Rais Magufuli: Huduma za NIDA ziwe kila Wilaya au NIDA watoe hela ya 'guest' kwa Wananchi. Ukiona bei ya mahindi iko juu, kalime yako

Rais Magufuli: Huduma za NIDA ziwe kila Wilaya au NIDA watoe hela ya 'guest' kwa Wananchi. Ukiona bei ya mahindi iko juu, kalime yako

Angejua hao anao waita wanyonge ndio wanaolia bei ya mahindi angechagua la kuongea, mbona dola hakuiacha ijipangie bei yenyewe ili wafanyabiashara wa fedha wanufaike? Bai kusiwe na bei elekezi kwa chochte hata madini yauzwe kwa utashi. Huyo mkurugenzi wa NIDA ajiandae kutumbuliwa kama kaitwa Morogoro wakati ni tatizo la nchi nzima ajue kachokwa.
 
Naomba nitoe ushauri kuhusu vitambulisho vya taifa.hao nida ilitakiwa wawepo kila wilaya na ofisi za kudumu ambozo hizo office inatakiwa ziwe na kila kitu kwa ajili ya kutengeneza vitambulisho na sio nida wawe wanatembelea watu hapana.nchi zote ndio wanafanya hivyo.
Zilikuwepo. Yeye ndiye aliziondoa
Mi nilipatia Kitambulisho NIDA Magomeni, baadaye wakahamishia Makao Makuu Kawe
 
Nida ni janga,yaani hata upate namba ya nida,kukidownload kitambulisho Napo ni bonge ya mtihani
 
Tatizo la NIDA ni bajeti finyu, hawawezi kuajiri watumishi na vifaa vya kutosha ni changamoto. Watafunguaje ofisi kila wilaya wakati hawana watumishi wa kupeleka huko?
 
Mtumishi wetu Dr Magufuli anatupigania

Subiri mpe kura yako 2020 ndio inayotafutwa tu, izo ni siasa tu sasa mkurugenzi kwani ndie anayekwamisha, mkurugenzi hazai vitambulisho, vile vitambulisho you never know pengine ata karatasi za kuchapishia serikali hawana, pengine hawana staff wa kutosha kwenye hii ajira zoezi ndio linakuwa gumu lakin akisimama atasema mkurugenz njoo haraka.

yaani mtapelekeshwa kweli kweli nyie nyumbu.
 
Vitambulisho vya taifa vingekuwa vinalipiwa, mathalani shilingi elfu 20, hiyo ingetosha kuwawezesha NIDA kufanya kazi yao vizuri na kwa uweledi, kinyume chake ni kuwachosha tu watendaji. Kama alivyoagiza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam muoge kabla ya kwenda mjni, mimi nashauri muoge kabla ya kwenda ofisi za NIDA mnatia gundu ndiyo maana vitambulisho vinachelewa, si kwa majasho na vikwapa vile, ofisi za NIDA siendi tena.
 
Nikuongee sio kila Wilaya iwe kila kata maana kuna vijiji vingine nauli kwenda wilayani ni kuanzia Tsh 7000 vip mtu atoe 14000 kwenda na kurudi na pengine aambulie nenoj njoo kesho.. hii warudi kwenye kila kata hata kwa siku 3 kila kata..itapunguza usumbufu
Naomba nitoe ushauri kuhusu vitambulisho vya taifa.hao nida ilitakiwa wawepo kila wilaya na ofisi za kudumu ambozo hizo office inatakiwa ziwe na kila kitu kwa ajili ya kutengeneza vitambulisho na sio nida wawe wanatembelea watu hapana.nchi zote ndio wanafanya hivyo.
 
Kiukwel ofisi za NIDA huduma zinaonekana zipo chini Kuna shida ambazo zinapelekea kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa namba +vitambulisho venyewe

1)Watumishi ni wachache, idadi ya watumishi ni wachache ukilinganisha na huduma zinazotolewa lwa wananchi watumishi waliopp wanalemewa na mzigo wa watu, wakati uncle anaingia madarakani aliwaondoka wafanyakazi takribani 500 waliokuwa wanafanya kazi kwa mikataba, hii kidgo ilikuwa inasaidia kupunguza mzigo wa kazi, sasa hv, ofisi za nida ukienda wafanyakazi hawazidi watano waliowwekwa permanent tena hao watano bahati na kama sipo wrong ni mkoa wa kagera nenda Morogoro pale tubuyu, ofisi ya nida ghorofa za kutosha lakini ulizia watumishi wa kufldumu wapo wangapi utaambiwa hata watano hawafiki.

2) Sehemu ya uchakataji, sehemu ambapo wanazalisha vitambulisho IPO moja pale kibaha, just imagine (tengeneza picha kichwani kwako) Tanzania nzima uchakataji/utengenezaji wa vitambulisho unafanyikia sehemu moja, watanzania tupo wangapi ?

Hapa ningeonelea kama wangekuwa na kanda/zones za kutengeneza vitambulisho kwa mfano kanda ya kati wawepo Dodoma wanazalisha vitambulisho, kanda ya kasakzn wawepo Arusha wanazalisha vitambulisho na kadhalika kusini wawepo mbeya wanazalisha vitambulisho ili kupunguza overrides ya kazi ya kuzalisha hizo I'd.

Nawasilisha
 
Nashauri zoezi la utoaji wa vitambulisho vya Taifa lisipewe presha kubwa na makampuni ya simu.
Zoezi la usajili wa line za simu na utoaji wa vitambulisho vya Taifa liwe ni zoezi endelevu.

Ofisi za wilaya za NIDA zishilikiane na Makampuni ya utoaji wa huduma za mawasiliano ili taarifa za waliopata vitambulisho zichukuliwe kama taarifa rasmi za usajili wa line za simu.

Hata hivyo Watanzania tujifunze kushiriki michakato au kutokudharau vitu muhimu ambavyo hapo baadae tunaanza kujutia kwanini tulishindwa kujitokeza mapema kushiriki.
 
Bado mahakamani, wanalambaga kuanzia 10 hadi 20 na haina risti. Kwa wale wasio na vyeti vya kuzaliwa
 
Hapa Nida wamezidiwa nguvu maana kuna watu waliondolewa Nida ambao walikuwa wamepewa training nzuri ya mwezi mzima mwaka 2016,Toeni ajira kwa vijana wapige kazi hasa wale mliowatoa maana wapo tu mitaani
 
Back
Top Bottom