Rais Magufuli huhitaji kujieleza unapomtoa Waziri. Kwa January Makamba jikalie kimya

Rais Magufuli huhitaji kujieleza unapomtoa Waziri. Kwa January Makamba jikalie kimya

Mimi nilifikiri baraza la mawaziri likikutana hapo ndipo waziri asiyetekeleza majukumu anapata kibano. Miaka minne ni mingi kwa asiyefanya kazi zake vizuri.
 
We jamaa kigoma vumbi linatuua halafu uko jf unajifanya mbunge wa taifa..
Najutia kura yangu niliyokupigia.
Hupati tena kura yangu..

KG kuna matatizo lukuki wewe unakazana na mambo ya kitaifa wakati mkoa wako upo kwenye top 5 ya umasikini..
Tunajua mbunge hana uwezo wa kujenga lami mwenyewe lakini una uwezo wa kuikumbusha serikali kila siku.
Lakini umekazana tu na korosho za mtwara mala mifuko ya plastic ....dadadeq
 
Mie ninachokiona hapa ni kuwa Makamba junior alibebwa kwa sababu ya baba kama mke wa JK ALIVYOINGIA MJENGONI. Vinginevyo dogo angesogezwa pembeni kabisa tangu mwanzo. Angalia waliomfuata kwenye kinyang'anyiro 2015 wapo wapi sasa, wanasikika!
sASA DOGO HANA LAKE TENA BAADA YA BABA kumnyooshea kidole Magu
 
Hapo ndipo unapofeli bwana Zitto. Unafiki mwingi sana unapoona fursa. Unasema hukusikia lalamiko kuhusu NEMC kwenye kikao cha rais na wafanyabiashara!

Mwakilishi kutoka Iringa alilalamika kuhusu nini. Kama una malengo na uongozi kuwa real. Ila kama lengo lako ni kujenga SACCOS big up. You are very smart at outsmarting cheap thinkers.
 
Unataka kusema raisi hajui ni kipi cha kusema au kutokusema??
Watu walitegemea JPM leo angeongea mengi sana,bahati nzuri naona washauuri wake walikuwa smart sana ktk hili tangu aingie madarakani,Ameongea short and clear hajaongea wengi walivyotarajia maana hata radio za mbao zilijiunga ikulu leo.

Tangu aingie madarakani,washauri wake wamefanya kazi yao vema sana.
 
Rais Magufuli kwenye sababu za kumuondoa January Makamba bora jikalie zako kimya.

Nimekusikia Rais leo ukijaribu kuelezea sababu za kumuondoa Uwaziri Bwana January Makamba. Kwa kweli hukuwa umejiandaa na maelezo ya kuridhisha.

Rais, kwenye suala la mifuko ya plastiki tunajua ukweli kwamba wewe ndiye ulizuia lisiendelee ulipoambiwa kwamba litaua viwanda. Tunajua kwamba January ndiye ametumia miaka mitatu kuwaandaa wenye viwanda vya mifuko ili wabadilishe teknolojia na wasipate hasara. Tunajua kwamba January alifanya vikao vya umma (public hearings) kuanzia Karimjee mwaka 2017 hadi Mwanza mwaka 2018 na kwingineko kushirikisha wananchi kwenye jambo hili. Tunajua kwamba hatukusikia kauli yako kwenye mifuko ya plastiki hadi baada ya suala hili kufanikiwa. Hii sio kawaida yako maana wewe ni very predictable.

Tunajua kwamba mlimtegea Makamba ili afeli halafu mumtimue. Hakufeli. Sasa mnamtimua kwa kukamilisha kazi kwa weledi mkubwa! Mhe Rais wewe ni mkali maelekezo yako yasipotekelezwa. Umemuachaje Waziri miaka minne kwa kutotii maelekezo halafu unamtoa baada ya utekelezaji? Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kukubali hoja yako hii dhaifu sana.

Bwana Rais ulikutana na wafanyabiashara kote nchini kutwa nzima. Walitaja kero zao zote, nami nikaziorodhesha. Sikusikia hata mmoja akilalamikia NEMC. Kwasababu gani? Kwasababu January ameibadilisha NEMC. Alitaka kuibadilisha huko nyuma na akavunja bodi na kuondoa menejimenti lakini kwakuwa inasemekana kulikuwa na ndugu zako walioguswa ukaagiza uamuzi ule ubatilishwe. Unadhani Watanzania wamesahau?

Bwana Rais fedha zinazotolewa na wahisani kwenye miradi ya mazingira zinakaguliwa na CAG na hakuna popote palipoonyesha ubadhirifu au upotevu. Kama upo uweke hadharani kama sisi tulivyoweka hadharani ubadhirifu wa TZS 1.5 Trilioni. Wacha wahisani, Serikali yako haijaweka hata senti tano kwenye miradi ya mazingira nchini. Mimi ni Mbunge na ninapitia kila Bajeti ya Serikali na Taarifa za CAG. Hujawahi kutenga fedha za Mazingira. Kwa kifupi, tunajua wewe binafsi sio mpenzi wa mazingira na umesema hivyo mara kadhaa. Hata huyo January mwenyewe “ulimtupa” kwenye mazingira ili apotee lakini ghafla kila Mtanzania leo anaongea mazingira. Hata wewe nawe leo unayaongea.

Bwana Rais hulazimiki kutoa sababu unapomuondoa Waziri. Kwa kutafuta kutoa sababu zisizoshiba leo, umeonyesha kwamba umesikia hisia za Watanzania kuhusu kuondolewa January Makamba. Umeondoa Waziri kipenzi cha Watanzania na Waziri weledi. Tunajua umemfukuza kwasababu nyingine, sio uchapakazi. Watanzania wote tunajua kwamba siku zote alikuwa anatafutiwa sababu tu ya kuondolewa. Ukisema uchapakazi ndio sababu Watanzania tunakushangaa kwasababu hawa mawaziri umewateua wewe lakini tathmini tunafanya sisi Watanzania. Na January Makamba ndiye alikuwa Waziri mbunifu na bora kabisa. Na ataendelea kuwa maarufu miongoni mwa Watanzania. Hakika ana nafasi kwenye uongozi siku sio nyingi sana zijazo. Mabadiliko ni lazima na January naamini atakuwa sehemu ya mabadiliko ili kujenga Tanzania inayojali watu wake na yenye Demokrasia iliyokomaa

Zitto ZR Kabwe
Mbunge Kigoma Mjini
Huyu jamaa ni mdini sana, utetezi huu base yake ni kwa sababu mtetewaji dini yake ni sawa na huyu jamaa..anazunguka zunguka kuokoteza vijisababu wala cyo substance kabisa, lengo ni kuonyesha support kumliwaza muumini mwenzie.
 
Nakubaliana na maneno yako ila sidhani kama nakubaliana na makamba
 
Hivi mlitaka raia wote milioni 50 wakemee kupigwa risasi Lissu??? Siwapendi CCM lakini pia sipendi zaidi upumbavu na unafiki wa chadema... yaaani kila tukio LISSU , mazingira Lissu kapigwa risasi , mkiongelea Kilimo Lissu kapigwa Risasi ..asingepigwa Risasi hivi msingekuwa na hoja nyingine!!! Wengine hatuna vyama ila kwa mikumbomikumbo ya Chadema na Upinzani kwa ujumla wao kurukia tu kana ngedere msituni likitoke hili hawaaaa oooh Lissu likitokea lile ooooh Kutekwa ..../ alipigwa Risasi Rais wa Uturuki hadharani mbona maisha yaaendelea??? Kennedy ...., kuweni wabunifu kuendesha chama sio vururuvururu ....hamtakuwa na tofauti na hao CCM
Wanazingua sana kuleta porojo kwenye kila kitu, badala ya kujikita katika kufanya tafiti na kukusanya data, kuzichambua na kisha kuja na comprehensive socio economic policy, itakayo likomboa hili taifa kwenye huu mkwamo wa spidi ndogo ya maendeleo kwa taklibani miaka 40 sasa kijamii,kiujumi na kisiasa.... Ila wao lisu/kutekwa/risasi na kurukiarukia tu hoja, watu makini wanawachoka.

Kuna Mambo mengi Sana wangejikita kuyatungia sera, mfano; Ni aibu leo zaidi 40 years ya Uhuru tunaapisha WAZIRI wa kilimo, ila changamoto za kilimo TZ ni zile zile na hazina hata dalili ya kupatiwa ufumbuzi wala kutatuliwa......
1- uzalisha duni wa mazao ya kilimo(Kuna sababu zake na julikana)
2- ukosefu wa viwanda vya kuchata mazao na kuongeza thamani...
3- ukosefu wa masoko ya uhakika wa mazao yetu na kuendelea kuwa kuwafurahisha wakulima nchini
4- kukosekana kwa msukumo wa dhati wa serikali kukisimia kilimo kwa sera na mipango Bora na endelevu ya kimkakati ili kutatua 1-3 hapo juu..

Sijui hata kwanini tuna wizara na WAZIRI wa kilimo [emoji45][emoji45][emoji45]
 
Membe baki CCM.
January baki CCM.
Nape baki CCM.
Kinana baki CCM.
Makamba Sr baki CCM.

Mkiwa na vinyongo vyenu endeleeni kubaki huko huko mkichochea kuni mpaka 2020.

LISSU rudi haraka Tanzania wakati ni huu, Mbowe kaa chini na ACT mkubaliane pamoja na Seif na akina Jussa na wazanzibar wote, bara asimame LISSU na visiwani kama kawa Maalim na ACT.. CCM kwa hali waliyonayo kuni zikichochewa wanaanguka mapema sana 2020..
Goli la mkono linawezekana vipi kuepukika?
 
Kuanzia tarehe 1 mwezi wa 8 2019
Mifuko ya plastic ruksa?
 
Rais Magufuli kwenye sababu za kumuondoa January Makamba bora jikalie zako kimya.

Nimekusikia Rais leo ukijaribu kuelezea sababu za kumuondoa Uwaziri Bwana January Makamba. Kwa kweli hukuwa umejiandaa na maelezo ya kuridhisha.

Rais, kwenye suala la mifuko ya plastiki tunajua ukweli kwamba wewe ndiye ulizuia lisiendelee ulipoambiwa kwamba litaua viwanda. Tunajua kwamba January ndiye ametumia miaka mitatu kuwaandaa wenye viwanda vya mifuko ili wabadilishe teknolojia na wasipate hasara. Tunajua kwamba January alifanya vikao vya umma (public hearings) kuanzia Karimjee mwaka 2017 hadi Mwanza mwaka 2018 na kwingineko kushirikisha wananchi kwenye jambo hili. Tunajua kwamba hatukusikia kauli yako kwenye mifuko ya plastiki hadi baada ya suala hili kufanikiwa. Hii sio kawaida yako maana wewe ni very predictable.

Tunajua kwamba mlimtegea Makamba ili afeli halafu mumtimue. Hakufeli. Sasa mnamtimua kwa kukamilisha kazi kwa weledi mkubwa! Mhe Rais wewe ni mkali maelekezo yako yasipotekelezwa. Umemuachaje Waziri miaka minne kwa kutotii maelekezo halafu unamtoa baada ya utekelezaji? Hakuna mwenye akili timamu anayeweza kukubali hoja yako hii dhaifu sana.

Bwana Rais ulikutana na wafanyabiashara kote nchini kutwa nzima. Walitaja kero zao zote, nami nikaziorodhesha. Sikusikia hata mmoja akilalamikia NEMC. Kwasababu gani? Kwasababu January ameibadilisha NEMC. Alitaka kuibadilisha huko nyuma na akavunja bodi na kuondoa menejimenti lakini kwakuwa inasemekana kulikuwa na ndugu zako walioguswa ukaagiza uamuzi ule ubatilishwe. Unadhani Watanzania wamesahau?

Bwana Rais fedha zinazotolewa na wahisani kwenye miradi ya mazingira zinakaguliwa na CAG na hakuna popote palipoonyesha ubadhirifu au upotevu. Kama upo uweke hadharani kama sisi tulivyoweka hadharani ubadhirifu wa TZS 1.5 Trilioni. Wacha wahisani, Serikali yako haijaweka hata senti tano kwenye miradi ya mazingira nchini. Mimi ni Mbunge na ninapitia kila Bajeti ya Serikali na Taarifa za CAG. Hujawahi kutenga fedha za Mazingira. Kwa kifupi, tunajua wewe binafsi sio mpenzi wa mazingira na umesema hivyo mara kadhaa. Hata huyo January mwenyewe “ulimtupa” kwenye mazingira ili apotee lakini ghafla kila Mtanzania leo anaongea mazingira. Hata wewe nawe leo unayaongea.

Bwana Rais hulazimiki kutoa sababu unapomuondoa Waziri. Kwa kutafuta kutoa sababu zisizoshiba leo, umeonyesha kwamba umesikia hisia za Watanzania kuhusu kuondolewa January Makamba. Umeondoa Waziri kipenzi cha Watanzania na Waziri weledi. Tunajua umemfukuza kwasababu nyingine, sio uchapakazi. Watanzania wote tunajua kwamba siku zote alikuwa anatafutiwa sababu tu ya kuondolewa. Ukisema uchapakazi ndio sababu Watanzania tunakushangaa kwasababu hawa mawaziri umewateua wewe lakini tathmini tunafanya sisi Watanzania. Na January Makamba ndiye alikuwa Waziri mbunifu na bora kabisa. Na ataendelea kuwa maarufu miongoni mwa Watanzania. Hakika ana nafasi kwenye uongozi siku sio nyingi sana zijazo. Mabadiliko ni lazima na January naamini atakuwa sehemu ya mabadiliko ili kujenga Tanzania inayojali watu wake na yenye Demokrasia iliyokomaa

Zitto ZR Kabwe
Mbunge Kigoma Mjini
Wewe Mrundi hata akili hunaga kabisa. Mbona nimesikiliza speech ya Rais na hakutaja popote kuwa kamtoa waziri aliepo kwa ajili ya uzembe wala nini? Kasema tu changamoto waziri kaziona bahati nzuri na angaongezea machache kama kuhakikisha vibali vinatoka on time na vitu vingine very positive. Ndiyo maana watu hawakupendi kumbe ni tabia zako za kugeuza maneno
 
Sijamsikia popote Rais Magufuli akitaja sababu za kumtumbua January. Ni kama vile unamlisha maneno!
Wewe umelishwa limbwata na muongo. Hata hivyo Watanzania siyo wajinga. Kwani lazima wewe usikie? Pigeni hela ya lishamba la kanda ya ziwa.
 
Kuna Mambo mengi Sana wangejikita kuyatungia sera, mfano; Ni aibu leo zaidi 40 years ya Uhuru tunaapisha WAZIRI wa kilimo, ila changamoto za kilimo TZ ni zile zile na hazina hata dalili ya kupatiwa ufumbuzi wala kutatuliwa......
1- uzalisha duni wa mazao ya kilimo(Kuna sababu zake na julikana)
2- ukosefu wa viwanda vya kuchata mazao na kuongeza thamani...
3- ukosefu wa masoko ya uhakika wa mazao yetu na kuendelea kuwa kuwafurahisha wakulima nchini
4- kukosekana kwa msukumo wa dhati wa serikali kukisimia kilimo kwa sera na mipango Bora na endelevu ya kimkakati ili kutatua 1-3 hapo juu..

Sijui hata kwanini tuna wizara na WAZIRI wa kilimo [emoji45][emoji45][emoji45]

Hiii swala la Kilimo kwa kweli naona kwa sasa kama tunarudi nyuma kuliko kipindi cha Mwalimu, inakuwaje haluna mkakati wa kukiinua Kilimo? Yaani jana ni nafuu kuliko leo.
 
Ulikuwa husikilizi au hukuelewa.

Kasema kwenye wizara yake kulikua na miradi hewa ya kupanda mikoko, matumizi mabaya ya fedha za wafadhili, na marufuku ya mifuko ya plastiki aliichelewesha kwa miaka 4 na hata lilipotekelezwa juzi ni yeye alimlazimisha.

Sijui kama ni kweli au ni kumpaka matope jamaa, Makamba nae katia ngumu, kagoma kwenda Ikulu leo kama watumbuliwa wengine wanavyohudhuria
Sasa unabisha kwamba alimlazimisha?
 
Wanazingua sana kuleta porojo kwenye kila kitu, badala ya kujikita katika kufanya tafiti na kukusanya data, kuzichambua na kisha kuja na comprehensive socio economic policy, itakayo likomboa hili taifa kwenye huu mkwamo wa spidi ndogo ya maendeleo kwa taklibani miaka 40 sasa kijamii,kiujumi na kisiasa.... Ila wao lisu/kutekwa/risasi na kurukiarukia tu hoja, watu makini wanawachoka.

Kuna Mambo mengi Sana wangejikita kuyatungia sera, mfano; Ni aibu leo zaidi 40 years ya Uhuru tunaapisha WAZIRI wa kilimo, ila changamoto za kilimo TZ ni zile zile na hazina hata dalili ya kupatiwa ufumbuzi wala kutatuliwa......
1- uzalisha duni wa mazao ya kilimo(Kuna sababu zake na julikana)
2- ukosefu wa viwanda vya kuchata mazao na kuongeza thamani...
3- ukosefu wa masoko ya uhakika wa mazao yetu na kuendelea kuwa kuwafurahisha wakulima nchini
4- kukosekana kwa msukumo wa dhati wa serikali kukisimia kilimo kwa sera na mipango Bora na endelevu ya kimkakati ili kutatua 1-3 hapo juu..

Sijui hata kwanini tuna wizara na WAZIRI wa kilimo [emoji45][emoji45][emoji45]
Ukishangaa ya Wizara ya Kilimo ..utakutana na Wizara ya Viwanda na Biashara ambao wanatakiwa kumeza mazao ya kilimo, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Technolojia hata halafu kibaya zaidi . Huu muundo wa Serikali zetu za Mitaa na Serkali kuu hazina Muunganiko kabisa ngazi za halmashauri na majiji. Huku afisa biashara anajibu kwa Mweka hazina ambaye yupo Wizara ya Fedha utacheka. Afisa Misitu na Mazingira anajibu kwa Mganga Mkuu wa wilaya DMO ambaye yupo Wizara ya AFyaaaa badala ya kujikita Wizara ya Misitu hapohapo unamleta mENEJA WA TFS , yaani shida sana .... walau Ardhi na Maji kwa sasa wamehamishiwa wizarani moja kwa moja yaani.
 
Tafadhali sana ndugu zito,
Usije ukamshauri bwana January kujiunga na upinzani.

Tunataka abakie huko huko ccm.

Januari usije ukaenda chama chochote ch upinzani.

Usije ukathubutu.

Baki hapo hapo.
Chezeni karata zenu vizuri.

Siku zote wakitaka kumshinda adui basi wanatakiwa wasikimbie uwanja wa vita bali wanatakiwa wabaki humohumo ili ikazi iwe rahisi tofauti na mtu anayetoka nje ya Cycle.
 
Back
Top Bottom