Tetesi: Rais Magufuli 'kuutumbua' Mwenge wa Uhuru

Tetesi: Rais Magufuli 'kuutumbua' Mwenge wa Uhuru

Ili kuenzi historia yetu MWENGE WA UHURU WAWEZA KUKIMBIZWA PALE UWANJA WA UHURU MNAMO TAR. 9 Desember
 
Ifike wakati tuanze kuulizana vyeti vya kuzaliwa maana wenzetu wengine uraia wenu unatia mashaka sana haya mwenge nao umekukosea nini; hivi umewahi kujiuliza sababu zake kwanza za kuanzisha mbio za mwenge au unadhani akina nyerere walikuwa hawana akili timamu. Watu tu wanaacha kuweka symbolism muhimu katika hizi ritual ndio maana wengine mnaleta madharau.

Ni kweli, Mwenge una historia nzito sana. Maneno ya Mwalimu J.K. Nyerere kuhusu Mwenge ni haya: "Tutawasha Mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, umulike mpaka nje ya mipaka yetu, ulete matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale palipojawa na chuki na heshima pale palipojaa dharau" Lakini ukiangalia kwa makini, wakati wake, Nyerere alifanya kweli. Tanzania ilikuwa inawaka nje ya mipaka yake. sisemi kwamba alifaulu alivyotaka, au kwamba hakufanya makosa, hapana, alifanya makosa mengi tu, lakini unaweza kuona alichopanga na alichokusudia na alichofanya. kwa hiyo Mwenge ni ishara ya yale ambayo nchi ilikuwa inafanya.

Lakini hivi sasa sisi kama nchi tunasimamia nini? tumeendesha operesheni kimbunga kuwafukuza "watu wasio raia" ambao kwa hakika ni waafrika wenzetu, isipokuwa ni mkoloni tu ndio alituambia wewe mkongo, wewe mtanganyika, wewe mkenya. wapi misimamo ya umajumui? tumeendesha vituko huko Zanzibar ambavyo tumeviita "uchaguzi wa marudio", nchi inapigwa kila kona huku viongozi wakiongoza upigaji. hapo kuna "kuleta matumaini pale pasipo matumaini"? watanzania tuna matumaini gani kiasi kwamba tuwasaidie na wengine? Kwa kweli kwa mazingira yetu ya sasa, wala hatuhitaji kujifanya tunawamulikia wengine, hivyo zoezi la Mwenge lisitishwe kwanza mpaka hapo tutakapoamua vinginevyo.
 
Hakuna mwenge wala nini kwa sasa,wananchi tuna hali ngum sana ki ukweli. Na vile tumeanza kukataa misaada basi ni bora tu ibaki kua history ili hizo pesa zifae kwa maendeleo ya kujenga nchi. Ila mzee ifikie time asitishe ili ikiwezekana izo ela achimbe ata visima kila mkoa. Na pesa ikipatikana ya ziada basi aipeleke kwenye mashirika mfano tanesco ata ewura ili mafuta yapungue bei coz itakua nafuu kwa mwananchi
 
Baada ya Rais John P. Magufuli kubadili na kuokoa fedha kwenye sherehe za Uhuru na Muungano,sasa Mwenge wa Uhuru uko njiani kutumbuliwa. Taarifa za kishushushu zinaonesha kuwa tayari Rais Magufuli ameitisha faili la Mwenge huo na kupata maelezo ya kutosha na kutisha kuhusu Mwenge huo.

Taarifa zinaonesha kuwa Rais Magufuli ameguswa na kutikiswa na matumizi makubwa yanayofanyika wakati wa mbio za Mwenge nchi nzima. Rais anapanga kutumbua Mwenge huo ambao sasa ni kero badala ya kuwa hero hapa nchini.

Wangapi wanaafiki bila unafiki?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Sisi tumekwisha kuwasha Mwenge,
Tumekwisha kuwasha mwenge. X2
Na kuuweka juu ya mlima,
Mlima Kilimanjaro. X2

Chorus: kuwasha Mwenge, kuwasha Mwenge, na kuuweka Kilimanjaro. X2

Umulike hata nje ya mipaka yetu,
Ulete tumaini. X2
Pale ambapo hamna matumaini,
Upendo mahali ambapo pana chuki
Na heshima ambapo pamejaa dharau. X2

Mwenge upelekwe Mlima Kilimanjaro, upitie Arusha. Magufuli arudishe Azimio la Arusha rasmi.

Call me whatever you want, but I have my values. Kitu kilichokuwa kinafanya kazi iweje kifanyiwe matengenezo?
 
Ni kweli, Mwenge una historia nzito sana. Maneno ya Mwalimu J.K. Nyerere kuhusu Mwenge ni haya: "Tutawasha Mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, umulike mpaka nje ya mipaka yetu, ulete matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale palipojawa na chuki na heshima pale palipojaa dharau" Lakini ukiangalia kwa makini, wakati wake, Nyerere alifanya kweli. Tanzania ilikuwa inawaka nje ya mipaka yake. sisemi kwamba alifaulu alivyotaka, au kwamba hakufanya makosa, hapana, alifanya makosa mengi tu, lakini unaweza kuona alichopanga na alichokusudia na alichofanya. kwa hiyo Mwenge ni ishara ya yale ambayo nchi ilikuwa inafanya.

Lakini hivi sasa sisi kama nchi tunasimamia nini? tumeendesha operesheni kimbunga kuwafukuza "watu wasio raia" ambao kwa hakika ni waafrika wenzetu, isipokuwa ni mkoloni tu ndio alituambia wewe mkongo, wewe mtanganyika, wewe mkenya. wapi misimamo ya umajumui? tumeendesha vituko huko Zanzibar ambavyo tumeviita "uchaguzi wa marudio", nchi inapigwa kila kona huku viongozi wakiongoza upigaji. hapo kuna "kuleta matumaini pale pasipo matumaini"? watanzania tuna matumaini gani kiasi kwamba tuwasaidie na wengine? Kwa kweli kwa mazingira yetu ya sasa, wala hatuhitaji kujifanya tunawamulikia wengine, hivyo zoezi la Mwenge lisitishwe kwanza mpaka hapo tutakapoamua vinginevyo.

Hili ni tatizo kubwa la ninyi wazee wetu wa miaka hii,kweli sisi wa leo ni wapuuzi kama unavyosema ,ila nitakushangaa kutuita wapuuzi wakati ukweli wenyewe wa jambo hamjatuambia ,hivyo kila mtu anatumia hisia zake kuelezea anachokijua ,kama unaujua ukweli na pengine ni siri isiyotakiwa kuwekwa wazi ,ungeheshimu michango ya hawa unaowaita wapuuzi au ungeweka wazi ukweli wenyewe
Mwalimu alifanya kazi kisayansi kwenye kujenga jamii kama ulivyoelezea sababu zake za uwepo wa mwenge. Naambiwa kuna watu vijijini miaka hiyo mwenge ulikuwa ukienda unapokelewa na shamra shamra za ajabu na inakuwa kama sababu ya kukusanyika na kufanya sherehe mpaka unaondoka.

Sasa utamaduni wa aina hiyo sio kwamba watu wanakaa nazo mwaka mzima mwenge ukipita kila mtu anaendelea na yake hila hisia za uzalendo zinakuwa tayari zimeshakuwa implanted ndani mwao at the back f their minds.

Leo mwenge una maana kwa UVCCM tu na wale wanaoukimbiza ndio maana wengi awaoni mantiki kwa nini? kwa sababu serikari aifanyi jitihada zozote za kuuwekea maanani kwenye kuiuza concept ya mwenge, kuujengea umuhimu kitaifa na mambo mengi. Binafsi sikuwahi kuukimbiza mwenge lakini nilikua na hamu ya kuuona na nilikua najua baadhi ya nyimbo zake leo sidhani kama vijana wanazijua nyimbo za mwenge.

Ukienda nchi za wenzetu viongozi wao wakiona watu wanaaza kuwa detached na symbolism and rituals za nationalism, wanaweza kutafuta ata msaada wa makampuni makubwa kama 'Saatchi and Saatchi' wapo tayari kulipa hela wawafanyie market strategy wanaiuza vipi concept.

Vitu aviwezi kuwa na maana baada ya muda mrefu kama jamii inashindwa kuona umuhimu wake; watu wengi awana uzalendo wa vile leo kwanini wasione mbio za mwenge kama upotezaji wa hela tu.

That is enough of a concern hawa jamaa inabidi watafute mbinu mpya za kuuza mwenge kwa kizazi cha leo demographic and perception imebadilika asilimia kubwa kwenye jamii yetu mwenge wameukuta umeshazaliwa na hakuna jitihada zozote zinazotumika kuujengea fikra za propaganda hili ndio tatizo. Sasa tena kuufuta na huo mwenge wenyewe ndio sijui serikari inabaki na tool gani ya propaganda hizi ndio sababu unakuta watu leo wapo loyal either kwa CCM, vyama vya siasa au dini zao; lakini loyalty ya taifa hakuna sana.

Lazima tukubali hivi vitu sio cheap kuviweka lakini faida zake zinatakiwa kujenga uzalendo kama rate inapungua; serikari lazima iangalie wapi inakosea na inarekebisha vipi lakini kufuta ritual za kitaifa sio option kabisa.
 
IMEANDIKWA......."Ole wao wakimbizao mioto na mwenge maana watapata laana vizazi hadi zizazi" .............
Mh.Rais usipate taabu ni nani aliyetuloga.......




Kumbeeeee mkuu kitabu gani hiko nisaidie u.ajua nilikiwa nahisia tu
 
Ndugu wana bodi,
Ningependa wale wote waliokunywa mvinyo wa vyama vyao au hawapo kuwasilisha mawazo na mitazamo yao huru na binafsi nawaomba kwa heshima na taadhima wapite hivi thread zipo nyingi humu JF, huu ni wakati sasa tunajenga Taifa tuko serious.

Nikirudi kwenye hoja ambayo ipo muda mrefu kidogo kuhusu mbio za mwenge kuna mawazo mchanganyiko hapa, kuna wale wanaotaka mwenge uwekwe jumba la makumbusho ubaki kuwa historia tu na kuna ambao wanaona mwenge uendelee lakini uwe kama kifimbo cha malkia ambacho kinakimbizwa kila baada ya miaka minne minne ila sisi tunaweza kuweka miaka sita sita au kumi.

Pia kuna kundi hili la tatu na bila kumung'unya maneno ni kundi la wanufaika wa mchezo huu wa mwenge, ukiwasikiliza hoja yao kuu ambayo ni dhaifu kabisa wanakwambia Mwenge unazindiwa miradi mingi ya maendeleo kana kwamba vile pesa za mwenge ndio zinagaramia ile miradi. Insanity.

Binafsi mimi mara ya mwisho kuchangia mwenge ni utawala wa Mwinyi kwa sababu ilikuwa shuleni ni lazima tuchangie mwenge, lakini kwa sasa kama afisa mtendaji hajipendi basi aje kwangu kunieleza habari za kuchangia mwenge kitakachopata atakuwa sample ya Taifa.

Kwahiyo mwenge umebaki kuwa mradi wa kuwakandamiza walimu kuwachangisha kinguvu (nipo tayari kukosolewa kama wameacha kuwalazimisha kuchangia mwenge) pili kuwandamiza wafanyabiashara hasa mabar maguest , mahotel hasa mikoani maana Dar watu wamepinda hata OCD anaweza kuliwa mitama.

Hivyo basi kwa maoni yangu binafsi kati ya mwenge na muungano mimi naona muungani ni zaidi ya mwenge, sasa najenga hoja kama Rais ameona umuhimu wa kuokoa pesa za kufanya sherehe za muungano kwa mwaka huu ili ziende moja kwa moja kwenye shughuli za maendeleo, je wadau huu si ni wakati muhafaka wa wa Rais kutumia option one kusitisha kwa miaka kadhaa au kuupeleka moja kwa moja jumba la makumbusho for good.

Naomba wadau tuweke mihemko ya vyama pembeni mimi chama changu ni Rais Magufuli, karibuni tuchangie kwa weledi na kwa mdau anayejuwa bajeti ya kukimbiza mwenge ni kiasi gani atuwekee hapa hili Rais apelekewe taarifa sahihi mchwa bado wengi wamemzunguka kila upande. Wale wanaohubiri uzalendo hebu onesheni uzalendo wenu hapa. Ni wakati sasa kila mtu ale kwa jasho lake tu.

Hapa kazi tu.

Cc: Pasco Manyerere Jackton Nyani Ngabu Kiranga
mkuu kwanza binafsi niungane nawe kuwa mwenge hauna manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi, sana sana unaongeza maambukizi ya ukimwi, au ghalama zisizo kuwa na maana, hlo nakubaliana nawe

sasa hoja ni moja kuu, kwa nn mwenge unaendelea kuwepo, watawara huwa wanatoa jib jepesi kuwa ni ishira ya kupata uhuru, na kuonesha kuwa hii nchi ni ya amani, jambo ambalo binafsi haliniingii akilini, anyway tufanye ni kweli lkn faida zake hakuna, matokeo yake imekuwa kitanzi kwa wananchi, hasa wafanyabiashara, waalim na wanakijiji..

nionavyo, kwa kuwa rais anania ya dhati kupana matumizi afanye kubadili hzo sherehe, badala ya kukimbizwa nchi iwekwe kwenye makumbusho mahali ambapo ni katkt kama dodoma, kila mmoja awe huru kwenda pale na kufanya tambiko au kuuona.

mwisho, kunamdau mmoja aliwahi kutoa historia ya mwenge humu jf, kama ni kweli rais wangu magufuri hawezi kuuondoa maana ni zindiko, hakuna namna inabidi tekeleze, sina uhakika kama ataweza kuuondo mwenge, na kama ataweza, hyo ndiyo itakuwa historia kubwa kuliko zote kuwahi kufanyika tz, na huenda akatawala na kuondoka kwa kung,atuka kam alivyofanya nyerere, i mean huenda akafanya kama alivyo fanya mbeki SA..

mwenge ni zaidi ya tuujuavyo....
 
Back
Top Bottom