamba hiyo karantini ni ngumu kutekelezeka na itatengeneza mianya ya rushwa na hao wanaosafiri nje ya dar wataendelea kutoka.

Umaskini wa wananchi, nchi, miundombinu, huduma za afya, uelewa na mifumo yetu ya kiutawala inafanya tusiige kila kinachofanyika huko kwingine.

Athari za ugonjwa kweli zipo, lakini karantini inaweza sababisha matatizo makubwa zaidi kuliko korona yenyewe kwa sababu nilizozitaja hapo juu.

Vilevile hatutarajii asilimia kubwa ya vifo kutokana na wakaazi wengi wa Dar ni vijana.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Karaoke,
Hiyo statement yako ya mwisho sijaielewa.kwamba vijana hawafi kwa Corona au? Au ndio kusema wanaokufa ni wale wenye magonjwa mengine pia?

Ni kweli karantini ina changamoto nyingi ambazo ni hatari na zinakwamisha mapambano dhidi ya COVID 19
 
mimi naungana na Mkuu LAKINI.....


“Wapo wanaotoa mawazo ya kuifunga DSM, haiwezekani kamwe, DSM ni center ambako asilimia kubwa ya mapato inapatikana, hatuwezi tu kuifunga DSM kisa corona, DSM ina Watu Million 6 hatuwezi kuwafungia, kesho tena Mwanza tuifunge hapana, hatuwezi kufanya lock down DSM”-

DSM, na Mwanza niliona mabasi yanapulizwa dawa na hasa DSM, hakuna upuliziaji dawa unaoweza kuua corona, ingekuwa pakipulizwa corona wanakufa, Nchi zinazoendelea wangemwagia Nchi zao kwa Ndege na wasingekuwa wanakufa, kule kupuliza dawa ni upuuzi tu” – JPM

“Hauwezi kuua corona kwa kupuliza dawa kwenye mabasi na mitaani ile unaua mende na wadudu wengine, ila hatujiulizi kwamba labda kupuliza ndio tunaongeza corona, maana DSM imepulizwa dawa tu na kasi ya wagonjwa imeongezeka, vyombo vya ulinzi mkachunguze nani alitoa hizo dawa”- JPM
 
Umetembelea mortuary za Marekani na Italy ambako wamejifungia? Au unasema tu, hata Rwanda umetembelea mortuary zake? Usijidanganye kaka, wewe mtaani kwako unakokaa, kazini kwako, kanisani kwako, kwenye ukoo wako umeona watu wangapi waliokufa kwa CORONA? Au unasikia maneno ya mtaani?
Mm nakaa mbezi beach waliokufa kwa corona wanaenda kuzikwa mbweni kwa siku zinapita gari kama 6 hivi. Kama huamini njoo ushinde mitaa hii utajionea ambulances zinavyopishana. Punguza mahaba mzee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom