Tetesi: Rais Magufuli Kufanya Ziara Mkoani Kilimanjaro

Tetesi: Rais Magufuli Kufanya Ziara Mkoani Kilimanjaro

Page 94

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
5,204
Reaction score
15,207
Salaam Wandugu,
Kwa taarifa nilizozipata,Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anategemea kufanya ziara Mkoani Kilimanjaro hasa Wilaya ya Siha kuanzia tar 1-9-2016.

Taarifa hizo zinadai atafanya mkutano wa hadhara katika mtaa wa Mji mwema,kijiji cha Roseline, kata ya Ndumeti tarafa ya Siha Magharibi. Na moja ya ajenda itakua ni ujenzi wa barabara kwa kiwango cha Lami kutoka Sanya-Juu kupitia Ngarenairobi mpaka Elerai kuelekea huko Kamwanga.

Je,ziara hii ya Rais itakuwa dawa tosha ya matatizo yanayowasibu Wananchi wa maeneo hayo? Je,wawekezaji wasio na tija katika taifa ukiwepo wa Endarakwai unaweza kutumbuliwa?

Je Mgogoro waArdhi usiokwisha baina ya wafugaji jamii ya Kimaasai na mwekezeji Peter Jones utatolewa ufumbuzi?

Je,ufisadi wa milion 250 zilizoripotiwa kufanywa na Mkurugenzi aliyemaliza muda wake Ndg Rashid Kitambulio na aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la madiwani Mh. Nassari utazungumziwa?

Je,ukodishwaji wa eneo kubwa ardhi kwa matajiri huku wananchi wakilalama wasipate hata pa kukodisha unaweza kupatiwa ufumbuzi?

Yote hayo na mengine mengi tutajua pale atakapowasili Mkuu wetu wa Kaya.

Tusubiri na tutaona.
Msiha.
 
Salaam Wandugu,
Kwa taarifa nilizozipata,Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anategemea kufanya ziara Mkoani Kilimanjaro hasa Wilaya ya Siha kuanzia tar 1-9-2016.

Taarifa hizo zinadai atafanya mkutano wa hadhara katika mtaa wa Mji mwema,kijiji cha Roseline, kata ya Ndumeti tarafa ya Siha Magharibi. Na moja ya ajenda itakua ni ujenzi wa barabara kwa kiwango cha Lami kutoka Sanya-Juu kupitia Ngarenairobi mpaka Elerai kuelekea huko Kamwanga.

Je,ziara hii ya Rais itakuwa dawa tosha ya matatizo yanayowasibu Wananchi wa maeneo hayo? Je,wawekezaji wasio na tija katika taifa ukiwepo wa Endarakwai unaweza kutumbuliwa?

Je Mgogoro waArdhi usiokwisha baina ya wafugaji jamii ya Kimaasai na mwekezeji Peter Jones utatolewa ufumbuzi?

Je,ufisadi wa milion 250 zilizoripotiwa kufanywa na Mkurugenzi aliyemaliza muda wake Ndg Rashid Kitambulio na aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la madiwani Mh. Nassari utazungumziwa?

Je,ukodishwaji wa eneo kubwa ardhi kwa matajiri huku wananchi wakilalama wasipate hata pa kukodisha unaweza kupatiwa ufumbuzi?

Yote hayo na mengine mengi tutajua pale atakapowasili Mkuu wetu wa Kaya.

Tusubiri na tutaona.
Msiha.

Ofisi ya Raisi si ofisi ya kutoa hukumu hadharani kwa mashauri ambayo taratibu za kisheria zinaendelea. Kama kuna Kiongozi anatuhumiwa kwa ufisadi wa fedha za umma mahakama ipo na baada ya kutoa hukumu ofisi inaweza kuchukua hatua za kinidhamu. Pia tatizo la mikataba ya ukodishwaji wa ardhi ni tatizo la kimfumo na wakati taratibu za ukodishaji zinafanyika hatua zote zilipitiwa kama kuna dosari zitabainishwa na wataalamu wa sheria na kuwekwa hadharani si kazi ya raisi kwenda kutoa value judgement kwenye mikutano ya hadhara
 
Ofisi ya Raisi si ofisi ya kutoa hukumu hadharani kwa mashauri ambayo taratibu za kisheria zinaendelea. Kama kuna Kiongozi anatuhumiwa kwa ufisadi wa fedha za umma mahakama ipo na baada ya kutoa hukumu ofisi inaweza kuchukua hatua za kinidhamu. Pia tatizo la mikataba ya ukodishwaji wa ardhi ni tatizo la kimfumo na wakati taratibu za ukodishaji zinafanyika hatua zote zilipitiwa kama kuna dosari zitabainishwa na wataalamu wa sheria na kuwekwa hadharani si kazi ya raisi kwenda kutoa value judgement kwenye mikutano ya hadhara
Naelewa hilo Mkuu,sijasema utatolewa Hukumu! Badala yake kwenye ishu ya Ufisadi wa mil 250 nimeuliza,je Utazungumziwa?

Ishu ya mashamba siyo ishu ya kimfumo. Ni nguvu ya Pesa. Watu wengi wanatoka maeneo mbalimbali na kuja kulima ekari nyingi hata kufikia ekari 100,huku wananchi wakiwa na uhitaji mkubwa tena wapo tayari kulipa kiasi kile kinachohitajika.
 
Sasa Rais akichukua hatua kama unavyotaka mnasema yeye ni "Dikteta" asipochukua mnalalamika, watanzania manataka nini hasa?
Mkuu hebu tuliza kichwa na unambie ni lini Rais kafanya jambo la kimaendeleo alafu ukasikia Mtu anasema ni Dictator? Nadhani upande wa Upinzani wanamuita Dikteta kwa sababu ya kuzuiwa mikutano ya vyama vya Siasa. Siyo kwa sababu nyingine.
 
Ofisi ya Raisi si ofisi ya kutoa hukumu hadharani kwa mashauri ambayo taratibu za kisheria zinaendelea. Kama kuna Kiongozi anatuhumiwa kwa ufisadi wa fedha za umma mahakama ipo na baada ya kutoa hukumu ofisi inaweza kuchukua hatua za kinidhamu. Pia tatizo la mikataba ya ukodishwaji wa ardhi ni tatizo la kimfumo na wakati taratibu za ukodishaji zinafanyika hatua zote zilipitiwa kama kuna dosari zitabainishwa na wataalamu wa sheria na kuwekwa hadharani si kazi ya raisi kwenda kutoa value judgement kwenye mikutano ya hadhara
Ofisi ya Raisi si ofisi ya kutoa hukumu hadharani kwa mashauri ambayo taratibu za kisheria zinaendelea. Kama kuna Kiongozi anatuhumiwa kwa ufisadi wa fedha za umma mahakama ipo na baada ya kutoa hukumu ofisi inaweza kuchukua hatua za kinidhamu. Pia tatizo la mikataba ya ukodishwaji wa ardhi ni tatizo la kimfumo na wakati taratibu za ukodishaji zinafanyika hatua zote zilipitiwa kama kuna dosari zitabainishwa na wataalamu wa sheria na kuwekwa hadharani si kazi ya raisi kwenda kutoa value judgement kwenye mikutano ya hadhara
We we huijui mizuka yake, labda pasiwepo wajambishaji.
 
Tetesi, unataka tujali nini sasa! bora ungetoa taarifa ya hiyo tetesi yako bila kutaja mambo ambayo unatarajia aidha kwa namna moja au nyingine ungependa yaguswe ktk tetesi yako! Any way, ahsante kwa tetesi hiyo!
 
Tetesi, unataka tujali nini sasa! bora ungetoa taarifa ya hiyo tetesi yako bila kutaja mambo ambayo unatarajia aidha kwa namna moja au nyingine ungependa yaguswe ktk tetesi yako! Any way, ahsante kwa tetesi hiyo!
Nimeyataja mambo hayo ili kama ikawa ni kweli basi Mh. Rais apate mwanga kuhusu yanayoelekea Siha. Simaanishi Rais hana hizo taarifa lakini mamo mengine yanaweza kufichwa. Huku naamini wapo wale majamaa na hakika watamfikishia.
 
Mkuu usipotoshe watu, sisi tunapinga kuchezea sheria na katiba kwa kukandamiza demokrasia, kutatua kero za wananchi na ufisadi tunamuunga mkono
Acha uongo wako. Ni lini mlimuunga mkono katika juhudi zake? Lete angalau tamko moja la Chadema. Kila kitu mmekalia kupinga tu, tena bila hata ya kufikiri.
 
magufuli tarehe hyo atakuwa anafungua mkutano wa wakandarasi Tanzania nchini dar es salaaam...
 
Back
Top Bottom