Rais Magufuli kuvunja Jiji la Dar es Salaam

Hapa tunashindwa kuelewa, kwa mfano Mwanza mjini (kati) kuna wilaya mbili ambazo ni Nyamagana na Ilemela.
Ilemela imepewa hadhi ya kuwa manispaa ya Ilemela, lakini hakuna Manispaa ya Nyamagana badala yake Nyamagana imebeba hadhi ya Jiji la Mwanza.
Katika matukio yote ukisikia wanaongea jiji la Mwanza maana yake wanaongelea wilaya ya Nyamagana na sio mkoa wote.
 
Naona amekiri kwa kinywa chake mwenyewe leo kuwa hawakuchaguliwa.

Hata mwenyewe hilo analijua, na anafahamu hata yeye hakushinda kwa kura 12m+, maana wapiga kura hawakufika hata 10m. Hivyo hao madiwani anawasema hivyo maana ukweli wote anaujua, ndio maana aliwaagiza wanaccm wenzake wasishangilie maana anajua kilichotangazwa sio kilichokuwa kwenye box la kura.
 
Dar es salaam Ni mega city, Sasa sijui katumia kigezo gani kuvunja, Dar es salaam Ni gongromerate city ambayo Ni muungano wa manispaa tofauti.
Mambo haya yalifanyika wakati wa Kodi ya majengo (property tax) kinyume na Sheria ya serkali za mitaa local government Act No. 2 na Property Tax ama Rating Act No .3 ya mwaka 1983. Wakapeleka TRA, Leo wamerudisha kulekule serikali za mitaa. Jiji la bandari Salama ni kongwe toka utawala wa Sultan mpaka leo lilipoondolewa uhai wake. Jiji la Dar es Salaam Ni land Mark kubwa sana, tuheshimu historia sio kila wazo lako litafaa kwa taifa mengine Baki nayo kichwani kwako. Rais ajaye naomba she afute maamuzi haya mchana kweupe.
 
Acha wehu wewe
Kwa hyo ndio 60m?
Wewe kama unampinga NI we
Usiwasemee watanzania wengine huo NI ujinga kqbisa

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Duhh...hivi humu kuna vilaza kiasi hiki!!!??

kwahiyo humu kuna watu tangu wazaliwe wanajua Dar si Mkoa..ila ni Jiji!??

Eeehh.... Hatari. Shuleni mlisomea nini!?? Ujinga!!??
Tulisoma uraiaa
 
nafikiri umemaliza.
 
kwa iyo wazee madiwan walikua wanapiga salio mara mbili kwa mfano diwani wa makurumla akachaguliwa kuwa diwan wa jiji alikua anapiga posho za ubungo na za jiji duuu
 
Mkoa ni mkubwa kuliko Halmashauri ya jiji. Dar kuna mkuu wa mkoa wa Dar (RC), halmashauri ya jiji inaongozwa na Mkurugenzi ambaye yupo chini ya mkuu wa Mkoa.
Vizuri sana sajo umeeleza vyema. Nadhani pia somo la Jiografia na Uraia yafundishwe strictly sasa.

Ukifuatilia unaona uhaba wa maarifa ya Jiografia na Uraia katika wahusika.
 
Dar inabaki kuwa jiji vile vile.

Ila ilala ndio makao makuu ya jiji,temeke na wenzake zinabaki kuwa manispaa.

Mfano arusha ni jiji,lakini manyara kule sio jiji na hawahusiki kuchagua meya wala kuchaguliwa kuwa meya wa jiji
 
Dar inabaki kuwa jiji vile vile.

Ila ilala ndio makao makuu ya jiji,temeke na wenzake zinabaki kuwa manispaa.

Mfano arusha ni jiji,lakini manyara kule sio jiji na hawahusiki kuchagua meya wala kuchaguliwa kuwa meya wa jiji
Dar ni ilala tu, temeke, ubungo, kino na kigamboni hamna tofauti na songea tu
 
Dar inabaki kuwa jiji vile vile.

Ila ilala ndio makao makuu ya jiji,temeke na wenzake zinabaki kuwa manispaa.

Mfano arusha ni jiji,lakini manyara kule sio jiji na hawahusiki kuchagua meya wala kuchaguliwa kuwa meya wa jiji
Manyara ni mkoa unaojitegemea.
 
Yan akivunja maana yake kutakuwa hakuna Dar es Salaam. Au nimeelewaje! Badala yake ilala ndo itakuwa jiji kama sasa tunavosema jiji la dar es salaam. Niko sahihi au.
Mi pia sijamuelewa kabisa Magufuli kuhusu hili.
 
Upuuzi tu wa kuongeza gharama za uendeshaji za Serikali. Husikii huu upumbavu nchi zilizoendelea wa kuongeza idadi ya mikoa au majimbo.
nadhani wakiondoa wale viongozi wa jiji la Dar( anaosema hawana watu wala eneo na hawakuchaguliwa na wananchi) na kubaki na moja ya manispaa ndio iwe jiji,hapa garama za uendeshaji zitakuwa zimepungua siyo kuongezeka...ila jiji la Dar lina sound vizuri kuliko hicho kitu kingine wanachotaka kuanzisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…